St. Paka Mweusi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2010
- 7,632
- 4,512
Wana JF nimekuwa nikijiuliza siku nyingi swali hili na sipati jibu sahihi.Utakuta umempenda mtu unaona ni heri umueleze kilicho moyoni mwako tena kwa upendo na upole tu,lakini matokeo yake majibu utakayokutana nayo inakuwa kama vile ni adhabu,utaambiwa huna adabu,kamtongoze mama yako,utapewa misonyo,pengine hata kichapo toka kwa watu,wengine waliwahi hata kusakiziwa mbwa,na mbaya zaidi unawezakuta mtu hakutaki lakini anaamua tu kukukomesha kwa kukupa shida zake zoote na wewe kwa kuwa umependa basi utamtimizia na bado unaambulia patupu.Mengine tunayokutana nayo wakuu mnaweza kuongezea lakini swali langu ni hilo,je kutongoza ni kosa mpaka wanaume tustahili adhabu zote hizi?