Hivi kuna umuhimu gani wa kuwa na taasisi kama SUMATRA, EWURA nk.kwa mwananchi wa kawaida?

Miwatamu

JF-Expert Member
Oct 2, 2012
1,450
487
Wanajamvi, kama kawaida yangu huwa siishi uchokonozi!! Leo nimekuja na hili baada ya kulitafakali kwa muda. Wakati zinaanzishwa taasisi hizi tuliambiwa kuwa zipo kwa ajili ya kumsimamia na kumtetea mwananchi wa kawaida ili asitwishwe zigo la gharama mbalimbali katika huduma zitolewazo kwa jamii na mashirika au makampuni ya biashara humu nchini. Lakini ukifuatilia kwa kina, utagundua kuwa taasisi hizi zimekuja kuwa mzigo wa nyongeza kwa mwananchi wa kawaida kutokana na ukweli kuwa kila kitu tunachokitumia ambacho wao wanasimamia, sisi hulazimika kuwalipa 1% (Iwe kwa lita au kilo). Lakini ukiangaliwa wao wanatusaidia nini huwezi ona!
Je, ipo haja ya kuendelea kuwepo hizi taasisi? Tulijadili pamoja.
 
Haja ya wao kuendelea kuwepo haipo.Umuhimu wao haujaonekana. Kama nauli bado zinapanda kiholela, umeme, mafuta, maji bado tabu.
 
Sidhani kwamba taasisi hizo zilianzishwa ili kuzuia nauli na umeme visipande....... !
 
Back
Top Bottom