Hivi kuna uhusiano wowote kati ya kuwahi kuuishi umaskini na kuwa kiongozi bora wa kuwaongoza watu kuondokana na umaskini?

The Phylosopher

JF-Expert Member
Mar 11, 2015
1,495
2,043
Mara kadhaa nawasikia viongozi wetu wakitamba kwamba wameuishi umaskini wa watanzania hivyo wanajua cha kufanya ili kuwatoa watanzania kwenye huo umaskini. Ndipo najiuliza kwani aliekulia maisha ya kitajiri hawezi kuwaongoza watanzania kujiapatia maendeleo?
 
Anajaribu kuendana na hali ya maisha ya walio wengi katika umasikini
 
kuna mtu aliwahi kuwajibu watu,kama hamna uwezo wa kununua mikate,nunueni hata keki mle msilale njaa.

Ni vigumu sana kumweleza mtu aliyekulia masaki,kwamba huna pesa ya kula mlo mmoja akakuelewa,atakushangaa na kukuuliza kwanini unakosa?
 
Mtaji wa ccm na viongozi wake siku zote ni Watanzania maskini na wasio na elimu ya uraia. Nashukuru sipo kwenye kundi hilo.

Na ndiyo maana naiombea mabaya ccm siku zote za maisha yangu hapa duniani. Ijifie tu kifo cha mende hata kesho! Nitafanya karamu kubwa na familia yangu.
 
kuna mtu aliwahi kuwajibu watu,kama hamna uwezo wa kununua mikate,nunueni hata keki mle msilale njaa.

ni vigumu sana kumweleza mtu aliyekulia masaki,kwamba huna pesa ya kula mlo mmoja akakuelewa,atakushangaa na kukuuliza kwanini unakosa????
Kuna uzi mmoja humu jamaa aliletaga anashangaa kuna jamaaake mmoja walikuwa wanasafiri sasa huyu mmoka wao akashikwa na haja kubwa, wakasimamisha gari jamaa akajisaidie! Ile jamaa anaenda uwani akarudi mbio anasema hawezi kwakweli...!! Wakamshangaa wakamuuliza kwanini akasema "Hawezi jisaidia choo cha shimo" eeeh jamaa alipigwa na butwaa sana.
 
Back
Top Bottom