Hivi kuna uhusiano wa karibu kati ya kusoma sana (e.g phd, professor, masters) na kipato(income)??

Hapana

Maprofessa ma madakta wa vyuo vikuu wote TZ hawana hela kama kina Chenge, Lowassa, Kikwete, Mramba, Yona, Rostam, Mkapa, Mengi, Manji, Mgonja, Rutabanzibwa nk.

Matajiri wakubwa duniani kama Bill Gates na Larry wa Facebook wali drop out of college.

Tajiri mkubwa kuliko wote TZ Mzee Bakhresa hana elimu.

Hivyo jibu ni hapana.

Ungeuliza kama kuna uwiano kati ya kusoma sana na kuishi maisha mazuri statistically jibu lingekuwa ndio.
 
PhD, Professor, Masters etc si kipimo cha kusoma sana. It's a system and there are ways to work it.

Nilishangaa mtoto mmoja - very smart - anasoma Ph.D ya sayansi ya ubongo at a prestigious college in the field, alipewa kazi ya kuandika habari za chumi za emerging markets na the so called BRICs, na jinsi public policy inavyoweza kunyanyua maisha ya watu masikini. Akawa hana pa kuanzia. Akasema anayemjua ni Muhammad Yunus tu wa Bangladesh ambaye hatafit kwa sababu hakutumia public policy kama elected official. Nikamwambia nenda kasome kazi za Fernando Henrique Cardosso. This was a no brainer, Cardosso being an academic turned president of one of the BRICS, he was bound to have tons of materials fit for this, off the top of my head I gave that name.

Muda si mrefu akanishukuru sana kwa sababu alipata materials kibao, na hata hakumjua president Cardosso. Na sio yeye tu, darasa lake zima la Ph.D walikuwa hawajawahi kumsikia, wanamuuliza "wewe umemsikia wapi huyu?" mtu kawa rais wa Brazil kwa miaka 8, 1995-2003.

Na nikiangalia kweli, wanasoma sana, lakini kila wanavyozidi kusoma ndo wanavyozidi ku specialize kwenye vitu vidogo kiasi kwamba hawana muda na vingine. Enzi za Renaissance men wanaojua mengi zinapita.

Sasa ukiangalia Ph.Ds kama watu wasio na muda wa kuwajua watu kama kina Cardosso unaweza kusema dhana nzima ya kupima usomi kwa Ph.D ni potofu. Unaweza kupima u specialist kwa Ph.D, lakini u specialist na usomi si kitu kimoja.
 
Inategemea Chuo kikuu umesomea digrii, maters na Phd za nini??!!!

Mf. Education (ualimu) ni kifo cha mende, hata ukiwa profesa

Uganga wa kutibu ( kazi kulilia mishahara na rushwa)

Haaaaaaaaaaa

Lakini kwa watu wa biashara, lazima utakuwa tajiri tu!! Bilivu mi, ukiwa na Bcom, then MBA.... Hapo ni ****-make bingo tu, njia nyeupeeeeee

Nimekujibu!!!
 
Sijajua kama unazungumzia utajiri,uhalisia au jinsi ilivyo.
Kwanza kuwa na PhD au masters sio kusoma sana ni kipimo cha elimu ya mtu
Kuhusu uhalisia ni kuwa hakuna mahusiano ya kusoma na kipato kwa kuwa labda niseme ni mazoea tu yametufikisha mahali tunadhani kusoma na kipato vina mahusiano.

Kama unazungumzia utajiri,ni kuwa kuwa na PhD sio kuwa tajiri.Shuleni na vyuoni hatufundishwi kutafuta au kuwa tajiri.Wapo watu hawajaenda hata shule ya msingi lakini wana kipato kikubwa.
Jinsi ilivyo ni kuwa wale "walio soma sana" hulipwa fedha nyingi lakini hii haina maana kuwa ukisoma kwa kiwango fulani ndo utakuwa na kipato kikubwa au utajiri.
 
Elimu haina uhusiano na utajiri, the summit of education is wisdom, sasa wisdom na kujilimbikizia Mali wapi na wapi , always huwa nina tafsiri kujilimbikizia Mali (utajiri) ni ukilaza , ndio maana watu wenye wisdom kama vile mwalimu Nyerere hawakuwa matajiri.
 
Elimu haina uhusiano na utajiri, the summit of education is wisdom, sasa wisdom na kujilimbikizia Mali wapi na wapi , always huwa nina tafsiri kujilimbikizia Mali (utajiri) ni ukilaza , ndio maana watu wenye wisdom kama vile mwalimu Nyerere hawakuwa matajiri.

Naipenda hii.
 
Big NO! Kwani kuna watu wengi sana wanamilki pesa nyingi lakini hata jina lao hawajui kuandika.
Mfano: chukulia wachimbaji na wamiliki wa migodi ya madini hapa nchini unamkuta mtu hajui chochote na darasa halijui kabisa lakini unaambiwa Account yake inasoma DIGITS za hatari kabisa.

Ila ukisoma utaweza kusimamia pesa zako kwa usahihi na kuzifanya endelevu kama utazipata lakini.
 
Juzi wametangazwa list ya matajiri 40 africa wakiongozwa na Aliko Dangote, wote 40 hakuna hata mmoja mwenye masters..

Na bongo napo tukatajiwa list ya matajiri wa 5 wakiongozwa na bakhresa na katika wote watano mwenye masters ni mzee mengi tu wengine wote hakuna kitu lakini ndo wana pesa mbaya..

Kwa wanaotafuta utajiri mkubwa hawawezi kusoma sana as shule inachukua mda mwingi na wao hawana huo muda idle wa kusoma as mda mwingi wanatumia kusaka pesa na utajiri
 
hapana

maprofessa ma madakta wa vyuo vikuu wote tz hawana hela kama kina chenge, lowassa, kikwete, mramba, yona, rostam, mkapa, mengi, manji, mgonja, rutabanzibwa nk.

Matajiri wakubwa duniani kama bill gates na larry wa facebook wali drop out of college.

Tajiri mkubwa kuliko wote tz mzee bakhresa hana elimu.

Hivyo jibu ni hapana.

Ungeuliza kama kuna uwiano kati ya kusoma sana na kuishi maisha mazuri statistically jibu lingekuwa ndio.


vema. Lakini mkuu kama pesa au kipato ni kidogo itakuwaje uishi maisha mazuri yapi hayo kwa standard ipi?
 
I salute your comment sir.
lakini suala langu ni kuhusu hawa maspecialist/wasomi per say mbona life lao sometimes taiti katika mazingira yetu contrary na mategemeo na wanakuwa frustrated sana coz wanaamini elimu itakuwa mkombozi wa maisha au kupata kipato kizuri


PhD, Professor, Masters etc si kipimo cha kusoma sana. It's a system and there are ways to work it.

Nilishangaa mtoto mmoja - very smart - anasoma Ph.D ya sayansi ya ubongo at a prestigious college in the field, alipewa kazi ya kuandika habari za chumi za emerging markets na the so called BRICs, na jinsi public policy inavyoweza kunyanyua maisha ya watu masikini. Akawa hana pa kuanzia. Akasema anayemjua ni Muhammad Yunus tu wa Bangladesh ambaye hatafit kwa sababu hakutumia public policy kama elected official. Nikamwambia nenda kasome kazi za Fernando Henrique Cardosso. This was a no brainer, Cardosso being an academic turned president of one of the BRICS, he was bound to have tons of materials fit for this, off the top of my head I gave that name.

Muda si mrefu akanishukuru sana kwa sababu alipata materials kibao, na hata hakumjua president Cardosso. Na sio yeye tu, darasa lake zima la Ph.D walikuwa hawajawahi kumsikia, wanamuuliza "wewe umemsikia wapi huyu?" mtu kawa rais wa Brazil kwa miaka 8, 1995-2003.

Na nikiangalia kweli, wanasoma sana, lakini kila wanavyozidi kusoma ndo wanavyozidi ku specialize kwenye vitu vidogo kiasi kwamba hawana muda na vingine. Enzi za Renaissance men wanaojua mengi zinapita.

Sasa ukiangalia Ph.Ds kama watu wasio na muda wa kuwajua watu kama kina Cardosso unaweza kusema dhana nzima ya kupima usomi kwa Ph.D ni potofu. Unaweza kupima u specialist kwa Ph.D, lakini u specialist na usomi si kitu kimoja.
 
kwa post ya ndugu kiranga-ambayo nakubaliana nayo- wanaume wasiogope kuoa wasichana wenye PhD. Ni kwaWa

hahaha ni kweli kabisa. nadhani changamoto ya kuoa ibaki kupima uelewa wa mtu husika na maswahiba yake na si kupima kwa mizani ya elimu.
 
katika hili ni more practical hapa nchini. kuna haja ya kutazama upya sera zetu ili ziweke usawa wa fursa kwa maendeleo ya taifa maana sekta zote zina mchango mkubwa sana katika maendeleo ya taifa letu.



Inategemea Chuo kikuu umesomea digrii, maters na Phd za nini??!!!

Mf. Education (ualimu) ni kifo cha mende, hata ukiwa profesa

Uganga wa kutibu ( kazi kulilia mishahara na rushwa)

Haaaaaaaaaaa

Lakini kwa watu wa biashara, lazima utakuwa tajiri tu!! Bilivu mi, ukiwa na Bcom, then MBA.... Hapo ni ****-make bingo tu, njia nyeupeeeeee

Nimekujibu!!!
 
eiyer umejibu vema hasa suala la kwamba shuleni hatufundishwi kutafuta pesa.

lakini nisaidie kwani kuna tofauti kati ya kusoma na kuwa na elimu?



Sijajua kama unazungumzia utajiri,uhalisia au jinsi ilivyo.
Kwanza kuwa na PhD au masters sio kusoma sana ni kipimo cha elimu ya mtu
Kuhusu uhalisia ni kuwa hakuna mahusiano ya kusoma na kipato kwa kuwa labda niseme ni mazoea tu yametufikisha mahali tunadhani kusoma na kipato vina mahusiano.

Kama unazungumzia utajiri,ni kuwa kuwa na PhD sio kuwa tajiri.Shuleni na vyuoni hatufundishwi kutafuta au kuwa tajiri.Wapo watu hawajaenda hata shule ya msingi lakini wana kipato kikubwa.
Jinsi ilivyo ni kuwa wale "walio soma sana" hulipwa fedha nyingi lakini hii haina maana kuwa ukisoma kwa kiwango fulani ndo utakuwa na kipato kikubwa au utajiri.
 
umesomeka mkuu.
kumbe ni optional kusaka noti au kupiga shule kusaka ustaarabu.


Juzi wametangazwa list ya matajiri 40 africa wakiongozwa na Aliko Dangote, wote 40 hakuna hata mmoja mwenye masters..

Na bongo napo tukatajiwa list ya matajiri wa 5 wakiongozwa na bakhresa na katika wote watano mwenye masters ni mzee mengi tu wengine wote hakuna kitu lakini ndo wana pesa mbaya..

Kwa wanaotafuta utajiri mkubwa hawawezi kusoma sana as shule inachukua mda mwingi na wao hawana huo muda idle wa kusoma as mda mwingi wanatumia kusaka pesa na utajiri
 
Huwezi kuwa tajiri kwa kulipwa mshahara au marupurupu ya safari tu, kumbuka wasomi wengi , hasa wa Tz wanachofikiria ni kuajiriwa tu , na haitawezekana kuwa matajiri kwa salary za Tz , japo ukweli bado uko wazi kwamba kimaisha wasomi wana nafuu kubwa kuliko mbumbumbu , bali siku PhD holders wakiamua kukata mizizi ya fitna , kuacha utumwa wa fikra za kuajiriwa na kuamua kuanzisha miradi yao mikubwa ya maendeleo , bila shaka watatisha .
 
Yaani mkubwa tu -unavyozi kusoma(elimika) ndipo unakuwa
1.unajari watu.
2.Sio risk taker maana unajua matokeo.
3.wizi,dhuluma,ufisadi hapana.
Kinyume na hapo lazima utoke.
 
HAZOLE ,hakuna tofauti kati ya kusoma na elimu lakini kuna tofauti kati ya kusoma na kuelimika.Unaweza kusoma halafu usielimike kabisa.
Unapomuona mtu anamuona yule ambae hajasoma kama binadamu nusu huyo hajaelimika japokua anaweza kuwa na PhD.
Unapomwona mtu ana PhD halafu anasubiri aajiriwe ili aendeshe maisha huyo hajaelimika.
Kuelimika ni kupata ufahamu kuhusu wewe na binadamu wenzako.Kupata mbinu za kuendesha maisha yako na jamii uliyopo kwa urahisi bila kikomo.
Ni ajabu sana unakuta unaibuka ugonjwa tunasubiri "wataalamu" kutoka nje waje wafanye utafiti wakati wapo wanaojiita wataalam tena wengi.
Yapo matatizo na changamoto nyingi ambazo tungeweza kupata ufumbuzi kwa hao wasomi kufanya tafiti zitakazopelekea kupata majibu,lakini hakuna kipya,wamebaki kulalamika bila aibu.
Hayo ni matokeo ya kutokuelimika pamoja na kupoteza muda mwingi na fedha kwenda shule !!
 
Last edited by a moderator:
duh kweli mzee


Yaani mkubwa tu -unavyozi kusoma(elimika) ndipo unakuwa
1.unajari watu.
2.Sio risk taker maana unajua matokeo.
3.wizi,dhuluma,ufisadi hapana.
Kinyume na hapo lazima utoke.
 
Back
Top Bottom