Elections 2015 Hivi kuna mtu mwenye akili timamu atakayempigia kura yake Magufuli na kumuacha Lowassa?

Ilikuwa orodha ya watuhumiwa wa ufisadi na si mafisadi. Lowassa ameshasema yeye hausiki na mhusika ni Kikwete. Hivyo Lowassa anatolewa rasmi kwenye listi ile ya watuhumiwa na mtuhumiwa hapa ni Kikwete.

Hata kwenye kutajwa kwa Lowassa kwenye maeneo mengine ukiacha Richmond bado ni kumtuhumu tu. Serikali iliyokuwepo madarakani wakati huo ilikuwa na jukumu la kumburuta mahakamani ili ajibu tuhuma kama zilikuwa na ushahidi wa uhusika wake kwenye matukio hayo. Kwa nini haikufanya hivyo?

Kama kweli Lowassa alihusika katika wizi anaoutuhumiwa, basi Serikali ya wakati huo nao ni wezi kwa kushindwa kumchukulia hatua kama walikuwa na ushahidi kwa sababu huwezi kumuacha mtu anaiibia Serikali mabilioni ya pesa bila kuchukua hatua yoyote kama wewe mwenyewe sio mwizi.

Sasa kwa issue ya Magufuli hii iko wazi kabisa kwamba kuna ushahidi wa kitaalam uliotolewa na CAG kwamba alitunga mradi hewa wa ujenzi wa barabara na kuupatia namba hewa ili kuiba mabilioni ya walipa kodi.

Inaingia akilini namna gani mtu ambaye amethibitishwa kuwa mwizi wa mali ya umma aliyekubuhu kwa kudanga mradi pamoja na namba ya mradi ndio huyo CCM inatuletea eti tumpigie kura ya kuwa Rais wa Tanzanina?

Kama aliweza kuiba mabilioni wakati akiwa waziri, ni wazi kwamba ataiba matrilioni akiwa rais tena bila kutunga uongo wa kuhalalisha wizi wake bali atakwapua mchana kweupe bila justification yoyote ile hata ya uongo.

Kwa nini CCM watuletee mwizi aliyekubuhu kwenye kinyang'anyiro cha mgombea urais? Bila shaka ni kwa sababu waliompigia debe ili agombee ni wezi wenzake ili waendelee kuliibia taifa hili kupitia mgongo wa mwizi mwenzao atakapoingia ikulu.

Watanzania mumuogope Magufuli kama Ebola ama sivyo nchi itafilisiwa kabisa katika kipindi chake cha mwaka mmoja tu.

Hata wale Team ya Ushindi si umeona majina yaleyale ya mfumo uleule. Kwa lugha nyingine pamoja na ukweli kwamba Dr Magufuli ni jembe, sioni namna bora atautosa mfumo ambao tayari umeshaundwa! Akitaka afanikiwe awatose na afanye mambo yake. Haki ya Mungu akitoa fadhila tu ndo mwanzo wa yeye kuyumba( hii ni endapo Magufuli akishinda). Anatakiwa awe bandidu kama Rais wa Malawi au Zambia kama sikosei. Wale wote wa chama chake aliwatosa akaunda team mpya. Hivyo washauri wa Magufuli kama akishinda na kuendelea kukumbatia watu walewale, atakuja kushangaa analaumiwa tu.
Hata huyu mheshimiwa anaemaliz muda wake wanamtandao ndiyo wamechangia kumpotosha na kumyumbisha kuja kushangaa madudu lukuki!
 
Ilikuwa orodha ya watuhumiwa wa ufisadi na si mafisadi. Lowassa ameshasema yeye hausiki na mhusika ni Kikwete. Hivyo Lowassa anatolewa rasmi kwenye listi ile ya watuhumiwa.

TUNAENDELEA. Hili ndo jibu pekee nililohitaji the rest was simply inconsequential.

Kumbe ni watuhumiwa tu? Toka lini mmegundua kuwa ni watuhumiwa na siyo mafisadi kama mlivyokuwa mnaimba?

Sasa rudini pale pale Mwembeyanga mkayaseme haya mtupe na sababu ni kwa nini mliamua kutudanganya na kwa manufaa ya nani.

Na kama mlitudanganya basi mtushawisi upya kwamba mtakachotuambia tena hakitakuwa uongo otherwise tuwapuuze milele.

Hivi wewe mtu akikuambia tu hahusiki halafu anakutajia mtu mwingine bila hata kuweka ushahidi wowote unakubali?

Unakuwa una akili kweli?

Halafu ni wapi alimtaja Kikwete kama mhusika? Weka clips kama unazo.

Alichokisema ni mamlaka za juu na kwa sisi walokole hakuna mamlaka za juu duniani instead iko mbinguni tu.

Sasa kama hakukubaliana na hiyo mamlaka kwa nini hakuachia ngazi?

Twende taratibu.
 

KILIMANJARO , ARUSHA NA MANYARA- WALISUSA KUJIANDIKISHA BVR- LOWASA ATAISOMA NUMBER.

MKUKI WA KULENGEA HUU HAPA; ASUBUHI NA MAPEMA ; CCM BIASHARA WALISHAMALIZA.

UKANDA WA KASKAZINI WAMEMSUSA SASA WA NN HUKU


DSC01009.jpg

Sasa una quote post yangu halafu unaweka utumbo huu ambao hata hauhusiani na points zilizopo kwenye post yangu!!! Jibu hoja au kaa kimya. Anzisha thread yako upost huo utumbo wako.

Hapa tunajadili masuala nyeti ya mustakabali wa taifa letu na kuweka hoja kwa nini Magufuli HAFAI KUINGIA IKULU HATA SEKUNDE MOJA. Jibu hoja hizo kama unataka kuchangia kwenye post hii.
 
Magufuli mwiziiii?????
Sababu kama hizi ndo zanifanya nione watu ni wanafiki na hawana hoja! Lowasa na magufuli ni nani anayesemekana ni mwizi??
 
Ukweli ni kwamba Lowassa atamletea Magufuli upinzani mkali, ila Magufuli ataibuka kidedea! Ukweli ni mchungu kwa watu ila ndo ukweli wenyewe huo!
 
TUNAENDELEA. Hili ndo jibu pekee nililohitaji the rest was simply inconsequential.

Kumbe ni watuhumiwa tu? Toka lini mmegundua kuwa ni watuhumiwa na siyo mafisadi kama mlivyokuwa mnaimba?

Sasa rudini pale pale Mwembeyanga mkayaseme haya mtupe na sababu ni kwa nini mliamua kutudanganya na kwa manufaa ya nani.

Na kama mlitudanganya basi mtushawisi upya kwamba mtakachotuambia tena hakitakuwa uongo otherwise tuwapuuze milele.

Hivi wewe mtu akikuambia tu hahusiki halafu anakutajia mtu mwingine bila hata kuweka ushahidi wowote unakubali?

Unakuwa una akili kweli?

Halafu ni wapi alimtaja Kikwete kama mhusika? Weka clips kama unazo.

Alichokisema ni mamlaka za juu na kwa sisi walokole hakuna mamlaka za juu duniani instead iko mbinguni tu.

Sasa kama hakukubaliana na hiyo mamlaka kwa nini hakuachia ngazi?

Twende taratibu.

Usiwe na wasiwasi. Tutaenda taratibu.

Kwa nini majina yale yalitajwa pale Mwembeyanga kama mafisadi? Ili vyombo vya sheria viweze kuwashughulikia na hivyo kuthibitisha au kutothibitisha ufisadi wao. Kwa nini vyombo vya sheria havikufanya hivyo wakati mabilioni ya pesa yalishathibitishwa kwamba yamepotea na kilichokuwa kimebaki ni kuthibitisha nani aliyeingia nayo mitini? Ni kwa sababu Serikali ya CCM haikuwa na nia ya kuliona suala hilo linaenda mahakamani kwa sababu wanafahamu kwamba wezi ni wao wenyewe Serikali.

Sasa suala la mamlaka ya juu kwa mazingira yale ya aliyokuwa anayasemea Lowassa akiwa kama Waziri Mkuu ni lazima iwe ofisi ya Rais. Ndio mamlaka ya juu ya Waziri Mkuu. Hayo ya mbinguni sioni mantiki yoyote ya kuyaingiza hapa kwani tunazungumzia mambo ya wanasiasa na sio viongozi wa dini.

Suala la kuachia ngazi ni suala jingine tofauti kabisa ambalo haliingiani na maudhui ya post yangu ambayo inaonyesha jinsi Magufuli alivyokuwa mwizi aliyekubuhu kwa kuiba hela za walipa kodi kwa kutunga mradi wa uwongo bila haya, wizi ambao umethibitishwa na CAG.

Lakini sio kila siku mtu unaachia ngazi kama hukubaliani na mamlaka fulani kwani wakati mwingine unapoteza fursa ya kuweza kupata nafasi ya kufikia kwenye ngazi hiyo usiyokubaliana nayo ili uweze kupata fursa ya kurekebisha yale ambayo uliyoyaona ni mabaya. Ndicho alichokifanya Lowassa. Akaamua kukaa kimya na baadaye akakubali kujiuzulu baada ya kushinikizwa kufanya hivyo ili asipoteze nafasi yake ndani ya chama ya kurudi tena na kugombea nafasi ya juu ndani ya chama chake ambacho amechangia mno kukijenga tangu ujana wake.

Sasa na wewe tueleze. Kama yeye ndie alihusika katika wizi ule wa Richmond, kwa nini Kikwete hakumburuta mahakamani ili arejeshe hela za walipa kodi pamoja na kutumikia kifungo kinachoendana na kosa lake la wizi wa mali ya umma na badala yake ameamua kutumia hiyo issue ya Richmond kama karata ya CCM ya kumuengua Lowassa kwenye kinyan'ganyiro cha Urais kwa kumpachika majina ya fisadi, asiye na maadili, n.k.?
 
Siku nitakapomsikia Dr. Slaa akimsafisha mamvi ndio nitaelewa hichi ulichoandika.

Queen Esther

Nauliza swali hilo kwa kigezo kimoja tu nacho ni wizi wa mali ya umma.

Lowassa anatuhumiwa kwenye wizi wa Richmond bila ushahidi wowote ule mpaka sasa. Wanaomtuhumu ni walewale ambao wanaoweza kuwa na ushahidi ambao kama kweli alikwapua basi walitakiwa wawe wameshamburuta mahakamani tangu wakati ushahidi ulipopatikana kama kweli wanauchukia wizi wa mali ya umma na kama kweli wao wenyewe sio wezi.

Magufuli sio tu anatuhumiwa bali kuna ushahidi wa kitaalam uliotolewa na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) ukimuhusisha na taarifa za uongo za kudai mabilioni ya pesa yametumika kujenga barabara wakati sio hivyo. Ni wazi kwamba Magufuli kakwapua hizo hela na hivyo HAFAI KUKAA IKULU HATA SEKUNDE MOJA.

Sasa jiulizeni hivi CCM imeshindwa kuja na mgombea wake ambaye sio mwizi? Kwa nini waweke mgombea ambaye ni mwizi kama wao wenyewe sio wezi?

Kifupi ni kwamba Magufuli atapigiwa kura tu na wezi wenzake wanaoliibia taifa hili usiku na mchana bila kunawa na hivyo kulifanya taifa hili lenye rasilimali lukuki kuendelea kuwa taifa masikini.

Watanzania wote wenye uchungu na nchi yao kama wamepewa kuchagua wa kumpigia kura kati ya mtu anayetuhumiwa tu bila ushahidi wowote na ambaye ameshathibitishwa kwamba ni mwizi na taasisi maalum yenye utaalamu kuhusu uthibitishaji huo basi watapiga kura kwa yule ambaye hajathibitishwa kwamba ni mwizi.

Je wewe kura yako iko kwa nani kati ya hawa wawili?
 
Nauliza swali hilo kwa kigezo kimoja tu nacho ni wizi wa mali ya umma.

Lowassa anatuhumiwa kwenye wizi wa Richmond bila ushahidi wowote ule mpaka sasa. Wanaomtuhumu ni walewale ambao wanaoweza kuwa na ushahidi ambao kama kweli alikwapua basi walitakiwa wawe wameshamburuta mahakamani tangu wakati ushahidi ulipopatikana kama kweli wanauchukia wizi wa mali ya umma na kama kweli wao wenyewe sio wezi.

Magufuli sio tu anatuhumiwa bali kuna ushahidi wa kitaalam uliotolewa na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) ukimuhusisha na taarifa za uongo za kudai mabilioni ya pesa yametumika kujenga barabara wakati sio hivyo. Ni wazi kwamba Magufuli kakwapua hizo hela na hivyo HAFAI KUKAA IKULU HATA SEKUNDE MOJA.

Sasa jiulizeni hivi CCM imeshindwa kuja na mgombea wake ambaye sio mwizi? Kwa nini waweke mgombea ambaye ni mwizi kama wao wenyewe sio wezi?

Kifupi ni kwamba Magufuli atapigiwa kura tu na wezi wenzake wanaoliibia taifa hili usiku na mchana bila kunawa na hivyo kulifanya taifa hili lenye rasilimali lukuki kuendelea kuwa taifa masikini.

Watanzania wote wenye uchungu na nchi yao kama wamepewa kuchagua wa kumpigia kura kati ya mtu anayetuhumiwa tu bila ushahidi wowote na ambaye ameshathibitishwa kwamba ni mwizi na taasisi maalum yenye utaalamu kuhusu uthibitishaji huo basi watapiga kura kwa yule ambaye hajathibitishwa kwamba ni mwizi.

Je wewe kura yako iko kwa nani kati ya hawa wawili?

We hujui demokrasia
 
Low hasa atopata kabisa kura yangu
Vigezo
1.Afya mbovu
2.sio mwadilifu
3.tamaa ya madaraka
4.mbadhilifu
5.anatumia pesa kununua wapga kura
Gud example ni chuoni kwe2 udom tumegegeda hela zake nimenunua plate 2 za jiko la gesi na samsung oven,hvyo
HAFAI ATABAKI KUWA LOW TENA HASA
 
Naona kama swali liko kinyume. Nadhani wa kupimwa akili ni atakayempigia Lowasa mtu ambaye Chadema walihifadhi ushahidi wa ufisadi wake kwa miaka 8 lkn wakamsafisha kwa wiki moja na kubadili agenda eti ni "mfumo". Mfumo ni nini kama sio lowasa, mbowe na mtei nk? (WATU).
 
Lowassa mpango wa Mungu lazima aingie IKULU mwaka huu mtake msitake wajinga wakubwa mnaongelea mambo ya wizi cha muhimu ni mabadolilo team UKAWA ndio watakaoendesha nchi wamemtumia EL kuoondoa ccm madarakani na hakuna atatayezuia mabadiloko haya mambo ya afya peleka hayahusiani na maendelea ya nchi hii kama hamtaki mabadiliko mkale malimao na mafisadi wenu ccm watesi na waonevu wakubwa.
 
mimi bahati mbaya si mhafidhina..
si muoga wa mabadiliko..
ukiona mke miaka 50 anakuzalia vichaa na magoigoi..
usiogope kujaribu mke mwengine..
huenda ukapata magenious na hata usipopata..
you have made a progress in an adventure where a step forward is more meaningful.
 
Low hasa atopata kabisa kura yangu
Vigezo
1.Afya mbovu
2.sio mwadilifu
3.tamaa ya madaraka
4.mbadhilifu
5.anatumia pesa kununua wapga kura
Gud example ni chuoni kwe2 udom tumegegeda hela zake nimenunua plate 2 za jiko la gesi na samsung oven,hvyo
HAFAI ATABAKI KUWA LOW TENA HASA

Siku hizi hakuna shule. Vijana mnaingia tu madarasani kutimiza wajibu. Sasa hapo unajibu hoja yangu au unajaza tu server.
 
Naona kama swali liko kinyume. Nadhani wa kupimwa akili ni atakayempigia Lowasa mtu ambaye Chadema walihifadhi ushahidi wa ufisadi wake kwa miaka 8 lkn wakamsafisha kwa wiki moja na kubadili agenda eti ni "mfumo". Mfumo ni nini kama sio lowasa, mbowe na mtei nk? (WATU).

Kama ushahidi ulikuwepo kwa nini Serikali isimburute mahakamani? Mbona mnashindwa kujibu swali rahisi sana? Hela zile zimeibiwa Serikalini zikiwa hela za walipa kodi. Anayetakiwa kuwa na uchungu wa wizi ule kwanza ni Serikali kwa sababu yenyewe ndio imepewa dhamana ya kulinda na kutumia vyema kodi za wananchi. Sasa iweje wamuache Lowassa apete na hela za wizi wa mali ya umma mtaani kipindi chote hicho mpaka leo?

Mimi sijadili CHADEMA hapa wala CCM. Nawajadili watu wawili ambao ni Lowassa na Magufuli ni nani mwenye afadhali kulinganisha na mwingine. Na nimeelezea jinsi wizi wa Magufuli ulivyo wazi na wenye vithibitisho ukilinganisha na tuhuma kwa Lowassa.

Sasa hii ndio hoja inayotawala post yangu hii na wanaojikita kwenye post hii waji confine kwenye boundaries za theme ya post hii na si vinginevyo.
 
Siku hizi hakuna shule. Vijana mnaingia tu madarasani kutimiza wajibu. Sasa hapo unajibu hoja yangu au unajaza tu server.

Ubaya wa watu wa ukawa muchknow sana. Yani wanajua kila kitu na wakisema nyoka ni mbuzi basi mkubali tu. Acha kilatu apige kura yake kwa yule anaempenda yeye sio kujifanya unajua sana kujaji mambo.
 
Sasa una quote post yangu halafu unaweka utumbo huu ambao hata hauhusiani na points zilizopo kwenye post yangu!!! Jibu hoja au kaa kimya. Anzisha thread yako upost huo utumbo wako.

Hapa tunajadili masuala nyeti ya mustakabali wa taifa letu na kuweka hoja kwa nini Magufuli HAFAI KUINGIA IKULU HATA SEKUNDE MOJA. Jibu hoja hizo kama unataka kuchangia kwenye post hii.

DSC01009.jpg
 
Sifikirii kama kuna mtanzania yeyote mwenye akili timamu anaweza kumpigia kura fisadi Lowassa ambae kwa zaidi ya miaka 8 amekuwa akipewa tuhuma za ufisadi na viongozi ambao walituaminisha kuwa ni fisadi halafu leo kwa miezi mitatu tu wanataka kutuaminisha kuwa fisadi Lowassa ni mtu safi. Kwa kweli watanzania hasa wale wazalendo tunataka mabadiliko, lakini si haya ya kununuliwa na mafisadi tunaowajua kwa zaidi ya miaka 8 na kujaribu kuwasafisha kwa miezi 3.
 
Kama ushahidi ulikuwepo kwa nini Serikali isimburute mahakamani? Mbona mnashindwa kujibu swali rahisi sana? Hela zile zimeibiwa Serikalini zikiwa hela za walipa kodi. Anayetakiwa kuwa na uchungu wa wizi ule kwanza ni Serikali kwa sababu yenyewe ndio imepewa dhamana ya kulinda na kutumia vyema kodi za wananchi. Sasa iweje wamuache Lowassa apete na hela za wizi wa mali ya umma mtaani kipindi chote hicho mpaka leo?

Mimi sijadili CHADEMA hapa wala CCM. Nawajadili watu wawili ambao ni Lowassa na Magufuli ni nani mwenye afadhali kulinganisha na mwingine. Na nimeelezea jinsi wizi wa Magufuli ulivyo wazi na wenye vithibitisho ukilinganisha na tuhuma kwa Lowassa.

Sasa hii ndio hoja inayotawala post yangu hii na wanaojikita kwenye post hii waji confine kwenye boundaries za theme ya post hii na si vinginevyo.

Unauliza kushtakiwa kwa Lowassa? Teh teh teh Butiku ameshawajibu hilo swali, acheni kushabikia ujinga hiv kumbe huwa mnabwabwaja tu humu JF bila kufatilia haya mambo kwa kina.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom