Hivi kuna mahusiano kati ya umaskini na kukosa utu!!!!!

Terminator

Member
May 27, 2009
32
10
nimekuwa nashangazwa sana na akili za watu kutokana na matendo ambayo binadamu hufanya, maana katika maisha kuna binadamu wameamua kuishi katika aina fulani ya maisha, mfano mwizi au jambazi, ushoga, mlevi wa kupindukia,na mambo mengine mabaya kama hayo ambayo watu hao ndio identity yao katika jamii.watu wa aina hii sio wa rahisi kuwashangaa kwa sababu ni tabia zao ambazo zinatambulika katika jamii.

ila hili la mtu ambaye usiye mtegemea kuvaa ukichaa na kufanya mambo ambayo yanaishangaza jamii, nasema hivyo kutokana na wimbi lilivyo sasa kwa mtu yeyote anaemiliki gari,kwa sasa ikitokea umepata ajali aidha uwe umesababisha au umesababishiwa na unakuwa katika wakati mgumu kutokana na watu wa maeneo utakapopata ajali kukosa utu, huwezi pata msaada wa watu kukuokoa ,kinachofanyika ni wizi kwanza mengine baadae kwa wale wenye utu ila asilimia kubwa ya watu hukimbilia mali na hata kama una vitu kama dhahabu unaweza katwa sikio au mkono ilimradi mhusika apate mali,

tabia hii kwa kweli inakera sana, maana hujui nini kitakutokea wakati wowote uwapo safarini. mfano kuna jamaa yangu wa karibu alibanwa na lori njiani ikabidi atanue kuepusha ajali akaenda kumgonga mwendesha pikipiki, kwa bahati mwendesha pikipiki alipata michubuko ila sasa,mwenye gari aliyegonga alitaka asimame ili kutoa msaada na pia kusubiri askari wapime,ila kilichotokea ni raia walianza kurusha mawe kwenye gari jamaa aliamua kuondosha gari yake kunusuru maisha yake.kwahiyo kilichoendelea ule msaada wa kumpeleka hospitali hakuwepo tena,pia gari husika halikupatikana tena.

pia hili lililotokea karibuni kwa marehemu sharo milionea, yaani limenikera sana watu badala ya kumsaidia waliamua kumvua nguo maana anaona kama kumpiga sachi anachelewa bora aondoke na nguo aende kuzikagua mbele ya safari. kitendo hicho ni cha kidhalilishaji, aidha namshukuru mkuu wa wilaya ya muheza kwa maamuzi aliyochukua ya kuwatafuta wote waliohusika katika kitendo hicho, na ninaamini watapatikana maana wote ni wakazi wa eneo hilo.

kwa hiyo hali hii ndio maana nashindwa kujua ni umaskini wetu umeondoa utu wetu badala ya kusaidia majeruhi au marehemu, mtu anakimbilia mali. hata utambuzi wa mhusika unakuwa mgumu kutokana na document muhimu za mhusika kuwa zimeibwa.


watu hawa ni ndugu zetu na wanahudhuria misikitini na makanisani,ila matendo haya kweli ni kinyume na maandiko tunayosoma.
 
Watu wamekuwa desperate ndugu yangu. Imefika mahali mtu anajisikia hakuna alichobakiza cha kupoteza. Ndo maana bob marley akasema:
they keep us hungry,
and when you gonna get some food,
your brother ought to be your enemy,
ambush in the night!
 
ikuna matajiri wamekosa utu kuna maskini wamekosa utu so this things sometimes proved to work perpendicular
 
kama viongozi hawana uzalendo utegemee nini kwa wananchi waliokata tamaa ya maisha.!
 
Things were meant to be used and people to be loved ila kwa dunia tunayoishi vitu ndo vinapendwa watu ni wa kutumiwa.
 
"Behaviours are motivated by people so as to meet their basic needs" Glasser (1965).
Ukiona mtu anafanya jambo fulani, anafanya hivyo ili kutimiza hitaji lake la msingi. 'Hitaji la msingi' ina maana kubwa sana. Kwa mfano, malazi ni hitaji la msingi, swali linakuja, je malazi (nyumba) ya aina gani? Na je iwe ya ubora gani?
Watu wote wanaofanya uhalifu, wanafanya hivyo ili kutimiza mahitaji yao ya 'msingi', kwa kuwa kutimiza mahitaji hayo hakukuwezekana, hivyo Id ikazidi Ego na Super-ego.. Ikumbukwe hata utulivu wa akili ni hitaji la msingi kwa binadamu.
 
Umasikini ni tatizo kubwa sana na kwa sababu unaendana sana na kukosa elimu , mahali ambako busara hupatikana , maana bila elimu hakuna busara , ndiyo maana mimi nimeamua kuupiga vita kabisaaa ! Na wanangu wote shule ( A must )
 
Kuna uhusiano
Umasikini kama hali ya kifikra (unaweza ukawa umezungukwa na mali lakini ukawa hujui) unaambatana kwa karibu sana na kukata tamaa.
Mtu aliyekata tamaa hawezi kuwa na utu.
Ndiyo maana dini nyingi zinapiga vita binadamu kukata tamaa.
 
umaskini na kukosa utu kuna uhusiano mkubwa kwani mtu akishakuwa maskini yupo tayari kufanya lolote kupata yale anayoyakosa wakati mwingine inapelekea kufanya vitendo vya ukosefu wa utu kwa binadamu wenzake,
mfano mtu kapata ajali anatokea mtu mwingine ambaye hata mkate wa siku hiyo hana baada ya kuwaza kumsaidia yule mpata ajali anaanza kumuibia na kula kona. laiti kama angekuwa na uwezo wake wazo hilo la kumuibia au kummalizia kabisa ili amuibie pengine lisingekuwapo angemsitiri na kumsaidia na kumuhifadhia vilivyo vya thamani vya aliyepata ajali.
hivyo tunaona kuwa umaskini umesababisha kukosekana na utu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom