Acha utoto ushaonyeshwa mti unaoweza kutibu kuwashwa afu unaleta porojo kwa nini usiumwagilie huo mti ili uendelee kustawi.Ama unapenda kuwashwa pia kuna njia nyingine za kukutibu pia.Asante mkuu... haya majani yapo mengi sana huku nilipo, upupu nao ni mwingi sana pia ila hapo changamoto ni mbili
Kwanza upupu unakuwa umekomaa kipindi cha kiangazi na ndio unakuwa unawasha haswa hata upepo tu ukivuma hapa kijijini kama mtu hakufunga madirisha basi kesho asubuhi atasimulia kilichompata usiku... lakini majani hayo kipindi hicho ni adimu maana yenyewe yanashamiri kipindi cha mvua
Pili ni kwamba hata nikiyapata hayo majani shughuli itakuja kwenye mtu wa kumfanyia majaribio hahahaaa