KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 26,213
- 56,849
Wiki iliyoisha tu kuna msela wangu kaachwa akawa analalamika mpak kulia! Kiberenge wa watu ndo kwanza sielewi nikawa namcheka naona huyu nae anajitafutia visa tu!
Yalayalayala!! Kumbe jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza na hata yule muhenga aliesema "usiombe yakakukuta" yaonyesha yalimkuta makubwa!.. wiki hii ikawa yangu kiberenge wa watu sina hata raha huku sio kutoswa ni kuteseka sasa! Nimeamka asubuhi hata sijakaa sawa nikaona sms yake ati "SIKUTAKI TENA!" nikajua mbwembwe zake tu kumpigia si akapokea jamaa linaniambia "Mkuu mpaka umeseviwa BATA bado unatafuta nini kwa huyu mwanamke!!" Simu ikakatwa hapohapo nikapatwa na kiu mixer mkojo kwa wakati mmoja!.
Baadae kupiga tena akapokea Sasa kitesa roho wangu! Nikaanza mlaumu na kulalamika jibu nililojibiwa ni "Bwana ee tafuta wa kumpa hayo mapenzi yako ya kibatabata!" Simu ikakatwa kupiga tena nakuta nishachezeshwa buloku pande zote.. haikutosha nikaamua nimfate ana kwa ana si nikakutananae aniambie hata sababu ya kuniacha,nilichoambulia nilichekwa halafu akaondoka ila kwa mbali nikasikia neno kama akisema "nimekuacha na uwabata wako" anyway sikusikia vizuri ila nikaona isiwe tabu nami nivunge nisimtafute!
Sasa tabu ipo hapo kwenye kuvunga! Jamani mapenzi yanauma nyie yani maumivu nayoyasikia sijui hata yanatokea wapi ila nachosikia yani mgongo unakuwa wamotooooo halafu Kama unafinywafinywa! Kichwa kimeshaparanganyika hapa nimejikuta nalia huku nimesimama lakini machozi yanaelekea masikioni!!
Mapenzi si kitu cha mchezo jamani😪
Yalayalayala!! Kumbe jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza na hata yule muhenga aliesema "usiombe yakakukuta" yaonyesha yalimkuta makubwa!.. wiki hii ikawa yangu kiberenge wa watu sina hata raha huku sio kutoswa ni kuteseka sasa! Nimeamka asubuhi hata sijakaa sawa nikaona sms yake ati "SIKUTAKI TENA!" nikajua mbwembwe zake tu kumpigia si akapokea jamaa linaniambia "Mkuu mpaka umeseviwa BATA bado unatafuta nini kwa huyu mwanamke!!" Simu ikakatwa hapohapo nikapatwa na kiu mixer mkojo kwa wakati mmoja!.
Baadae kupiga tena akapokea Sasa kitesa roho wangu! Nikaanza mlaumu na kulalamika jibu nililojibiwa ni "Bwana ee tafuta wa kumpa hayo mapenzi yako ya kibatabata!" Simu ikakatwa kupiga tena nakuta nishachezeshwa buloku pande zote.. haikutosha nikaamua nimfate ana kwa ana si nikakutananae aniambie hata sababu ya kuniacha,nilichoambulia nilichekwa halafu akaondoka ila kwa mbali nikasikia neno kama akisema "nimekuacha na uwabata wako" anyway sikusikia vizuri ila nikaona isiwe tabu nami nivunge nisimtafute!
Sasa tabu ipo hapo kwenye kuvunga! Jamani mapenzi yanauma nyie yani maumivu nayoyasikia sijui hata yanatokea wapi ila nachosikia yani mgongo unakuwa wamotooooo halafu Kama unafinywafinywa! Kichwa kimeshaparanganyika hapa nimejikuta nalia huku nimesimama lakini machozi yanaelekea masikioni!!
Mapenzi si kitu cha mchezo jamani😪