Hivi kati ya maombi na nyungu, kipi kimetusaidia? Pia tumegunduwa dawa za kutosha! ni wazi Tanzania tumeishinda covid-19!

jmushi1

Platinum Member
Nov 2, 2007
24,989
22,521
Mimi binafsi nasema ni jambo la kumshukuru Mungu kwasababu amejibu maombi yetu na tumeishinda corona.

Hatahivyo ninafahamu kuwa kuna wale ambao nyungu imewasaidia. Kuna member humu waliotoa ushuhuda.

Kwa hali inavyoendela, dawa tunazo za kutosha zimezinduliwa na wataalam wetu na kuthibitishwa na serikali. Mtaani maisha yanaendelea fresh kabisa na watoto wanarudi Shule karibuni huku tukiendelea kuchapa maombi na dua!

Lakini mafanikio haya ya kuishinda corona, wengi wamempa sifa rais kwa sababu hakuweka lockdown kama mataifa mengine na kwahiyo apewe sifa anazostahili. Pia ni yeye aliyetutaka tufanye maombi na baadaye kujifukiza. Kwahilo pia anastahili sifa zake kwakuwa tumeishinda covid-19.

Lakini swali langu hili ni la muhimu kwasababu kuna wale waliokuwa wakiamini kuwa maombi yatasaidia na kwamba yamesaidia, lakini pia, kwa upande wa pili, kuna wale waumini wa nyungu! Hao nao wanadhani ndiyo imesaidia kuishinda covid.

Hata hivyo kuna wale wanaodai mambo ya nyungu ni uchawi. Hii sijui imekaaje? Hao lazima wanaamini ni maombi na siyo hizo nyungu. Lakini pia tusiwasahau na wataalam wetu ambao wamegunduwa dawa za corona.

Ni wazi kuwa mataifa mengine yatakuja kutaka kujifunza kutoka kwetu na pengine kupata dawa nk. Wengi wetu kusema kweli tulishangazwa na hatua za rais kukubali mikusanyiko ya kuliombea Taifa na hata sasa mikusanyiko hiyo bado ipo na corona imefutiliwa mbali. Hivyo maoni yangu mimi, ni MAOMBI yamefanya kazi.
 
Hii ndiyo imesaidia.
tapatalk_1589275216683.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa kubwa iliyotuaidia Tanzania ni kutotoa takwimu za ukweli, then tukaach akabi akutoa takwimu! It works a lot.
Hivi mkuu hizo Takwimu zinasaidia nini kama ukienda kazini kila mtu unayemfahamu yuko, kanisani wako, kazini wako. Shida iko wapi? Halafu Kwani watu wameanza kufa leo? Magonjwa mengine hayaui?

Kutoa takwimu kabla hatujajiridhisha kuwa wamekufa kweli na corona(kumbuka vipimo vilitoa matokeo fekero baada ya issue ya papai nk)

Mkuu ukweli wa corona unafahamika mtaani. Kama watu wako poa, hakuna haja ya kupanikishana na mitakwimu.
 
Mkuu kwa namna watu huku mitaani wanavyokufa na hakuna msaada imenibidi nikimbie😁😁
Mkuu sikuwa nafahamu kama kuna watu wanakufa mtaani. Mitaa gani hiyo? Mbona maisha yanaendelea freshi tu?
 
Hivi mkuu hizo Takwimu zinasaidia nini kama ukienda kazini kila mtu unayemfahamu yuko, kanisani wako, kazini wako. Shida iko wapi? Halafu Kwani watu wameanza kufa leo? Magonjwa mengine hayaui?

Kutoa takwimu kabla hatujajiridhisha kuwa wamekufa kweli na corona(kumbuka vipimo vilitoa matokeo fekero baada ya issue ya papai nk)

Mkuu ukweli wa corona unafahamika mtaani. Kama watu wako poa, hakuna haja ya kupanikishana na mitakwimu.
Hahahhaa basi sawa
 
Mimi binafsi nasema ni jambo la kumshukuru Mungu kwasababu amejibu maombi yetu na tumeishinda corona.

Hatahivyo ninafahamu kuwa kuna wale ambao nyungu imewasaidia. Kuna member humu waliotoa ushuhuda.

Kwa hali inavyoendela, dawa tunazo za kutosha zimezinduliwa na wataalam wetu na kuthibitishwa na serikali. Mtaani maisha yanaendelea fresh kabisa na watoto wanarudi Shule karibuni huku tukiendelea kuchapa maombi na dua!

Lakini mafanikio haya ya kuishinda corona, wengi wamempa sifa rais kwa sababu hakuweka lockdown kama mataifa mengine na kwahiyo apewe sifa anazostahili. Pia ni yeye aliyetutaka tufanye maombi na baadaye kujifukiza. Kwahilo pia anastahili sifa zake kwakuwa tumeishinda covid-19.

Lakini swali langu hili ni la muhimu kwasababu kuna wale waliokuwa wakiamini kuwa maombi yatasaidia na kwamba yamesaidia, lakini pia, kwa upande wa pili, kuna wale waumini wa nyungu! Hao nao wanadhani ndiyo imesaidia kuishinda covid.

Hata hivyo kuna wale wanaodai mambo ya nyungu ni uchawi. Hii sijui imekaaje? Hao lazima wanaamini ni maombi na siyo hizo nyungu. Lakini pia tusiwasahau na wataalam wetu ambao wamegunduwa dawa za corona.

Ni wazi kuwa mataifa mengine yatakuja kutaka kujifunza kutoka kwetu na pengine kupata dawa nk. Wengi wetu kusema kweli tulishangazwa na hatua za rais kukubali mikusanyiko ya kuliombea Taifa na hata sasa mikusanyiko hiyo bado ipo na corona imefutiliwa mbali. Hivyo maoni yangu mimi, ni MAOMBI yamefanya kazi.
Hata mwenyezi Mungu mwingi wa rehema alisema jilinde nami ntakulinda. Nafikiri ayo ni maswala ya kiimani zaidi na kila mmoja kwa imani yake amepata kile alichostahili.
 
Back
Top Bottom