Kuna mambo rais wetu amekuwa hayachukulii hatua zinazostahili dhidi ya wateule wake kwa wakati mwafaka kwa sababu ambazo sisi wananchi wa kawaida hatuzielewi so tafsiri ya haraka ya hali hii ni dharau kwetu tuliompa dhamana ya kutuongoza. Naomba nitoe mifano michache:
(i)Mtakumbuka alipounda baraza la mawaziri mwaka 2006 alikuja na mawaziri lukuki wapatao 60. Tulilalamika na kulalamika mpaka tukachoka aliweka pamba masikioni pasi na kuchukua hatua. Mungu bariki ikaja issue ya Richmond ndio hapa sasa akaitumia nafasi kupunguza idadi ya mawaziri. Juzi kaja tena jamani na mawaziri wengine 50 kutoka 47 nadhani wa 2008. Amekuja mpaka na waziri wa mahusiano wassira (nina hamu sana ya kuiona job description yake) Ni ajabu na kweli kwamba wafadhili wetu kama UK wako busy kupunguza matumizi ya serikali sisi watembeza bakuli tuko busy kuongeza matumizi.
(ii) Wakati wa sakata la Richmond 2008 miongoni mwa maazimio ya Bunge letu ilikuwa ni kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa AG wa wakati huo na boss wa PCCB bwana Hosea hilo halikufanyika asilani. AG aliachwa mpaka astaafu kwa mujibu wa sheria na Hosea anadunda mpaka leo. Hii ilikuwa ni dharau ya waziwazi ya rais kwa bunge na wananchi kwa ujumla. Kama haitoshi juzi tena Hosea kaivua nguo ofisi ya rais ambako ndiko PCCB iliko kwa kumsafisha Chenge kinyume cha sheria. Nashindwa kuelewa kwamba aibu yote hii bado rais anaona si kitu. Hii pia ni dharau kwetu watanzania kwamba kuna watu wanaweza kufanya lolote wakati wowote na still wasiguswe, Hosea ni mmojawapo. So JK Hosea naye anasubiriwa mpaka astaafu kwa mujibu wa sheria? Tunshukuru sana kwa dharau zako kwetu sisi maboss wako uliopita juzi na kukaa nasi mpaka sakafuni ili tu tukupe kura zetu.
(iii) Mfano wa mwisho kwa leo ni wa bwana mrema aliyestaafu juzi Tanroads. Ni bahati mbaya sana kwamba kuna watu pasipokujua wanampa credits Magufuli asizostahili. Mrema hajafukuzwa kazi na Magufuli bali amestaafu kwa mujibu wa sheria. Mrema naye kama ilivyo kwa Hosea alifanya vituko vya ajabu sana hapo Tanroads lakini hakukuwa na wa kumgusa akiwemo rais wa nchi. Tumepiga kelele weeeeh wapi hakuna wa kutusikiliza. Hiki si kingine bali ni dharau za rais kwa maboss wake. Ni dharau kwani hao wote kwa mujibu kwa katiba yetu iliyoaachwa mbali na wakati ni wateule wake so hakuna mwingine wa kuchukua hatua zaidi yake.
Nahitimisha kwa kumuuliza tena swali Jk, so Hosea naye pamoja na madudu yote anayofanya anaachwa mpaka astaafu kama Mrema wa Tanroads na former AG Mwanyika? Kama ndivyo kuna haja gani ya kuwa na wewe kama kazi yako ni kuteua tu na kwaacha watu wafanya wafanyavyo pasipokuchukiwa hatua yeyote?
(i)Mtakumbuka alipounda baraza la mawaziri mwaka 2006 alikuja na mawaziri lukuki wapatao 60. Tulilalamika na kulalamika mpaka tukachoka aliweka pamba masikioni pasi na kuchukua hatua. Mungu bariki ikaja issue ya Richmond ndio hapa sasa akaitumia nafasi kupunguza idadi ya mawaziri. Juzi kaja tena jamani na mawaziri wengine 50 kutoka 47 nadhani wa 2008. Amekuja mpaka na waziri wa mahusiano wassira (nina hamu sana ya kuiona job description yake) Ni ajabu na kweli kwamba wafadhili wetu kama UK wako busy kupunguza matumizi ya serikali sisi watembeza bakuli tuko busy kuongeza matumizi.
(ii) Wakati wa sakata la Richmond 2008 miongoni mwa maazimio ya Bunge letu ilikuwa ni kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa AG wa wakati huo na boss wa PCCB bwana Hosea hilo halikufanyika asilani. AG aliachwa mpaka astaafu kwa mujibu wa sheria na Hosea anadunda mpaka leo. Hii ilikuwa ni dharau ya waziwazi ya rais kwa bunge na wananchi kwa ujumla. Kama haitoshi juzi tena Hosea kaivua nguo ofisi ya rais ambako ndiko PCCB iliko kwa kumsafisha Chenge kinyume cha sheria. Nashindwa kuelewa kwamba aibu yote hii bado rais anaona si kitu. Hii pia ni dharau kwetu watanzania kwamba kuna watu wanaweza kufanya lolote wakati wowote na still wasiguswe, Hosea ni mmojawapo. So JK Hosea naye anasubiriwa mpaka astaafu kwa mujibu wa sheria? Tunshukuru sana kwa dharau zako kwetu sisi maboss wako uliopita juzi na kukaa nasi mpaka sakafuni ili tu tukupe kura zetu.
(iii) Mfano wa mwisho kwa leo ni wa bwana mrema aliyestaafu juzi Tanroads. Ni bahati mbaya sana kwamba kuna watu pasipokujua wanampa credits Magufuli asizostahili. Mrema hajafukuzwa kazi na Magufuli bali amestaafu kwa mujibu wa sheria. Mrema naye kama ilivyo kwa Hosea alifanya vituko vya ajabu sana hapo Tanroads lakini hakukuwa na wa kumgusa akiwemo rais wa nchi. Tumepiga kelele weeeeh wapi hakuna wa kutusikiliza. Hiki si kingine bali ni dharau za rais kwa maboss wake. Ni dharau kwani hao wote kwa mujibu kwa katiba yetu iliyoaachwa mbali na wakati ni wateule wake so hakuna mwingine wa kuchukua hatua zaidi yake.
Nahitimisha kwa kumuuliza tena swali Jk, so Hosea naye pamoja na madudu yote anayofanya anaachwa mpaka astaafu kama Mrema wa Tanroads na former AG Mwanyika? Kama ndivyo kuna haja gani ya kuwa na wewe kama kazi yako ni kuteua tu na kwaacha watu wafanya wafanyavyo pasipokuchukiwa hatua yeyote?