Hivi JF hakunaga wachawi wa kutoa mbinu bora za kukabiliana na kuishi na jamii za kichawi?

Hivi hawa wachawi huku Africa hawaoni aibu jinsi jamii zinavyoteseka kwa ujinga wao...

Wakiacha uchawi ukawa haupo watu wakaishi vizuri tu kuna shida gani?.....ni vyema ule utamaduni wakuwaua wachawi na washirikina ukaanza kila akutwaye na vitendea kazi na tabia hizi risasi.... baada ya miaka 20 nina uhakika jamii itaishi kwa raha sana...

Naamini moja ya vitu vinavyosababisha jamii nyingi kuwa masikini Tanzania ni uchawi uliokithiri kwenye koo pamoja na mitaani, watu kuendekeza kuharibiana maisha...
Tukutane usiku wa saa 8
 
Hi mada, wamealikwa wachawi na vigagura kuja kutoa shuhuda humu, lakn cha ajabu walokole na wanoko ndyo wameivamia mada kwa kujfanya wajuaji na kutoa michango yao yakipuuz isiyohitajika ktk mada.

Watz tujfunzen kuelewa mada kabla hujaijibu, hasa nyie wafuas wa dini...
 
Uchawi ni imani.
Ukiona unaogopa wachawi na uchawi jua wewe ni muumini wa hiyo imani..maana nyingine wewe pia ni mchawi.

Tusubiri wachawi wenzio waje watoe elimu ya hiyo dinidinia
WANAOJAZANA MAKANISANI NA MISIKITINI BY 80 PC, NI WACHAWI.HATA PENGINE HATA WEWE NI MCHAWI AU UMEKWENDA KWA MGANGA.
Yaani anakwenda kanisani at the same time, Anakuwa na kaimani kengine.
Kumshinda Azazel purification yake sio ya mchezo mchezo, Toka atamke nakwenda kushika mali na anasa zote za dunia,sasa imani ya mungu iliyo Kali NA pure ndiyo itakayoweza kumnyanganya Azazel,ndio naans huwapa mali walio dhaifu kwa mikataba.
 
Hi mada, wamealikwa wachawi na vigagura kuja kutoa shuhuda humu, lakn cha ajabu walokole na wanoko ndyo wameivamia mada kwa kujfanya wajuaji na kutoa michango yao yakipuuz isiyohitajika ktk mada.

Watz tujfunzen kuelewa mada kabla hujaijibu, hasa nyie wafuas wa dini...
Ili elimu ibalance sahihi makundi yote yatoe uzoefu wao.Huwezi mjua Mungu bila kumjua shetani,Ili uwe mlokole kamili ni lzm uujue uchawi unavyofanya kazi,Ili uushinde,uwafunze watu jinsi ya kuushinda.
Huwezi mshinda adui wako bila kumjua.
Hata kwenye ujasusi na upelelezi uchawi unatumika kwa wenzetu walioadvance.
Mfano kuingia sehemu bila kuonekana na kuchukua taarifa,kujua tukio na kulidhibiti au kutoa taadhari kabla alijafanyika mfano alert za mwafrika ujifunza uchawi Ili aharibu watu Mzungu ujifunza uchawi Ili kupata maendeleo.
 
Hi mada, wamealikwa wachawi na vigagura kuja kutoa shuhuda humu, lakn cha ajabu walokole na wanoko ndyo wameivamia mada kwa kujfanya wajuaji na kutoa michango yao yakipuuz isiyohitajika ktk mada.

Watz tujfunzen kuelewa mada kabla hujaijibu, hasa nyie wafuas wa dini...
Kuna mtu nilikuta kaandika humu wachawi na wafiraji Jf hawana ujasiri wa kujitaja hata nyuma ya maandishi.
 
Elimu zote zipo google kuhusu uchawi,codes zake,na Kinga zake,miiko na Kazi zake,kurogwa na kutorogeka,Elimu ni pana uchawi unajifunza unafundishwa vyuoni ukitaka na unahitimu kipo chuo Temeke kinafunza uchawi miaka 5 then uganga miaka 2.Ili uwe mganga ni lzm ujifunze uchawi.
Mchawi na mganga ni kampuni moja SAwa na coca na fanta maana wote boss wao ni mmoja anaewapa nguvu za kutenda.
Mchawi anaweza akamroga mganga na viceversa.Mchawi umuua mganga na mganga umuua mchawi hapa ni uwezo binafsi wa nguvu aliyonayo muhisika na nguvu hizi wanapewa na shetani kama asante ya kumfurahisha shetani ikiwemo ikiwemo kutoa watu kafara.
Kadri mchawi na mganga wanavyoua Sana na ndivyo vyeo vyao na nguvu zao uongezeka sana.
Mganga akimuua mganga mwenzake anapanda cheo.Mchawi akimuua mganga cheo kinapanda, mganga akimuua Mwenyekiti wa wachawi cheo kinapanda.
Mganga umroga mteja wake asiishiwe magonjwa Ili apige pesa.
Mganga akimuwekea kinga mtu aliyerogwa na wachawi au kujifanya kumtibu wachawi wanaungana kumuua mganga, mganga umuomba ruhusa au umpa pesa mchawi auondoe ugonjwa aliouweka kwa mtu waliyemroga na mchawi akiridhia uuondoa uchawi na mgonjwa huwa mzima.
Hivi uchawi ni kwa ajili ya kila mtu au ni baadhi ndo hueeza kujifunza au kudhurika nao?
 
Hivi uchawi ni kwa ajili ya kila mtu au ni baadhi ndo hueeza kujifunza au kudhurika nao?
Uchawi ni kwa ajili ya watu wapumbavu yaani Jamii za kichawi.Mtu aliyeelimika hafanyi mambo ya upumbavu.Na wapumbavu uwaridhisha upumbavu kizazi chao, kizazi cha wapumbavu uzaa wapumbavu.Ukiwa na positive power hao wapumbavu waganga na wachawi hawawezi kukudhuru, uchawi ni negative power na negative power usafiri kwenye negative power, positive power ni poor conductors yaani umeme hauwezi nasa plastic,ubao,mpira.Nk.
Uchawi hauna faida si kwa jamii hata kwa mchawi mwenyewe.
Na lengo kuu la ushirikina ni kupunguza uwezo wa kufikiri yaani kupumbaza uwezo wa kufikiri aliopewa binadamu na Mwenyezi Mungu.Majini ndio waliowafunza wanadamu uchawi.
 
Hapa JF Kuna mada nyingi kuhusu watu wakieleza uzoefu wao juu ya mambo ya kichawi. Ni bahati mbaya zaidi sijawahi kuona hata mmoja akikiri kuwa yeye ni mchawi na akatuelimisha mengi kuhusu uchawi kama:-

Mimi nadhani naweza kuwa ndio mwenye mada nyingi za uchawi kuliko mwingine yoyote hapa JF.. Sikubakisha kitu kwenye ushirikina .Naujua ndani nje kwa kuusomea na kuufanya lakini si kama mimi ni mchawi kamili.. Mimi nilichokuwa nafanya ni fantasy witchcraft

Uchawi ni imani ya siri yenye matendo kificho yasiyo ya uwazi, uchawi ni kaliba
Kongwe tangu kuumbwa kwa ulimwengu na uchawi ni sehemu ya uumbaji, yaani ni ukamilifu wa uwili kwenye mwanga na giza, uchawi ukiwa ni upande wa giza..!

Uchawi ni aina ya sayansi kinyume cha sayansi ithibati na formula, uchawi hupimwa kwa matokeo na si mchakato...kwa maana ya kwamba huwezi kuthibitisha uchawi kwa formula bali kwa matokeo
Uchawi ukiwa umewekwa kwenye ulimwengu wa kiroho wa giza ni kinyume cha ulimwengu wa roho wa mwanga kwahiyo kwa namna yoyote ile hauwezi kuwa na faida wala manufaa kwenye dunia ya macho ya nyama na mwanga
Uchawi upo kwa ajili ya kutesa, kuharibu kupotosha na kudanganya, kati ya yote haya je kuna lenye faida?? Jibu ni hapana

Zaidi uchawi ni tawi tu kwenye mti shina wa USHIRIKINA, Ushirikina ndio unabena uchawi, ulozi kuwanga na matendo yote yanayofanana na hayo!
Uchawi una madaraja na matabaka.. Kuna uchawi mwepesi ama rahisi na kuna uchawi mgumu ama mzito kuna uchawi kwa nia ya kujifurahisha lakini pia kuna uchawi wa kuumiza na kuharibu..!

Uchawi ni imani pia yenye mkuu na madhabahu zake nitakuwekea mada kadhaa ujifunze zaidi
Pia uchawi upo wa KILA namna na hali tofauti tofauti,maana uchawi ni elimu pana,pia KILA chama cha kichawi kina malengo na ajenda zao.Uchawi ni kama Jamii ya wezi,wezi wapo wa aina nyingi kuna wanao shughulika na magari,tv simu na radio,kuna vibaka,kuna wapiga finger,kuna wezi wa mitandaoni,nk na ni nadra Sana kukuta mwenye fani zote za wizi,ndivyo ilivyo Jamii ya wachawi wapo ambao miiko yao awaui watu bali uharibu tu maisha yao,uwachezea,uwatumikisha kichawi usiku,nk.Upo ushirika mwingine wa wachawi chama chao awaui mama mjamzito uamini utakua umeua watu wawili kwa pamoja means aliyetumboni hana hatia,wapo ambao awamwagi damu,nk ,nk vipo vyama vingi sana vya kichawi, vingine ndivyo uratibu na kuongoza hadi shughuli za kisiasa wakiwa pia na wanachama wao ambao wapo kwenye vyombo vya maamuzi nchini.So zipo ajenda zingine za kinchi au kidunia lakini zimetoka kwenye kamati za vyama vya kichawi.
 
Ninawasubiria waje.Unakuta mtoto anarithishwa au anabebwa kwenda kuroga sijui inakuwaje yaani.
Kwa mtoto ni rahisi kufunzwa kuliko mtu mzima.Pili ni kuongeza ufuasi kama iliyo mtoto Mdogo kupelekwa kanisani.
Kumbuka uchawi umekuwepo tangu zamani hata kabla ya dini
 
Kuna mwamba mwenye uelewa na hizi mambo ngoja atakuja
Zipo nyingi sana youtube na shuhuda za watu mbalimbali waliokuwa kwenye uchawi na ushirikina ikiwemo kuwa hata daraja la juu na wakatoka huko wanaeleza ABC kuhusu uchawi na jinsi ya kujikinga nao na jinsi walivyoshinda hatari ya kuuwa kumbuka ukiacha uchawi,au ukitoa Siri zao ni lazima wakuue hasa kama huna Mungu au positive power au ant missile yaani viblock uchawi.
 
Huwezi mjua Mungu kujua uKuu wake bila kumjua shetani na vitendea Kazi vyake.Ili uive imani ni lazima ujifunze kuhusu imani zote.
 
1. Uchawi unazidiana, Wapo Waganga ambao pia ni Wachawi, wapo Waganga ambao pia sio Wachawi.
2. Mganga anaweza kulogwa pia na Mchawi.
3.Kinga ya kweli ya Uchawi, sio kutoamini kwenye Uchawi kuwa haupo, Imani hii haiwezi kukusaidia usilogwe, unalogeka Vizuri tu! Ila kinga Bora ni Kusali, kuomba kwa nguvu iliyo juu zaidi ambayo ni ya Mungu, coz Mungu ni Nuru, Uchawi ni Giza, hata Giza likiwa Totoro kiasi gani, Mwanga wa Tochi tu unaondoa Giza eneo Hilo, but Giza hata liwe Totoro kiasi gani, haliwezi kufunika Mwanga ...

4.Moja Kati Sheria za kichawi ni kurithishana, Kizazi mpaka Kizazi, ni kosa kubwa kwa Mchawi kufa bila kurithisha Uchawi, ama kwa Mtoto, Watoto, Wajukuu, Watoto wa Ndugu take n.k na ikishindikana Mchawi hurithisha Uchawi hata kwa Mtoto wa jirani yake!

5. Wachawi, Wachungaji wa kweli, Masheikh wa kweli na Majini, Hawa wote wanaweza kuona Kiroho, ama kwa msaada wa Roho wa Mungu, ama msaada wa Shetani, mtoto mdogo akizaliwa, hao watu hapo juu, wanaweza kujua huyo mtoto atakua Tajiri, Masikini, Kiongozi mkubwa au MTU mkuu hapo baadaye, wanajua kupitia Nyota ya mtu HUSIKA, (Rejea kisa Cha Yesu na Mamajusi).

So Wachawi na Majini coz always wao ni Waaribifu ndo kipindi wanamroga mtoto na kuharibu future yake (mti wenye matunda......)
Ukiona mtoto anahangaika na maradhi ya kulogwa, Shule hasomi n.k Basi mtoto huyo ana akili, na angekua mtu mkuu baadaye, Watoto wa aina hii, wanakua hawana akili shuleni, but soon tatizo lao liisha, wanaanza kufanya vizuri shuleni...
True wanachukua nyota za watoto wenye vipawa na kuziuza kwa wenye pesa.
Kosa kubwa Sana wanalokosea wazazi ni kuwapeleka watoto wadogo kwa waganga hapa wanakuwa wamemkabidhi mtoto kwa shetani.Siri hii weupe wanaijua thus watoto au uzao wao umeendelea.Wazazi wengi ndio uuwa future /hatma za watoto wao kwa kuwapeleka watoto kwa waganga, waganga ni SAwa na fundi simu ukimuachia simu au computer wanaiba hard disc yako nzuri wanakuwekea mbovu au inayosumbua kisha wanauza hard disc,memory drive au utumbo wa simu kwa wenye pesa.Na Jamii yenye kuendekeza ushirikina haiwezi kuwa na maendeleo.
 
True wanachukua nyota za watoto wenye vipawa na kuziuza kwa wenye pesa.
Kosa kubwa Sana wanalokosea wazazi ni kuwapeleka watoto wadogo kwa waganga hapa wanakuwa wamemkabidhi mtoto kwa shetani.Siri hii weupe wanaijua thus watoto au uzao wao umeendelea.Wazazi wengi ndio uuwa future /hatma za watoto wao kwa kuwapeleka watoto kwa waganga, waganga ni SAwa na fundi simu ukimuachia simu au computer wanaiba hard disc yako nzuri wanakuwekea mbovu au inayosumbua kisha wanauza hard disc,memory drive au utumbo wa simu kwa wenye pesa.Na Jamii yenye kuendekeza ushirikina haiwezi kuwa na maendeleo.
Kabisa, na Watu hawajui kwamba hata Waganga wanachukua Rushwa toka kwa Wachawi, kwa ajiri vitu ambavyo vipo nje wa Wachawi kuvipata na Waganga wanavyo, ama nguvu ya mganga no kubwa kuliko ya Mchawi, Kuna siku ntakuja kuleta kiss kimoja Cha kweli!
 
Waganga na wachawi inafaa wauwawe kama walivyofanya ulaya Ili maendeleo yake, maana wanaharibu Sana jamii,wanaleta mafarakano kwenye Jamii,wanapunguza uwezo wa kufikiri wa jamii,wanawapa wezi na majambazi nguvu na roho ya kutenda uhalifu kuiba mali za watu,kuuwa watu na Jamii inakuwa masikini kwa sababu ya hawa wapumbavu.
Yafaa watenganishwe na jamii awafai kabisa kuwepo duniani hawa wapumbavu.
 
Uchawi na wachawi limekuwa ni tatizo kubwa katika jamii tangu kuwepo kwa Dunia. Watu wengi katika jamii wanapenda kujua mengi kuhusu uchawi maana kwa wengine ni jambo la kusadikika kutokana na usiri mkubwa juu ya uchawi na wachawi na mbinu zao, kusudio lao, kwamba uchawi ni dini, ushirika, Chama au ni muunganiko wa namna gani?

Hapa JF Kuna mada nyingi kuhusu watu wakieleza uzoefu wao juu ya mambo ya kichawi. Ni bahati mbaya zaidi sijawahi kuona hata mmoja akikiri kuwa yeye ni mchawi na akatuelimisha mengi kuhusu uchawi kama:-

1. Ni sababu gani inayoweza kufanya mtu ashambuliwe na wachawi au mchawi?

2. Kuna kinga yoyote ninayoweza kuchukua ili nisiadhibiwe na wachawi?

3. Uchawi ni zao la urithi, je wanaangalia sifa gani ya mtu wanaetaka kumrithisha katika familia?

4. Kuna uhusiano wa kirafiki au kiuadui kati ya wachawi na waganga wa jadi?

5. Ikiwa waganga wanatibu madhara ya uchawi ndio kusema waganga wa jadi wana maarifa zaidi ya wachawi?

Juu ya hayo ningeomba kwa faida ya wengi hapa JF kama sehemu ya kupata elimu ya jamii wajitokezee watu ambao ni wachawi bila hofu nikiamini vile wapo nyuma ya maandishi hawatapata athari zozote, kutusaidia kutoa elimu kubwa juu ya uchawi, wachawi, walengwa wa uchawi, waganga na Siri nyingine ambazo jamii ipo gizani juu ya uchawi.

Ahsanteni
Sidhani kama mchawi ana nia njema na anayetaka kumdhuru, sasa iweje akupe mbinu ambayo itamfanya yeye asifanikiwe?
 
Uchawi na wachawi limekuwa ni tatizo kubwa katika jamii tangu kuwepo kwa Dunia. Watu wengi katika jamii wanapenda kujua mengi kuhusu uchawi maana kwa wengine ni jambo la kusadikika kutokana na usiri mkubwa juu ya uchawi na wachawi na mbinu zao, kusudio lao, kwamba uchawi ni dini, ushirika, Chama au ni muunganiko wa namna gani?

Hapa JF Kuna mada nyingi kuhusu watu wakieleza uzoefu wao juu ya mambo ya kichawi. Ni bahati mbaya zaidi sijawahi kuona hata mmoja akikiri kuwa yeye ni mchawi na akatuelimisha mengi kuhusu uchawi kama:-

1. Ni sababu gani inayoweza kufanya mtu ashambuliwe na wachawi au mchawi?

2. Kuna kinga yoyote ninayoweza kuchukua ili nisiadhibiwe na wachawi?

3. Uchawi ni zao la urithi, je wanaangalia sifa gani ya mtu wanaetaka kumrithisha katika familia?

4. Kuna uhusiano wa kirafiki au kiuadui kati ya wachawi na waganga wa jadi?


5. Ikiwa waganga wanatibu madhara ya uchawi ndio kusema waganga wa jadi wana maarifa zaidi ya wachawi?

Juu ya hayo ningeomba kwa faida ya wengi hapa JF kama sehemu ya kupata elimu ya jamii wajitokezee watu ambao ni wachawi bila hofu nikiamini vile wapo nyuma ya maandishi hawatapata athari zozote, kutusaidia kutoa elimu kubwa juu ya uchawi, wachawi, walengwa wa uchawi, waganga na Siri nyingine ambazo jamii ipo gizani juu ya uchawi.

Ahsanteni
Mimi ninakujibu swali lako la pili Mkuu kinga dhidi ya wachawi ipo ukihitaji nitafute kwa wakati wako ili nikupe kinga ya mwili wako na mahali unapo kaa ili wachawi wasiweze tena kukuchezea wewe na familia yako.

Swali la 3 Jibu lake hili hapa Wachawi katika kila familia zetu za kiafrika kuna mchawi japo mmoja au wawili wanapokuwa wazee karibu ya kufa mchawi katika familia yenu anatafuta mtu mmoja anaye mpenda anamfundisha uchawi usingizini kwa muda fulani mpaka akiona sasa yule anaye kufundisha umehitimu anakufundisha wazi wazi na kukkabidhi mikoba yake ya uchawi. Akifariki na wewe ndio unarithi uchawi wake katika familia unakuwa wewe ndio mchawi mkuu katika familia yenu.

Jibu Swali la 4 ndio kuna uhusiano Mkubwa kati ya mchawi na mganga wa asili. Kuna mchawi anaye juwa uchawi lakini anapata usaidizi kwa mganga wa asili na kuna mchawi anashirikiana na mganga wa asili kuroga pamoja.

Jibu la swali la 5 Waganga wengi ndio wachawi wenyewe mganga amemzidi mchawi. Mchawi anafundishwa na mganga wa asili uchawi wake.
 
Back
Top Bottom