Hivi JF hakunaga wachawi wa kutoa mbinu bora za kukabiliana na kuishi na jamii za kichawi?

Bwajilo

JF-Expert Member
Dec 5, 2021
345
880
Uchawi na wachawi limekuwa ni tatizo kubwa katika jamii tangu kuwepo kwa Dunia. Watu wengi katika jamii wanapenda kujua mengi kuhusu uchawi maana kwa wengine ni jambo la kusadikika kutokana na usiri mkubwa juu ya uchawi na wachawi na mbinu zao, kusudio lao, kwamba uchawi ni dini, ushirika, Chama au ni muunganiko wa namna gani?

Hapa JF Kuna mada nyingi kuhusu watu wakieleza uzoefu wao juu ya mambo ya kichawi. Ni bahati mbaya zaidi sijawahi kuona hata mmoja akikiri kuwa yeye ni mchawi na akatuelimisha mengi kuhusu uchawi kama:-

1. Ni sababu gani inayoweza kufanya mtu ashambuliwe na wachawi au mchawi?

2. Kuna kinga yoyote ninayoweza kuchukua ili nisiadhibiwe na wachawi?

3. Uchawi ni zao la urithi, je wanaangalia sifa gani ya mtu wanaetaka kumrithisha katika familia?

4. Kuna uhusiano wa kirafiki au kiuadui kati ya wachawi na waganga wa jadi?

5. Ikiwa waganga wanatibu madhara ya uchawi ndio kusema waganga wa jadi wana maarifa zaidi ya wachawi?

Juu ya hayo ningeomba kwa faida ya wengi hapa JF kama sehemu ya kupata elimu ya jamii wajitokezee watu ambao ni wachawi bila hofu nikiamini vile wapo nyuma ya maandishi hawatapata athari zozote, kutusaidia kutoa elimu kubwa juu ya uchawi, wachawi, walengwa wa uchawi, waganga na Siri nyingine ambazo jamii ipo gizani juu ya uchawi.

Ahsanteni
 
Uchawi ni imani.
Ukiona unaogopa wachawi na uchawi jua wewe ni muumini wa hiyo imani..maana nyingine wewe pia ni mchawi.

Tusubiri wachawi wenzio waje watoe elimu ya hiyo dini.
Haya ndio niliyoyata kujua, japo umejibu swali moja ila nakushukuru sana na kuomba kama hutojali fafanua na umalizie na hayo mengine. Ila wachawi mna visa sana.
 
Ule ni ulimwengu mwengine kabisa aisee wana taratibu zao, viongozi wao wa kikanda, kitaifa na hata kibara, ukitaka kujua hivyo vitu itabidi uingie kwenye ulimwengu wao ila kwa wao kutoa siri zao kwa mtu ambaye hayupo kwenye ulimwengu wao huwa ni nadra sana aisee.
 
Ule ni ulimwengu mwengine kabisa aisee wana taratibu zao, viongozi wao wa kikanda, kitaifa na hata kibara, ukitaka kujua hivyo vitu itabidi uingie kwenye ulimwengu wao ila kwa wao kutoa siri zao kwa mtu ambaye hayupo kwenye ulimwengu wao huwa ni nadra sana aisee.
Kwa hiyo kumbe hapa nimeandika kazi bure wana kiapo cha kutotoa Siri?
 
1. Uchawi unazidiana, Wapo Waganga ambao pia ni Wachawi, wapo Waganga ambao pia sio Wachawi.
2. Mganga anaweza kulogwa pia na Mchawi.
3.Kinga ya kweli ya Uchawi, sio kutoamini kwenye Uchawi kuwa haupo, Imani hii haiwezi kukusaidia usilogwe, unalogeka Vizuri tu! Ila kinga Bora ni Kusali, kuomba kwa nguvu iliyo juu zaidi ambayo ni ya Mungu, coz Mungu ni Nuru, Uchawi ni Giza, hata Giza likiwa Totoro kiasi gani, Mwanga wa Tochi tu unaondoa Giza eneo Hilo, but Giza hata liwe Totoro kiasi gani, haliwezi kufunika Mwanga ...

4.Moja Kati Sheria za kichawi ni kurithishana, Kizazi mpaka Kizazi, ni kosa kubwa kwa Mchawi kufa bila kurithisha Uchawi, ama kwa Mtoto, Watoto, Wajukuu, Watoto wa Ndugu take n.k na ikishindikana Mchawi hurithisha Uchawi hata kwa Mtoto wa jirani yake!

5. Wachawi, Wachungaji wa kweli, Masheikh wa kweli na Majini, Hawa wote wanaweza kuona Kiroho, ama kwa msaada wa Roho wa Mungu, ama msaada wa Shetani, mtoto mdogo akizaliwa, hao watu hapo juu, wanaweza kujua huyo mtoto atakua Tajiri, Masikini, Kiongozi mkubwa au MTU mkuu hapo baadaye, wanajua kupitia Nyota ya mtu HUSIKA, (Rejea kisa Cha Yesu na Mamajusi).

So Wachawi na Majini coz always wao ni Waaribifu ndo kipindi wanamroga mtoto na kuharibu future yake (mti wenye matunda......)
Ukiona mtoto anahangaika na maradhi ya kulogwa, Shule hasomi n.k Basi mtoto huyo ana akili, na angekua mtu mkuu baadaye, Watoto wa aina hii, wanakua hawana akili shuleni, but soon tatizo lao liisha, wanaanza kufanya vizuri shuleni...
 
1. Uchawi unazidiana, Wapo Waganga ambao pia ni Wachawi, wapo Waganga ambao pia sio Wachawi.
2. Mganga anaweza kulogwa pia na Mchawi.
3.Kinga ya kweli ya Uchawi, sio kutoamini kwenye Uchawi kuwa haupo, Imani hii haiwezi kukusaidia usilogwe, unalogeka Vizuri tu! Ila kinga Bora ni Kusali, kuomba kwa nguvu iliyo juu zaidi ambayo ni ya Mungu, coz Mungu ni Nuru, Uchawi ni Giza, hata Giza likiwa Totoro kiasi gani, Mwanga wa Tochi tu unaondoa Giza eneo Hilo, but Giza hata liwe Totoro kiasi gani, haliwezi kufunika Mwanga ...

4.Moja Kati Sheria za kichawi ni kurithishana, Kizazi mpaka Kizazi, ni kosa kubwa kwa Mchawi kufa bila kurithisha Uchawi, ama kwa Mtoto, Watoto, Wajukuu, Watoto wa Ndugu take n.k na ikishindikana Mchawi hurithisha Uchawi hata kwa Mtoto wa jirani yake!

5. Wachawi, Wachungaji wa kweli, Masheikh wa kweli na Majini, Hawa wote wanaweza kuona Kiroho, ama kwa msaada wa Roho wa Mungu, ama msaada wa Shetani, mtoto mdogo akizaliwa, hao watu hapo juu, wanaweza kujua huyo mtoto atakua Tajiri, Masikini, Kiongozi mkubwa au MTU mkuu hapo baadaye, wanajua kupitia Nyota ya mtu HUSIKA, (Rejea kisa Cha Yesu na Mamajusi).

So Wachawi na Majini coz always wao ni Waaribifu ndo kipindi wanamroga mtoto na kuharibu future yake (mti wenye matunda......)
Ukiona mtoto anahangaika na maradhi ya kulogwa, Shule hasomi n.k Basi mtoto huyo ana akili, na angekua mtu mkuu baadaye, Watoto wa aina hii, wanakua hawana akili shuleni, but soon tatizo lao liisha, wanaanza kufanya vizuri shuleni...
Salute kwako, japo umenipa mwanga kidogo. Nasubiri kama wenye nyama zaidi.
 
Hivi hawa wachawi huku Africa hawaoni aibu jinsi jamii zinavyoteseka kwa ujinga wao...

Wakiacha uchawi ukawa haupo watu wakaishi vizuri tu kuna shida gani?.....ni vyema ule utamaduni wakuwaua wachawi na washirikina ukaanza kila akutwaye na vitendea kazi na tabia hizi risasi.... baada ya miaka 20 nina uhakika jamii itaishi kwa raha sana...

Naamini moja ya vitu vinavyosababisha jamii nyingi kuwa masikini Tanzania ni uchawi uliokithiri kwenye koo pamoja na mitaani, watu kuendekeza kuharibiana maisha...
 
Hivi hawa wachawi huku Africa hawaoni aibu jinsi jamii zinavyoteseka kwa ujinga wao...

Wakiacha uchawi ukawa haupo watu wakaishi vizuri tu kuna shida gani?.....

Nafikiri kuna manufaa makubwa wanayoyapata labda.
 
Back
Top Bottom