Hivi jamani huu moyo wa kumpenda mtu usie fahamiana nae unatokana na nini?

Pendaelli

JF-Expert Member
Feb 13, 2014
8,907
23,201
Saivi niko kwenye shida moja haikai mbili haisomi, ni takribani wiki 11 tulikua kwenye semina ya maisha ya kiroho kanisani kwetu, ambapo leo tumehitimu na kutumwa rasmi kuihubiri Injili, sa huyu dada mara ya kwanza kumuona nikajisemea tu ndoto yangu ni kuja kuoa mwanamke kama, najua kila mtu ana ndoto ya chaguo lake au unakua na taswira ya mwenzi wako,ama mfupi,mweupe,mnene,au umbile fulani.

Na ndivyo ilivyo kwangu, sasa huyu dada msomi pamoja na leo ilikua siku ya kipekee kaniachia kamaumivu japo najua kataisha lakini . Tumepangwa kwa majina yanayofuatiana leo hii tumekaa pamoja toka saa 2 mpaka 10 na nusu, tumeongea mawili matatu wakati wa kula tumetoka mkoa mmoja, lakini leo ndio mwisho kuonana majaliwa lakini hii roho ya kupenda penda hii nilio nayo inanitia garama ya stress sana Mungu aniondolee kikombe hiki tu kwa kweli, naumiaje!.
 
Unataka tukusaidieje sasa maana hujaweka bayana! Unavyosema kupendapenda inamasnisha umezoe kufanya hivyo au?
 
Back
Top Bottom