daza steven
JF-Expert Member
- Aug 30, 2016
- 359
- 357
Zamani wakati wa ujinga wengi tulikuwa hatujui kuhusu hiyo Marekani tulimezeshwa kila kitu cha upande 1 wa shilingi. lakini inatia aibu kijana ambaye wazazi wake wamempeleka shule lakini leo bado yupo katika zama za ujinga bado anaona kama Marekani ndiyo kimbilio wakati ni nchi hatari hasa kwa bara la Afrika, jamani tujikwamue kutoka utumwa wa kiakili
Mimi huko nyuma nilikuwa nikiamini kuwa Marekani ndiyo taifa ambalo linaongoza kwa kuwa na democrasia kubwa na pana kuliko nchi yoyote hile Duniani kumbe siyo, ukifika Amerika unaweza shangaa jinsi watu wanavyoishi kwa hofu na mashaka. Lakini likitokea jambo dogo tu hapa Bongo utasikia wanalikimbiza ubalozi wa Marekani hivi vijana mnakwama wapi? Mnalijua vizuri taifa hili?
Watu wamekuwa wakilalamikia polisi wa Tanzania kuwa hawatendi haki mimi sibishi, sasa nenda kaangalie polisi wa Marekani utarudi spidi mwenyewe bongo
Marekani ndiyo nchi pekee iliyobaki ambapo inawaumiza sana nduguzetu weusi kwa kuwabagua katika kila jambo si elimu, afya na haki zingine za mtu na utu lakini mimi nashangaaga kuona mtu anakimbilia kujisalimisha kwa Marekani ni dhambi inayokutosha kukufikisha motoni, Marekani inaua, inapiga, inafunga, inanyanyasa, inatesa, sheria kandamizi wenyewe mmeshuhudia maandamano makubwa ambayo hayajawai tokea Huko Marekani tangia kuanzishwa kwa taifa hilo kwa kuuliwa Geoge Floyd. Hari ni mbaya nduguzangu huko Marekani mnakoona kimbilio
Angalia Marekani ilichokifanya Libya hadi leo hakuna taifa kama lile la Gadafi ambalo alikuwa hata na ombaomba 1, elimu bure, maji bure, umeme bure, afya bure lakini Marekani kuna omba omba fatilieni mambo. Leo hii Libya haina uchumi, haina chakula cha kutosha, hakuna huduma nzuri za afya tena, miundombinu imebomolewa wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe iliyochochewa na Marekani, Libya ni vita asubuhi mpaka asubuhi
Libya leo inatoa wakimbizi haya yote ni matokeo ya Marekani tena kwa kigezo cha kuwa eti Libya haikuwa na democrasia jamani tumswalie Mtume, huko marekani kuna democrasia? wana nchi wa Libya wanajuta mwaka jana walikuwa wanatimiza mika kama 8 hivi tangia kupinduliwa kwa gadafi wengi walikusanyika juu ya kaburi la Kanal Muhal Gadafi kuomba dua ya msamaha lakini majuto ni mjukuu.
Iraq leo hari ni mbaya kuliko wakati wowote hata juzi wananchi walipokuwa wanaambiwa kuwa kuna Korona hawakuiogopa kwani wao wanamajanga makubwa mara 10 ya Korona, haya yote yamesababiswa na Marekani. Baada ya Marekani kumuondoa Sadam Hussen leo hakuna ile Iraq ya Sadam ni vilio na kusaga meno kasome utaona mambo ya ajabu sana.
Nchi ya Liberia ambayo ni koloni la Marekani wamekuwa na hari mbaya tangia kurudishwa kwa manegro kutoka Marekani hari yao ni mbaya sana na hata leo nchi hiyo ambayo imepita katika vipindi vigumu vigumu ni chini maskini ya chini kutoka chini lakini bado ukiangalia bendera yao iko kopilaiti na ya Marekani. Ni taifa ambalo Marekani ilihakikisha inaligawa kwa maslai yake binafsi ndiyo maana katika Afrika Liberia ndiyo taifa linaloongoza kwa ukabila Afriaka na Duniani ni balaa nenda ukasome utaona vitu vya ajabu Marekani wamevijenga.
Tulishuhudia Geoge W Bush alipokuja Bongo alitoa zawadi ya vyandarua, Kweli. Yaani taifa kubwa kama hilo linatupa sisi vyandarua vya mbu wakati lilikuwa na uwezo wa kumdhibiti mbu kabla hajafika ndani, mbona Baba wa taifa Nyerere aliweza kudhibiti mbu, sisi tukiwa wadogo hakukuwa na vyandarua kama sasa nakumbuka kulikuwa na utaratibu wa kumwaga dawa katika manyumba yetu kila sehemu yenye maji maji kama choo, bafu, mitaro na kadhalika tena ilikuwa bure sasa Bush anatuletea chandarua chenye dawa, kumbe dawa ya kumuua mbu ipo ila yeye anachanganya hapo hapo, hiyo ndiyo Marekani mnayo itukuza.
Angalia jinsi walivyo mmisilidi Mzee Mkapa wakati wauongozi wake maana vuvuzela lilipigwa na nakumbuka wote tuliaminishwa kuwa huwezi kuwa na viwana au nchi ya viwanda kama unafuata siasa za ujamaa na kujitegemea au ukomunist. Hayo yalikuwa mafundisho kutoka Marekani na Mzee Mkapa akaingia mkenge bila kujua na zile kelele zilimchanganya akaviuza viwanda vyote na vikafa yaani ubinafsi-shaji hiyo ndiyo Marekani.
Kuwa na viwanda haijalishi uko katika mfumo gani wa siasa viwanda ni maisha na maisha ni viwanda, hata Adam na Eva Mungu alipowaacha katika busta ya Edeni walianzisha viwanda, hata kabla ya mwarabu au mzungu kuja Afriaka tayari tulikuwa na viwanda. Ndugu zangu wametudanganya vya kutosha, wametudharau vya kutosha na wameturudisha nyuma vya kutosha sasa tuanze kuachana na fikra za Marekani vijana tunapotea tutalipeleka wapi taifa hili.
Nampongea Dkt Magufuli hata kuwakatila njia wanazotumia wazungu kupambana na Korona Marekani na wazungu wanaamini katika loludouni lakini sisi hatuamini kufungia watu na njia zetu zimezaa matunda si kila kitu kufuata Marekani, Marekani leo Korona imenywea yenyewe hakuna mtu anaeamini.
Nchi ya Namibia nduguzangu imepita katika nyakati ngumu sana nendeni mkasome mtaona yote yaliyotokea yalikuwa na mkono wa Marekani, angalia Savimbi njinsi alivyotumika na Marekani na Kaburu Bota utaona vitu vya ajabu sana na kusikitisha, Utajiri wa Almasi Namibia ulikuwa laana kwao, angalia leo jinsi inavyotengeneza mashirika ya kiterolist na kujitoa muhanga hadi wasilamu wenyewe wanashangaa hii ni Marekani.
Tuanze kubadilika vijana. Maana pia nimesikia kunamtu anataka uraisi yeye anasema Marekani wanataka yeye ndiyo awe raisi wa Tanzania.
Mimi huko nyuma nilikuwa nikiamini kuwa Marekani ndiyo taifa ambalo linaongoza kwa kuwa na democrasia kubwa na pana kuliko nchi yoyote hile Duniani kumbe siyo, ukifika Amerika unaweza shangaa jinsi watu wanavyoishi kwa hofu na mashaka. Lakini likitokea jambo dogo tu hapa Bongo utasikia wanalikimbiza ubalozi wa Marekani hivi vijana mnakwama wapi? Mnalijua vizuri taifa hili?
Watu wamekuwa wakilalamikia polisi wa Tanzania kuwa hawatendi haki mimi sibishi, sasa nenda kaangalie polisi wa Marekani utarudi spidi mwenyewe bongo
Marekani ndiyo nchi pekee iliyobaki ambapo inawaumiza sana nduguzetu weusi kwa kuwabagua katika kila jambo si elimu, afya na haki zingine za mtu na utu lakini mimi nashangaaga kuona mtu anakimbilia kujisalimisha kwa Marekani ni dhambi inayokutosha kukufikisha motoni, Marekani inaua, inapiga, inafunga, inanyanyasa, inatesa, sheria kandamizi wenyewe mmeshuhudia maandamano makubwa ambayo hayajawai tokea Huko Marekani tangia kuanzishwa kwa taifa hilo kwa kuuliwa Geoge Floyd. Hari ni mbaya nduguzangu huko Marekani mnakoona kimbilio
Angalia Marekani ilichokifanya Libya hadi leo hakuna taifa kama lile la Gadafi ambalo alikuwa hata na ombaomba 1, elimu bure, maji bure, umeme bure, afya bure lakini Marekani kuna omba omba fatilieni mambo. Leo hii Libya haina uchumi, haina chakula cha kutosha, hakuna huduma nzuri za afya tena, miundombinu imebomolewa wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe iliyochochewa na Marekani, Libya ni vita asubuhi mpaka asubuhi
Libya leo inatoa wakimbizi haya yote ni matokeo ya Marekani tena kwa kigezo cha kuwa eti Libya haikuwa na democrasia jamani tumswalie Mtume, huko marekani kuna democrasia? wana nchi wa Libya wanajuta mwaka jana walikuwa wanatimiza mika kama 8 hivi tangia kupinduliwa kwa gadafi wengi walikusanyika juu ya kaburi la Kanal Muhal Gadafi kuomba dua ya msamaha lakini majuto ni mjukuu.
Iraq leo hari ni mbaya kuliko wakati wowote hata juzi wananchi walipokuwa wanaambiwa kuwa kuna Korona hawakuiogopa kwani wao wanamajanga makubwa mara 10 ya Korona, haya yote yamesababiswa na Marekani. Baada ya Marekani kumuondoa Sadam Hussen leo hakuna ile Iraq ya Sadam ni vilio na kusaga meno kasome utaona mambo ya ajabu sana.
Nchi ya Liberia ambayo ni koloni la Marekani wamekuwa na hari mbaya tangia kurudishwa kwa manegro kutoka Marekani hari yao ni mbaya sana na hata leo nchi hiyo ambayo imepita katika vipindi vigumu vigumu ni chini maskini ya chini kutoka chini lakini bado ukiangalia bendera yao iko kopilaiti na ya Marekani. Ni taifa ambalo Marekani ilihakikisha inaligawa kwa maslai yake binafsi ndiyo maana katika Afrika Liberia ndiyo taifa linaloongoza kwa ukabila Afriaka na Duniani ni balaa nenda ukasome utaona vitu vya ajabu Marekani wamevijenga.
Tulishuhudia Geoge W Bush alipokuja Bongo alitoa zawadi ya vyandarua, Kweli. Yaani taifa kubwa kama hilo linatupa sisi vyandarua vya mbu wakati lilikuwa na uwezo wa kumdhibiti mbu kabla hajafika ndani, mbona Baba wa taifa Nyerere aliweza kudhibiti mbu, sisi tukiwa wadogo hakukuwa na vyandarua kama sasa nakumbuka kulikuwa na utaratibu wa kumwaga dawa katika manyumba yetu kila sehemu yenye maji maji kama choo, bafu, mitaro na kadhalika tena ilikuwa bure sasa Bush anatuletea chandarua chenye dawa, kumbe dawa ya kumuua mbu ipo ila yeye anachanganya hapo hapo, hiyo ndiyo Marekani mnayo itukuza.
Angalia jinsi walivyo mmisilidi Mzee Mkapa wakati wauongozi wake maana vuvuzela lilipigwa na nakumbuka wote tuliaminishwa kuwa huwezi kuwa na viwana au nchi ya viwanda kama unafuata siasa za ujamaa na kujitegemea au ukomunist. Hayo yalikuwa mafundisho kutoka Marekani na Mzee Mkapa akaingia mkenge bila kujua na zile kelele zilimchanganya akaviuza viwanda vyote na vikafa yaani ubinafsi-shaji hiyo ndiyo Marekani.
Kuwa na viwanda haijalishi uko katika mfumo gani wa siasa viwanda ni maisha na maisha ni viwanda, hata Adam na Eva Mungu alipowaacha katika busta ya Edeni walianzisha viwanda, hata kabla ya mwarabu au mzungu kuja Afriaka tayari tulikuwa na viwanda. Ndugu zangu wametudanganya vya kutosha, wametudharau vya kutosha na wameturudisha nyuma vya kutosha sasa tuanze kuachana na fikra za Marekani vijana tunapotea tutalipeleka wapi taifa hili.
Nampongea Dkt Magufuli hata kuwakatila njia wanazotumia wazungu kupambana na Korona Marekani na wazungu wanaamini katika loludouni lakini sisi hatuamini kufungia watu na njia zetu zimezaa matunda si kila kitu kufuata Marekani, Marekani leo Korona imenywea yenyewe hakuna mtu anaeamini.
Nchi ya Namibia nduguzangu imepita katika nyakati ngumu sana nendeni mkasome mtaona yote yaliyotokea yalikuwa na mkono wa Marekani, angalia Savimbi njinsi alivyotumika na Marekani na Kaburu Bota utaona vitu vya ajabu sana na kusikitisha, Utajiri wa Almasi Namibia ulikuwa laana kwao, angalia leo jinsi inavyotengeneza mashirika ya kiterolist na kujitoa muhanga hadi wasilamu wenyewe wanashangaa hii ni Marekani.
Tuanze kubadilika vijana. Maana pia nimesikia kunamtu anataka uraisi yeye anasema Marekani wanataka yeye ndiyo awe raisi wa Tanzania.