Half american
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 25,749
- 67,442
Kwa mujibu wa mtaalamu wa Psychiatry, magonjwa ya akili miongoni mwa wakina mama walioko kwenye ndoa ni mengi sana na yanawasababishia kufanya mabaya kwa wenzi wao, mfano ndo kama huu hapa:
Picha hii inamuonesha mwanaume mmoja nchini Kenya ajulikanae kwa jina la Dan Shisia Matakhaya, mwenye umri wa miaka 31 na ni Askari polisi nchini humo.
Hakuzaliwa na sura ya kutisha namna hii. Unachokiona ni matokeo ya mabishano kati yake na mke wake.
Siku moja, Matakhaya na mke wake walipishana kuhusu masuala kadhaa ya kifamilia, yeye alichukulia mtafaruko au mapishano hayo kama kitu cha kawaida tu na baadae siku hiyohiyo akaenda kazini. Aliingia zamu ya usiku na kurudi kesho yake majira ya saa kumi na moja na nusu alfajiri.
Kwasababu alifanya kazi usiku kucha, baada ya kurudi nyumbani alienda moja kwa moja kitandani na kulala.
Huo ukawa wakati mzuri kwa mke wake kuja na kumwagia tindikali usoni. Kisha mkewe akakimbia na kuondoka zake. Lakini haikutosha kwa mwanamke huyo kuiharibu sura ya mumewe, akalimwaga pia maji sakafuni na kuunganisha nyaya za umeme ilikusudi mumewe akikanyaga maji yale apigwe shoti ya umeme, na mumewe kweli alikanyaga maji yale na kurushwa na shoti ya umeme.
Alipokuwa akipiga kelele,majirani walikuja wakamkuta ameanguka hajitambui na haelezeki. Majrani wakampeleka hospitalini. Maisha yake yakaokolewa, lakini macho yake yakapofuka kabisa.
Mke wake alikamatwa na baadaye kuachiwa kwa dhamana ili kungoja kesi mahakamani. Matakhaya akamsamehe mke wake kwa yote aliyoyafanya japo akasema hatoweza kuondoa kesi mahakamani dhidi ya mwanamke huyo.
Amekutana naye mara moja mahakamani kisha mwanamke huyo akasema hajui ni kwanini alifanya hayo ya aibu na hatari kweli kweli!
Hapa ndipo utajua muishipo watu wawili na zaidi yawapasa kuomba amani kwa Mwenyezi Mungu, maana mmeingia kwenye hali ya hatari endapo shetani akajipenyeza kwa mmoja wenu.
Matakhaya alisoma sheria na kufuzu Shahada ya suala jinai (criminology). Anajitahidi sasa kila siku kuendana na maisha yake mapya. Ndoto yake ni kuwa kiongozi wa mfano kwenye harakati za kupambana na unyanyasaji majumbani (Domestic violence).
NB: Mkipishana kauli kwenye familia hakikisheni mnatumia muda na akili alikadhali hekima kufikia mwafaka, kuanzisha mtafaruko na kuondoka unarudi huna hata muda wa kuwekana sawa ni jambo la hatari sana wewe baba na wewe mama mkae mkilijua hilo. Inasikitisha sana.
Picha hii inamuonesha mwanaume mmoja nchini Kenya ajulikanae kwa jina la Dan Shisia Matakhaya, mwenye umri wa miaka 31 na ni Askari polisi nchini humo.
Hakuzaliwa na sura ya kutisha namna hii. Unachokiona ni matokeo ya mabishano kati yake na mke wake.
Siku moja, Matakhaya na mke wake walipishana kuhusu masuala kadhaa ya kifamilia, yeye alichukulia mtafaruko au mapishano hayo kama kitu cha kawaida tu na baadae siku hiyohiyo akaenda kazini. Aliingia zamu ya usiku na kurudi kesho yake majira ya saa kumi na moja na nusu alfajiri.
Kwasababu alifanya kazi usiku kucha, baada ya kurudi nyumbani alienda moja kwa moja kitandani na kulala.
Huo ukawa wakati mzuri kwa mke wake kuja na kumwagia tindikali usoni. Kisha mkewe akakimbia na kuondoka zake. Lakini haikutosha kwa mwanamke huyo kuiharibu sura ya mumewe, akalimwaga pia maji sakafuni na kuunganisha nyaya za umeme ilikusudi mumewe akikanyaga maji yale apigwe shoti ya umeme, na mumewe kweli alikanyaga maji yale na kurushwa na shoti ya umeme.
Alipokuwa akipiga kelele,majirani walikuja wakamkuta ameanguka hajitambui na haelezeki. Majrani wakampeleka hospitalini. Maisha yake yakaokolewa, lakini macho yake yakapofuka kabisa.
Mke wake alikamatwa na baadaye kuachiwa kwa dhamana ili kungoja kesi mahakamani. Matakhaya akamsamehe mke wake kwa yote aliyoyafanya japo akasema hatoweza kuondoa kesi mahakamani dhidi ya mwanamke huyo.
Amekutana naye mara moja mahakamani kisha mwanamke huyo akasema hajui ni kwanini alifanya hayo ya aibu na hatari kweli kweli!
Hapa ndipo utajua muishipo watu wawili na zaidi yawapasa kuomba amani kwa Mwenyezi Mungu, maana mmeingia kwenye hali ya hatari endapo shetani akajipenyeza kwa mmoja wenu.
Matakhaya alisoma sheria na kufuzu Shahada ya suala jinai (criminology). Anajitahidi sasa kila siku kuendana na maisha yake mapya. Ndoto yake ni kuwa kiongozi wa mfano kwenye harakati za kupambana na unyanyasaji majumbani (Domestic violence).
NB: Mkipishana kauli kwenye familia hakikisheni mnatumia muda na akili alikadhali hekima kufikia mwafaka, kuanzisha mtafaruko na kuondoka unarudi huna hata muda wa kuwekana sawa ni jambo la hatari sana wewe baba na wewe mama mkae mkilijua hilo. Inasikitisha sana.