Hivi inakuajekuaje kati ya mamilioni ya watu, unaibuka kupata bahati ya kuwa Rais wa Nchi?

Yeremia 1:5
Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua,
kabla hujatoka tumboni nalikutasaka.
Nimekuweka kuwa nabii wa mataifa

Kwa mazingira ya kawaida raisi wa nchi anapatikana kwenye sanduku la kura lakini Kiuhalisia Raisi wa Nchi anakuwa ni Raisi Tangu tumboni mwa mama yake..
 
Hiyo ni mipango yake Mola Maulana

Ukitafakari Mzee Mwinyi alipataje Urais wa Znz na Tanzania utashangaa sana tena mbele ya Magwiji

1977 anajiuzulu uwaziri,

1983 anarudishwa Nyumbani toka Ubalozini Misri anakuwa 'Baba wa Nyumbani' kwa miezi 11 hadi anatokea Mlemavu wa macho a.k.a Kawawa wa Znz (Sheikh Thabit Kombo) Katibu mstaaf wa ASP anaombwa ushaurh na MWL Nyerere nani amrithi Jumbe …nae anamtaja Ally

MWINYI KATOKEA BENCHI
Jidanganye tu huo muda mwinyi alikuwa anaroga,bila uchawi ukanyagi ikulu
 
Jidanganye tu huo muda mwinyi alikuwa anaroga,bila uchawi ukanyagi ikulu
Aliyekwambia kuwa kiongozi akiwa mchawi hakupangwa na Mungu ni nani.....

Kasome Biblia Kuhusu Farao.....alikuwa ni mchawi haswa mpaka Fimbo ya Musa ilipogeuka nyoka na wachawi wa farao waligeuza fimbo kuwa Nyoka...
Lakini Maandiko yanamtaja Farao kama mtumishi wa Mungu

Nebukadreza alikuwa Mchawi 1st class na alisimamisha sanamu kubwa ya dhahabu lakini Mungu anamuita mtumishi wake
↓↓↓ soma hiyo Yeremia na utafakari kwa makini huo mstari wa 9
Screenshot_20210712-090442.jpg
 
Bado najiuliza ni bahati iliyoje kati ya mamilioni ya watu MTU mmoja tuu unapata bahati ya kuwa rais wa Nchi,cheo ambacho unaweza kuwataka watu wote wasitoke majumbani,ukiagiza ghorofa lijengwe linajengwa japo litachelewa,

Mliosoma history za viongozi mtujuze makuzi ya watu hawa huwa yakoje mpaka kupata bahati hii kubwa.
Utoto bwana!
 
Aliyekwambia kuwa kiongozi akiwa mchawi hakupangwa na Mungu ni nani.....

Kasome Biblia Kuhusu Farao.....alikuwa ni mchawi haswa mpaka Fimbo ya Musa ilipogeuka nyoka na wachawi wa farao waligeuza fimbo kuwa Nyoka...
Lakini Maandiko yanamtaja Farao kama mtumishi wa Mungu

Nebukadreza alikuwa Mchawi 1st class na alisimamisha sanamu kubwa ya dhahabu lakini Mungu anamuita mtumishi wake
↓↓↓ soma hiyo Yeremia na utafakari kwa makini huo mstari wa 9
View attachment 1850297
Unaamini hizo story za kutunga za waisrael,we maji yajigawe mara mbili sijui nini,hizo ni hekaya tu
 
Unaamini hizo story za kutunga za waisrael,we maji yajigawe mara mbili sijui nini,hizo ni hekaya tu
Inaweza kuwa siyo kwa ajili yako...hapa JF wako watu tofauti tofauti...kama wewe unaziita hekaya na hauamini acha watakuja wanaoamini na watajifunza kitu.....
Siyo kila kinachoandikwa humu ni kwa faida yako Binafsi...
Kisipokufaa wewe kitawafaa wengine...
Mleta mada ameuliza swali na hajachagua ajibiwe kwa namna gani ....kwa hiyo kila mtu anajibu kulingana na anavyoamini na mleta mada atachagua jibu lipi linamfaa...

Haya ni maoni yangu...unaweza kuwa na yako.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom