Hivi ilikuwaje kwa Prof. Jay na Rashida Wanjara?

Interest

JF-Expert Member
Apr 11, 2015
3,432
7,055
Sisi wengine mambo ya siku hizi hayatunogei. Bora tukumbukie ya zamani tu!

Kwa wafuatiliaji wa game hii ya burudani, watakumbuka jinsi Prof Jay alivyokuwa akiburuzwa na penzi la mwanadada sistaduu aliyewahi kuwa Miss Mara, Miss Kanda ya Ziwa na Miss Tanzania (Top 5) miaka hiyo, Rashida Wanjara.

DF39851A-6F8D-4080-9BD1-3BE29B1447CB.jpeg


Profesa akiwa mmoja wa wasanii bora sana kipindi hicho, labda tuseme namba 1 kwa upande wa Hiphop, alifikia hatua ya kugombana mpaka na baadhi ya wasanii wenzake pale walipomchana ukweli kuwa huyu dada ni mdangaji tu atakuja kumletea matatizo na kumharibia career yake/heshima aliyonayo.

Kuna tape fulani ya Kikosi cha Mizinga ilivuja, ambapo pamoja na mambo mengine, walisikika kina Kala Pina wakimnanga Prof. kwamba "kaungua" kwa sababu ya kujilipua kwa demu supastaa mdangaji. Rashida???

Tangu hapo, Jay kama alikosa utulivu hivi wa kisaikolojia, ambapo ilipelekea awe anajitetea kwenye kila ngoma anayoachia, akidai anasingiziwa mengi ikiwemo kuwa ameathirika. Wanaofuatiliaga ngoma zake wanajua.

01A17327-CADC-4C63-A927-2772BB4D854A.jpeg


Leo Rashida ni boss wa Bunyero Bunyero. Project fulani hivi ya wasasambuaji wenye misambwanda. Inadaiwa humo ndani anauza mpaka mapunga. Watu wa chimbo za town wanaelewa vizuri. WCB team ni VIP pale!

Haya mambo yalitokea. Huenda sio kwa 100% kama nilivyoeleza lakini yalitokea. Najua wenye kumbukumbu nzuri zaidi watakuja kujazia jazia ili kuweka rekodi sawa.

Ni muhimu vijana wa kileo wakafahamu mambo yalivyo ili wanapoona mtu kama Profesa Jay amefanikiwa kwenye muziki na mambo mengine yakiwemo siasa, waelewe kapitia dhoruba nyingi. Wasichukulie poa!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom