Hivi ile video kamera aliyokuwa anatumia Marehemu Daudi Mwangosi ipo wapi?

Lyimo

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
3,826
2,017
Ni dhahiri kuwa Marehemu Daudi Mwangosa alikuwa akichukua matukio mablimbali katika matafaruku wa Polisi na wafuasi wa CDM pale Nyororo (Mfindi). Bilashaka kumbukumbu alizokuwa akichukua za kuonyesha jinsi polisi wakiwashambulia wananchi, polisi hawakupenda hilo. Pia tumemshuhudia akiwa ameishiishikilia mkononi pale alipokuwa anashambuliwa na kundi la polisi kabla hajalipuliwa na bomu. Bila shaka Kamera yake ingekuwa na matukio mengi muhimu ambayo yangetumika kama ushahidi wa mauaji yake. Kama itakuwa haijapatikana, tunaomba hiyo TUME inayofatilia iulizie chombo chake hiki na kuona kama kumbukumbu zake hazijaharibiwa. Tunasikitika sana kwa msiba wa mwanahabari huyu aliyeuwawa kinyama na chombo cha dola chenye mamlaka ya kulinda raia. Tunazidi kusisitiza uwajibikakaji/uwajibishwaji wa kila mtu aliyehusika kwa namna moja ama nyingine ili tuweze kurudisha imani kwa serikali yetu. Mungu awape faraja ndugu na jamaa wote walioguswa na msiba huu. Mungu amlaze mahali pema marehemu Daudi Mwangosa, AMEN.

View attachment 63880
 
Nadhani yale mambwa koko yameshaitafuna tafuna hiyo! ikipatikana itakuwa ni hot cake sana ktk kusaidia uchunguzi!
 
Back
Top Bottom