Hivi ilani ya uchaguzi ya cuf huko zenj, nayo imeunganishwa na ile ya ccm?

Byendangwero

JF-Expert Member
Oct 24, 2010
871
56
Katika hotuba yake aliyoitoa mda mfupi baada ya Shein kutangazwa mshindi katika kinyanganyiro cha urais wa zenj Maalim Seif alisema hapekuwepo mshindi. Kauli yake hiyo kwangu mimi ina maana kwamba, ilani za uchaguzi zote mbili, ile ya ccm pamoja na ile ya cuf, machoni mwawazenj, zilikuwa na mvuto unaolingana. Kama hivyo ndivyo, maadam vyama hivyo hivi sasa vimeunda serikali ya umoja, basi na ilani zote mbili zingelijumuishwa pamoja kwaajili ya utekelezaji. Hayo ndiyo huwa yanafanyika kwa wenzetu katika nchi zilizoendelea, mara zote vyama zaidi ya kimoja vinapoungana kuunda serikali. Kuna anayeweza kunijulisha mambo yakoje huko Zenj kuhusiana na suala hilo.
 
Thubutu!!ccm hawawezi kuwapa hiyo chance,kwa taarifa yako cuf ni watumwa kwenye hiyo serikali,labda kilicho wazi viöngozi wa cuf wameona bora nao wawemo ktk mgao wa keki ya taifa-siasa hakuna ni usanii m2pu
 
Back
Top Bottom