Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Katika hotuba yake aliyoitoa mda mfupi baada ya Shein kutangazwa mshindi katika kinyanganyiro cha urais wa zenj Maalim Seif alisema hapekuwepo mshindi. Kauli yake hiyo kwangu mimi ina maana kwamba, ilani za uchaguzi zote mbili, ile ya ccm pamoja na ile ya cuf, machoni mwawazenj, zilikuwa na mvuto unaolingana. Kama hivyo ndivyo, maadam vyama hivyo hivi sasa vimeunda serikali ya umoja, basi na ilani zote mbili zingelijumuishwa pamoja kwaajili ya utekelezaji. Hayo ndiyo huwa yanafanyika kwa wenzetu katika nchi zilizoendelea, mara zote vyama zaidi ya kimoja vinapoungana kuunda serikali. Kuna anayeweza kunijulisha mambo yakoje huko Zenj kuhusiana na suala hilo.