Hivi ikiwa mdaiwa ameshindwa kulipa deni baada ya muda uliopangwa na mahakama nini kinafuata na ikiwa mdaiwa hana mali yoyote.

Ligaba

JF-Expert Member
Oct 12, 2018
1,045
2,821
Mnaojua sheria maomba msaada katika hili. Nilikuwa na kesi ya wizi na kukabwa mtaani, kesi iliisha kwa mtuhumiwa kufungwa miezi sita kwa kila kosa, kwa makosa mawili au kila kosa fine ya Tsh. 150,000/= ambayo mkosaji alilipiwa. Vilevile alitakiwa kulipa fedha alizochukua wakati wa tukio na simu aliyochukua jumla ikiwa 2,750,000/=.

Tangu ipite hukumu huu ni mwezi wa 5 na sioni dalili kama atalipa ndani ya miezi 6 aliyotakiwa na mkosaji hana mali za thamani ya fedha anazopaswa kulipa. Swali langu kwenu wanasheria, ikiwa muda umeisha na hajalipa ni nini kitatokea kwa mkosaji au napaswa nifanye nn ili niipate haki zangu?



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo aliekukaba hakuwa na wadhamini?

Kesi ilifunguliwa ni madai au jinai?

Makubaliano ya kulipana ilikuaje kwamba atakua anapeleka pesa mahakamani au atakulipa wewe mwenyewe..

Kama ni madai amini ukimfunga,akiwa gerezani itakupasa uwe unampelekea chakula,

Ikipita muda hajakulipa hata kidogo nenda mahakamani kakaze hukumu...

Mimi sio mwanasheria nawachokoza tu wenye fani yao waje kujibu kisomi zaidi
 
Kinachotakiwa kufuata ni kufuta deni, kifupi unasamehe na kusahau kama kuna unaemdai. Samehe saba mara sabini.
 
Huyo aliekukaba hakuwa na wadhamini?

Kesi ilifunguliwa ni madai au jinai?

Makubaliano ya kulipana ilikuaje kwamba atakua anapeleka pesa mahakamani au atakulipa wewe mwenyewe..

Kama ni madai amini ukimfunga,akiwa gerezani itakupasa uwe unampelekea chakula,

Ikipita muda hajakulipa hata kidogo nenda mahakamani kakaze hukumu...

Mimi sio mwanasheria nawachokoza tu wenye fani yao waje kujibu kisomi zaidi

Shukrani
Kesi ilifunguliwa ya Jinai.
Makubaliano ni kwamba hela atalipa mahakamani.
Nashukuru kwa ushauri, jana nimefika na nilipatiwa barua ya kumwita mahakamani. Tarehe 1/2 nitakupa mrejesho.
 
Kinachotakiwa kufuata ni kufuta deni, kifupi unasamehe na kusahau kama kuna unaemdai. Samehe saba mara sabini.

Ni kweli mkuu ila nimeshavua nguo acha tu maji nioge, niliumia sana na kila nikikumbuka manyuzi niliyo shonwa nakosa kabisa usamehefu. Labda mungu aniongoze upya.
 
Huyo aliekukaba hakuwa na wadhamini?

Kesi ilifunguliwa ni madai au jinai?

Makubaliano ya kulipana ilikuaje kwamba atakua anapeleka pesa mahakamani au atakulipa wewe mwenyewe..

Kama ni madai amini ukimfunga,akiwa gerezani itakupasa uwe unampelekea chakula,

Ikipita muda hajakulipa hata kidogo nenda mahakamani kakaze hukumu...

Mimi sio mwanasheria nawachokoza tu wenye fani yao waje kujibu kisomi zaidi
Mkuuu hapo unakaza hukumu na watakao beba mzigo ni wadhamini
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom