Dotto Athumani
Senior Member
- Feb 11, 2012
- 106
- 23
Napata shida sana kuelewa pengine ni ujinga wangu au kwa kuwa nimekosa pa kuaminia. Kila napomuona Rais anapost jambo kwenye facebook au Twitter afu nchi inajadili jambo tofauti kabisa huwa sielewi kabisa. Unaambiwa Rais yuko busy akishughulikia masuala muhimu nchi inayumba lakini ukiingia kwenye mitandao ya kijamii unamkuta busy akiweka mijadala kwenye facebook/twitter. Nisaidie hivi huyu ni Rais huyu huyu au kuna mtu kapewa jukumu hilo pale Ikulu, na je ni sahihi kama anaeweka posts hizo si Rais na bado anatumia jina hilo?