Tegelezeni
JF-Expert Member
- Dec 31, 2009
- 268
- 124
Ni jirani yangu na wakati nahamia katika nyumba ninayoishi nilimkuta akiwa na mwanamke ambaye nilijua ni mkewe Baadae yule mwanamke akamwambia mke wangu kuwa yule mwanaume anaye mkewe ambaye walioana na kuzaa naye watoto wawili, na walidumu katika ndoa kwa miaka saba na kutengana hivyo akarudi Mkoani na ndipo akachukuliwa yeye na kuja kupangishiwa nyumba hapa jirani na tunapoishi. (wameishi bila ndoa miaka 3 na wala hawajapata mtoto).
Huyu bwana ni mtu wa kusafiri mara kwa mara hivyo sina mazoea naye. Siku za hivi karibuni huyu bwana alinijia akitaka nimweleze kama huyu mwanamke wake (ngoja nimuite hawara yake) ni Malaya? Nilimwambia sijui lolote kwa kuwa mimi sishindi hapa nyumbani. Ilipofika usiku nikasikia ugomvi wakipigana na huyo hawara yake, na ilipofika asubuhi nikamuona huyo mwanamke anafungasha na kuondoka. Siku huyu jamaa alipokuwa anasafiri alinijulisha kwamba nisije shangaa maana mkewe wa ndoa anakuja kutoka mkoani na ni yeye atakayekuwa akiishi hapo.
Ni kweli mke alikuja na kujitambulisha kwetu kama jirani. Lakini jana huyo mkewe kaja na kumweleza mke wangu kuwa mumewe kampigia simu kuwa yule hawara atakuja na kufikia hapo na kulala kwa siku moja kisha ataondoka na kuendelea na safari yake kwenda Arusha, hivyo amruhusu kulala hapo nyumbani lakini haruhusuwi kuchukua chochote. Yule hawara alifika kwa mbwembwe jana jioni na ilipofika usiku hatukulala, kwani alikuwa anamfanyia vurugu mke wa jamaa kwa kuvunja vyombo eti kwa madai kuwa walinunua wote na huyo mwanaume.
Huyu mwanamke wa ndoa mpaka sasa yuko kimya na anamwangalia tu jinsi huyo hawara anavyofanya vurugu na kuvunja vyombo na makabati, na hivi ninavyoandika hapa ninashuhudia vituko mbwembwe na tambo za huyo hawara akimfanyia mwenzake, lakini mwenzake kapiga kimya kama hakuna kitu.
Najiuliza:
1.Hivi huyu mwanaume ana akili kweli?
2. Je wakiuana humo ndani ya nyumba ni nani atakuwa responsible na hivyo vifo?
3. Hivi kweli unawezaje kuruhusu hawara aje afikie kwako wakati mkeo wa ndoa yupo na watoto, Je akiwadhuru watoto?
Mimi ni mwanaume lakini anavyofanya huyu mwenzangu simuelewi kabisa, au ndivyo wanaume wa kanda ya ziwa walivyo?
Hebu wale wadada na wakaka watetezi wa haki za ndoa hapa JF mkuje kutoa ushauri: gfsonwin, snowhite, King'asti, jouneGwalu, Mwita Maranya, Jiwe Linaloishi, nivea, FirstLady, sweetlady MwanajamiiOne, SnowBall, The Boss, Neylu, BADILI TABIA, nyumba kubwa, Dark City, Arushaone, Mungi, Preta, lara 1, giLESi, charminglady, cacico, Remmy, Bujibuji, Scofied, KakaKiiza, Kaizer na wengineo niliowasahau lakini wana michango yenye kujenga hapa MMU
Huyu bwana ni mtu wa kusafiri mara kwa mara hivyo sina mazoea naye. Siku za hivi karibuni huyu bwana alinijia akitaka nimweleze kama huyu mwanamke wake (ngoja nimuite hawara yake) ni Malaya? Nilimwambia sijui lolote kwa kuwa mimi sishindi hapa nyumbani. Ilipofika usiku nikasikia ugomvi wakipigana na huyo hawara yake, na ilipofika asubuhi nikamuona huyo mwanamke anafungasha na kuondoka. Siku huyu jamaa alipokuwa anasafiri alinijulisha kwamba nisije shangaa maana mkewe wa ndoa anakuja kutoka mkoani na ni yeye atakayekuwa akiishi hapo.
Ni kweli mke alikuja na kujitambulisha kwetu kama jirani. Lakini jana huyo mkewe kaja na kumweleza mke wangu kuwa mumewe kampigia simu kuwa yule hawara atakuja na kufikia hapo na kulala kwa siku moja kisha ataondoka na kuendelea na safari yake kwenda Arusha, hivyo amruhusu kulala hapo nyumbani lakini haruhusuwi kuchukua chochote. Yule hawara alifika kwa mbwembwe jana jioni na ilipofika usiku hatukulala, kwani alikuwa anamfanyia vurugu mke wa jamaa kwa kuvunja vyombo eti kwa madai kuwa walinunua wote na huyo mwanaume.
Huyu mwanamke wa ndoa mpaka sasa yuko kimya na anamwangalia tu jinsi huyo hawara anavyofanya vurugu na kuvunja vyombo na makabati, na hivi ninavyoandika hapa ninashuhudia vituko mbwembwe na tambo za huyo hawara akimfanyia mwenzake, lakini mwenzake kapiga kimya kama hakuna kitu.
Najiuliza:
1.Hivi huyu mwanaume ana akili kweli?
2. Je wakiuana humo ndani ya nyumba ni nani atakuwa responsible na hivyo vifo?
3. Hivi kweli unawezaje kuruhusu hawara aje afikie kwako wakati mkeo wa ndoa yupo na watoto, Je akiwadhuru watoto?
Mimi ni mwanaume lakini anavyofanya huyu mwenzangu simuelewi kabisa, au ndivyo wanaume wa kanda ya ziwa walivyo?
Hebu wale wadada na wakaka watetezi wa haki za ndoa hapa JF mkuje kutoa ushauri: gfsonwin, snowhite, King'asti, jouneGwalu, Mwita Maranya, Jiwe Linaloishi, nivea, FirstLady, sweetlady MwanajamiiOne, SnowBall, The Boss, Neylu, BADILI TABIA, nyumba kubwa, Dark City, Arushaone, Mungi, Preta, lara 1, giLESi, charminglady, cacico, Remmy, Bujibuji, Scofied, KakaKiiza, Kaizer na wengineo niliowasahau lakini wana michango yenye kujenga hapa MMU
Last edited by a moderator: