Tegelezeni
JF-Expert Member
- Dec 31, 2009
- 268
- 124
- Thread starter
- #61
Bado haiondoi hadhi yake kama mke halali kwa mujibu wa sheria unless kama alipodundwa alikabidhiwa na talaka yake otherwise mume huyo anao wake wawili mpaka sasa. Kuishi na mwanamke miaka 7 kama mke ni mkewe halali. Hayo ya kutokuwa mwaminifu, sijui kicheche hayaondoi title ya mke au mume ndoani unless talaka imehusika.
Kwa taarifa hii ninaanza kupata picha mpya kabisa ya tukio hili. Inawezekana sasa mume amelitambua kosa lake la kumtelekeza mke mkubwa sasa ametaka kumrudisha lakini akajisahau kuwa ALIOA mke wa pili (hata kama hakufunga nae ndoa) so mke wa pili nae anayo haki ya kumclaim yeye kama mumewe. Ila swali ni kwamba alikuwa akiwaza nini kuwaweka mahali pamoja?
Na huyo mama wa ndoa mwambie aache ujinga anasafisha nyumba ya nini aache mumewe aje ashuhudie ukuchaa wa bi mdogo wake, ye anatupa vidhibit?
Ninavyofahamu mimi hata dini inayoruhuru kuoa wake wengi mojawapo ya masharti ni kutowaweka katika nyumba moja. lakini hata kama unasema wote ni wake zake mimi sioni logic, maana jamaa alioa Kiislamu huyu mke wa ndoa, lakini huyu hawara ni M-Lutheran na ndio hapo najiuliza itakuwa ni ndoa ya aina gani hapo?