Hivi huwa nini kinajadiliwa kwenye Baraza la Mawaziri? Kuna umuhimu gani wa kutupa taarifa kuwa wamekutana?

The Phylosopher

JF-Expert Member
Mar 11, 2015
1,503
2,046
Naombeni wanaoelewa sana mambo haya wanisaidie kufahamu. Inavyoonekana kikao cha Baraza la Mawaziri huwa ni cha siri. Kinachonisumbua ni kwamba mara nyingi wakikutana kwa kikao tunajulishwa kuwa wamekutana.

Na kwenye hilo Baraza huwa mambo gani hujadiliwa na vikao vya siku ngapi?
 
Na kwa sababu wanaapa kutunza siri za Baraza la Mawaziri, hakuna sababu ya sisi kujua wanakaa lini na wapi maana yake hata vikao pia ni vya siri.Au Zuhura hands hicho kiapo?
 
Siri ina mipaka yake ya kutolewa, vikao vya baraza vya mawaziri ni moja ya vikao vya Siri mno na taarifa pekee ya kufanyika kwake inatosha.

Licha ya Siri zake lakini kuna matokeo baada ya vikao hivyo na hayo ndio Wananchi wayasubiri. Utekelezaji wa maazimio ya vikao ndio Jambo la msingi
 
Sio kila kitu kinachojadiliwa katika baraza la mawaziri ni siri.
Afya, maji, umeme, madarasa na mengine mengi sio siri.
Na kwa sababu wanaapa kutunza siri za Baraza la Mawaziri, hakuna sababu ya sisi kujua wanakaa lini na wapi maana yake hata vikao pia ni vya siri.Au Zuhura hands hicho kiapo?
 
Naombeni wanaoelewa sana mambo haya wanisaidie kufahamu. Inavyoonekana kikao cha Baraza la mawaziri huwa ni cha siri. Kinachonisumbua ni kwamba mara nyingi wakikutana kwa kikao tunajulushwa kuwa wamekutana.

Na kwenye hilo Baraza huwa mambo gani hujadiliwa na vikao vya siku ngapi?

Kichekesho ni pale wanapotokea chawa na kusema huo ndio uwazi tunaoutaka.
 
Hiyo impact ya kukutana kwao kwanza hata haionekani, Bora kusingekuwa na Baraza la mawazir tu
 
Naombeni wanaoelewa sana mambo haya wanisaidie kufahamu. Inavyoonekana kikao cha Baraza la Mawaziri huwa ni cha siri. Kinachonisumbua ni kwamba mara nyingi wakikutana kwa kikao tunajulishwa kuwa wamekutana.

Na kwenye hilo Baraza huwa mambo gani hujadiliwa na vikao vya siku ngapi?
Balaza la mawaziri la Tanzania lina kazi kupokea maelekezo ya rais na kushangilia kila kitu anachosema. Sio balaza la kujadili hoja na kutoa ushauri kama ilivyo kwenye nchi za kidemokrasia
 
Ni upuuzi tu, mambo ya hovyo kabisa. Ndio vikao ambavyo serikali ya CCM inavitumia kupitisha miradi ya kitapeli, manunuzi ya magari ya anasa (V8 n.k) na kufanya ufisadi
 
Nchi inaliwa tu, na ngono zembe juu..

Stupid.jpg
 
Back
Top Bottom