Ugiligili
JF-Expert Member
- Jun 20, 2014
- 3,023
- 4,050
Hii ni baada ya bomoabomoa ya vile vibanda vya chipsi inayoendelea nchi nzima..bomoabomoa iliacha watu vinywa wazi na kujiuliza kama walifanya makosa kumfanya yule mtu awe kiranja wao wa ule ukoo!
Saaa nikachanganyikiwa zaidi niliposikia lile banda la kuku linatakiwa kubomolewa! Nikajiuliza swali: JE kiranja wetu huwa nawauliza wahusika kuhusu njia yoyote au uwezekano wowote wa kulinusuru lile banda au vile vibanda vya chipsi kule kabla ya kuvibomoa!?
Je hawa wataalamu wetu huwa wanatoa ushauri wa kitaalamu hata kama unamuumiza kiranja!? Au huwa nao wanapindisha taaluma ili kwenda sawa na kiranja!?
Alafu yule kiranja wetu anasema anapunguza matumizi lkn nikiangalia hili banda likibomolewa itakuwaje!? Je kuna banda lingine limeshajengwa kwa ajili ya kazi hii..!? Je limejengwa kwa pesa ngapi!? Ss kama tukifanya namna yoyote kuinusuru hiyo pesa si tungeweza kuitumia kupelekea watoto shule!?
Baadae nikaiona picha kutoka ukoo wa jirani..picha ikionesha wataalamu wa ujenzi wamejenga njia ya juu inayofanana na yetu lakini imepindishwa vizuri ili kulikwepa banda moja kuubwa la kuku wao.nikawapa heko wale waheshimiwa wa ukoo ule kwa kufanya maamuzi yasioumiza upande mwingine.
Nisiwe muongo kwakweli lile banda la kuku litaniuma kama likibomolewa,kiranja nakuomba usikie haya.
Ni hayo tu.
Saaa nikachanganyikiwa zaidi niliposikia lile banda la kuku linatakiwa kubomolewa! Nikajiuliza swali: JE kiranja wetu huwa nawauliza wahusika kuhusu njia yoyote au uwezekano wowote wa kulinusuru lile banda au vile vibanda vya chipsi kule kabla ya kuvibomoa!?
Je hawa wataalamu wetu huwa wanatoa ushauri wa kitaalamu hata kama unamuumiza kiranja!? Au huwa nao wanapindisha taaluma ili kwenda sawa na kiranja!?
Alafu yule kiranja wetu anasema anapunguza matumizi lkn nikiangalia hili banda likibomolewa itakuwaje!? Je kuna banda lingine limeshajengwa kwa ajili ya kazi hii..!? Je limejengwa kwa pesa ngapi!? Ss kama tukifanya namna yoyote kuinusuru hiyo pesa si tungeweza kuitumia kupelekea watoto shule!?
Baadae nikaiona picha kutoka ukoo wa jirani..picha ikionesha wataalamu wa ujenzi wamejenga njia ya juu inayofanana na yetu lakini imepindishwa vizuri ili kulikwepa banda moja kuubwa la kuku wao.nikawapa heko wale waheshimiwa wa ukoo ule kwa kufanya maamuzi yasioumiza upande mwingine.
Nisiwe muongo kwakweli lile banda la kuku litaniuma kama likibomolewa,kiranja nakuomba usikie haya.
Ni hayo tu.