Hivi huu ndo utaratibu wa nchi ya Tanzania?

Masauni

JF-Expert Member
Aug 15, 2010
386
58
Nianze kwa kusema jamani tembea uone. Wiki iliyopita nilisafiri kwa gari yangu nikitokea south africa ili nije nyumbani tanzania kwa likizo ya mwezi mmoja. Nimepita vizuri katika nchi zote namaanisha south africa, zimbabwe na zambia
katika nchi zote hizo maafisa wa revenue walinipa ushirikiano mkubwa sana hawakuniomba hata senti moja. Matatizo yalianza pale nilipofika katika nchi yangu, nilikuwa na furaha sana kuiona tena nchi yangu baada ya muda mrefu.Lakini furaha yangu ilibadirika na kuwa majonzi makubwa pale watu wa TRA walipoanza kunisumbua, pamoja na kuwaonyesha documents zote bado walinisumbua mno. Jambo la ajabu ni kwamba katika nchi zote nilizopita utaratibu huko wazi kabisa ni tanzania tu ambayo utaratibu hauko wazi kila mtu anasema la kwake. Rushwa inatisha mno pale mpakani. NILIWAHI KUSEMA SIKU MOJA HUMU JAVINI ,KWAMBA TATIZO LA TANZANIA NI SYSTEM MBAYA CHINI YA UONGOZI WA CCM. HATA AKITOKEA MALAIKA KUTAWALA CHINI YA MFUMO WA CCM NOTHING WILL CHANGE
. NAKUBALIANA NA DR. SLAA ALIPOSEMA MFUMO WA UONGOZI TANZANIA UNABIDI UFUMULIWE NA KUSUKWA UPYA ,ALIKUWA SAHII 100%. UKIENDA KWENYE INTERNET UWEZI UKAPATA TAARIFA ZA TRA ZILIZO WAZI, HII INAASHIRIA KUWA WANAFANYA MAKUSUDI ILI KUPATA MIANYA YA RUSHWA. JAMANI HATA SASA ZAMBIA WANATUSHINDA!!!! NIMALIZIE KWA KUSEMA CHINI YA UONGOZI WA CCM NOTHING WILL CHANGE BELIEVE ME.



.
 
Back
Top Bottom