TANZANIAN NINJA
JF-Expert Member
- Apr 19, 2018
- 441
- 496
Sawa hapo nimeelewa lakini mbona ipo kwenye taasisi ya serikali pia nimewahi iona kwenye noti ya miatano.Ukisoma biblia kuna mahali waisraeli walimuasi Mungu wakashushiwa nyoka waliumwa wengi wakafa, ilibidi Musa apewe maagizo na Mungu atengeneze nyoka wa shaba ambaye alitakiwa amtundike kwenye mti. Walioumwa waliambiwa wamuangalie watapona na kweli walipona . Pia kifo cha Yesu msalabani ni kama nyoka wa shaba (waislamu na imani zingine hawakubaliani na hili). Kwa hiyo, hiyo alama inatumika dunia nzima katika kuonesha uponyaji wa afya za awatu upo kwenye logo nyingi za wanaohusika na huduma za afya kama WHO,MNH n.k.