Hivi hili linawezekana! (2 in 1)

DASA

JF-Expert Member
Jan 6, 2011
1,031
301
Kuna majamaa wawili ambao wanafahamiana kwa muda mrefu tangu wakiwa masomoni, kwa bahati nzuri au mbaya wamejikuta kila mmoja anatarajia kufunga ndoa kwasababu zisizozuilika mwezi wa kumi na moja mwishoni. Sasa kila mmoja ana tatizo la pesa, kwahiyo maandalizi kwao yanakuwa magumu ukizingatia na gharama za kufanya harusi hapa Dar. Sasa walipogundua kwamba matatizo yao yanafanana wameamua kufanya harusi kwa pamoja siku moja na kwamba watashare ukumbi na mambo mengine yote yatakayowezekana kushare. Sasa katika harakati za kupunguza gharama wanafikiria pia kila mmoja awe bestman wa mwenzie na wake zao watarajiwa kila mmoja awe matron wa mwenzie hiyo siku ya harusi.



Sasa jamani hivi hili kweli linawezekana!, kuna mtu ameshawahi shuhudia kitu kama hiki!, na kama inawezekana nashindwa kupata picha kanisani na ukumbini shughuli itakuwa inaendeshwa vipi!.
 
Inawezekana tu, kwa sababu maana ya ndoa sio sherehe, halafu mambo mengine ni mbwembwe tu,.
 
no, napinga kabisa. utakuwaje best man wakati hujaoa? ubahili mngine bwana...
 
Hao watu ni noma, si bora waende tu kanisani halafu warudi nyumbani na wake zao watulie, wakipata hela hata mwaka ujao wavae nguo zao za harusi, waende kanisani wakarudie nadhiri yao ya ndoa halafu wafanye sherehe.
 
inawezekana kwani arusi ni kanisani ukumbini ni sehemu ya kufurahi na kupongezana.
 
Sema ni wewe,ucwasingzie wa2 wengne mkuu,acha ubahili.
 
Sijui kwanini watu wanataka makubwa wakati hawayawezi.ebu mwambie huyu rafiki yako ajikune anapojifikia....
 
wazo zuri mkuu we fanya hiyo kitu inawezekana kabisa, harusi sio sherehe kuuubwa kihivyo
wengi wetu huwa tunapenda kujionyesha tunazo ndio maana tunafanya shere kuuubwa
 
inawezekana kwani arusi ni kanisani ukumbini ni sehemu ya kufurahi na kupongezana.

sasa suale ni hizo taratibu za ndoa zinaweza kufanyika hasa hapo kanisani katika hali hiyo. hapa ni kama unaelewa taratibu za ndoa kanisani.
 
Hao watu ni noma, si bora waende tu kanisani halafu warudi nyumbani na wake zao watulie, wakipata hela hata mwaka ujao wavae nguo zao za harusi, waende kanisani wakarudie nadhiri yao ya ndoa halafu wafanye sherehe.

tatizo mkuu masuala ya ukumbini sio tatizo, watu watachangia angalau hata kitu kidogo kwa ajili ya ukumbusho kinaweza kufanyika. swala hapa ni hizo taratibu za kanisani kama zinaruhusu hivyo.
 
Fungeni ndoa kanisani, baada ya hapo andaa sherehe ndogo hata ya nyumbani ambayo haina gharama ya ukumbi. Hapo nyumbani wapishi ni nduguzo mwenyewe nahisi itafana kuliko kwenda kwenye liukumbi likuuuubwa halafu huna uwezo nalo.
 
Kuna majamaa wawili ambao wanafahamiana kwa muda mrefu tangu wakiwa masomoni, kwa bahati nzuri au mbaya wamejikuta kila mmoja anatarajia kufunga ndoa kwasababu zisizozuilika mwezi wa kumi na moja mwishoni. Sasa kila mmoja ana tatizo la pesa, kwahiyo maandalizi kwao yanakuwa magumu ukizingatia na gharama za kufanya harusi hapa Dar. Sasa walipogundua kwamba matatizo yao yanafanana wameamua kufanya harusi kwa pamoja siku moja na kwamba watashare ukumbi na mambo mengine yote yatakayowezekana kushare. Sasa katika harakati za kupunguza gharama wanafikiria pia kila mmoja awe bestman wa mwenzie na wake zao watarajiwa kila mmoja awe matron wa mwenzie hiyo siku ya harusi.



Sasa jamani hivi hili kweli linawezekana!, kuna mtu ameshawahi shuhudia kitu kama hiki!, na kama inawezekana nashindwa kupata picha kanisani na ukumbini shughuli itakuwa inaendeshwa vipi!.

hahaa,hii ya kila mmoja awe mpambe wa mwenziwe sijawahi sikia,kushare ukumbi nimeona!kweli shida ni kipimo cha akili.....mimi sioni kama kuna shida yoyote ila nachoshindwa kushangaa kwa nini watake makubwa wakati uwezo hamna?wanawezafunga then wanarudi home,kanisani ndio kitu cha msingi haya mengine ya mtaani tu...mbwemwe tu
 
Kuna majamaa wawili ambao wanafahamiana kwa muda mrefu tangu wakiwa masomoni, kwa bahati nzuri au mbaya wamejikuta kila mmoja anatarajia kufunga ndoa kwasababu zisizozuilika mwezi wa kumi na moja mwishoni. Sasa kila mmoja ana tatizo la pesa, kwahiyo maandalizi kwao yanakuwa magumu ukizingatia na gharama za kufanya harusi hapa Dar. Sasa walipogundua kwamba matatizo yao yanafanana wameamua kufanya harusi kwa pamoja siku moja na kwamba watashare ukumbi na mambo mengine yote yatakayowezekana kushare. Sasa katika harakati za kupunguza gharama wanafikiria pia kila mmoja awe bestman wa mwenzie na wake zao watarajiwa kila mmoja awe matron wa mwenzie hiyo siku ya harusi.



Sasa jamani hivi hili kweli linawezekana!, kuna mtu ameshawahi shuhudia kitu kama hiki!, na kama inawezekana nashindwa kupata picha kanisani na ukumbini shughuli itakuwa inaendeshwa vipi!.

hahaa,hii ya kila mmoja awe mpambe wa mwenziwe sijawahi sikia,kushare ukumbi nimeona!kweli shida ni kipimo cha akili.....mimi sioni kama kuna shida yoyote ila nachoshindwa kushangaa kwa nini watake makubwa wakati uwezo hamna?wanawezafunga then wanarudi home,kanisani ndio kitu cha msingi haya mengine ya mtaani tu...mbwembwe tu
 
Sijawhi ckia kitu kama hiki, labda wakaulize kanisani wanakotaka kwenda kufungia hiyo ndoa yao wapewe utaratibu huo kama upo, nawashauri km ishu ni hela wafunge ndoa kama kawaida sherehe za ukumbini watafanya watakapopata hela wakati mwingine.
 
Kuna majamaa wawili ambao wanafahamiana kwa muda mrefu tangu wakiwa masomoni, kwa bahati nzuri au mbaya wamejikuta kila mmoja anatarajia kufunga ndoa kwasababu zisizozuilika mwezi wa kumi na moja mwishoni. Sasa kila mmoja ana tatizo la pesa, kwahiyo maandalizi kwao yanakuwa magumu ukizingatia na gharama za kufanya harusi hapa Dar. Sasa walipogundua kwamba matatizo yao yanafanana wameamua kufanya harusi kwa pamoja siku moja na kwamba watashare ukumbi na mambo mengine yote yatakayowezekana kushare. Sasa katika harakati za kupunguza gharama wanafikiria pia kila mmoja awe bestman wa mwenzie na wake zao watarajiwa kila mmoja awe matron wa mwenzie hiyo siku ya harusi.



Sasa jamani hivi hili kweli linawezekana!, kuna mtu ameshawahi shuhudia kitu kama hiki!, na kama inawezekana nashindwa kupata picha kanisani na ukumbini shughuli itakuwa inaendeshwa vipi!.

mi naona ni sawa tu,basicaly ndoa ni mkataba,best/matron ni mashahidi wa mkataba.
 
Kuna majamaa wawili ambao wanafahamiana kwa muda mrefu tangu wakiwa masomoni, kwa bahati nzuri au mbaya wamejikuta kila mmoja anatarajia kufunga ndoa kwasababu zisizozuilika mwezi wa kumi na moja mwishoni. Sasa kila mmoja ana tatizo la pesa, kwahiyo maandalizi kwao yanakuwa magumu ukizingatia na gharama za kufanya harusi hapa Dar. Sasa walipogundua kwamba matatizo yao yanafanana wameamua kufanya harusi kwa pamoja siku moja na kwamba watashare ukumbi na mambo mengine yote yatakayowezekana kushare. Sasa katika harakati za kupunguza gharama wanafikiria pia kila mmoja awe bestman wa mwenzie na wake zao watarajiwa kila mmoja awe matron wa mwenzie hiyo siku ya harusi.

Unajua Watanzania wengi tunapenda wenyewe ugumu wa maisha kwasababu zifuatazo;
1. Sio lazima kila sherehe ya harusi ikafanyike ukumbini sababu gharama zake ni kubwa mno hivyo ni lazima ujifunge kibwebwe, Gharama zenyewe zatokana na a) Gharama ya ukumbi wenyewe b) Gharama za Upambaji wa ukumbi c) Gharama za vyakula na vinywaji d) Gharama za usafiri.
Watu wengi tunapenda gharama ambazo hatuna uwezo nazo hivyo Fanya kitu kutokana na uwezo wako, hata hivyo kizuri gharama bwana
 
no, napinga kabisa. utakuwaje best man wakati hujaoa? ubahili mngine bwana...
alosema mpaka uoe nani,bestman/matron ni ma witness tu wa mkataba wa ndoa,all you need ni kuwa na umri wa kushuhudia mkataba na sio kuoa/kuolewa.
 
Back
Top Bottom