mm ya kwangu ilivunjika bila huruma baada ya mke kuanza kusali makanisa hayo anafululiza mwezi mzima eti yupo mkesha!Inanibidi niseme nisiposema basi hawa mabinti watazidi kujifaragua na kuhalibu sifa za wanawake wengine wenye maadili na hekima njema....
Ni hawa mabinti wa Kirokole...
Utasikia naenda kwenye mkesha,naenda kwa mwakasego,naenda kwa katunzi..naenda semina ya vijana,
Lakini sasa!!!!!!Daaaaah
Acha leo tuwachane live.....
NI nyie nyie.....
1.mnao ongoza kwenda makanisani na kwenye majukwaa ya semina za kikanisa WAKATI kwenye ndoa zenu hamjitolei sawasawa
2.Mnaongoza kujipendekeza kwa kuheshimu wachungaji na wazee wakanisa Wakati waume zenu hata tone la heshima hamna
3.mnaongoza kwa matendo mabaya kuliko hata wapagani wasiomjua mungu...ni waongo,wanafiki,wasengenyaji,wasiosamehe,wenye chuki mioyoni mwenu...
4.mwisho ni kuwa ndo nyie nyie mnaongoza kwa kuvunja ndoa kila siku..tena ndoa zenyewe zilighalamika kwa kila khari...daaaaah!!!Hivi hawa watu wana matatizo gani???
ngoja nisimalizie.....
Wadau malizieni.......
mkuu sio vizuri mwambie relato we need her word kwa nini uje mwenyewe lakini mkuu? hahahWachane tu...
Hapana mkuu...nimefululuzia kuona ndoa tano za wanawake wakirokole sasa zinavunjika na ukiangalia tatzzo ni hawa wachingaji wanaosimama makanisani nakuwafundisha wanawake mafundisho ya kishetani...Mkuu punguza jazba maana umetumia hasira kurusha ujumbe. Inaonesha wazi shemeji yetu ameokoka so kuna kitu amemisbehave ndo umekuja huku kuwahukumu usiowajua THATS NOT FAIR!
Hakuna mtu asiye na madhaifu na kama hujui kuokolewa kunaanza ndipo tabia za mtu huanza kubadilika taratibu kwa kadri anavyopata mafundisho ya Kristo yaliyo sahihi,narudia YALIYO SAHIHI. neno ndilo humbadilisha mtu ila wokovu hupewa bure kwa kumuamini Yesu na kazi yake ya msalaba.
Siwatetei wadada waliomwamini Kristo aka kuokolewa kwani acjilia mbali wokovu suala la amekuzwaje liko palepale. So utamkuta Dada aliyeokoka mwongeaji sana, mkimya sana mkali sana mwenye hasira sana,mwenye upendo sana mkarimu nk nk.
Ni kama kusema mafisadi walioko bongo haimaanishi watumishi wa umma wote mafisadi au labda zile kashfa za mapadre wa Katoliki kulawiti watoto huko USA je tuconclude hata wazee wetu hawa wa hapa Tz wanafanya hivyo?? Hapana.
La msingi anayekosea na kufanya unafiki aambiwe yeye i asaidike kuliko kutomwambia ukaja kurusha huku.
Mwisho nakupa pole ya dhati maana hapana shaka kuna mtu amekukwaza bro
Post sent using JamiiForums mobile app
Pole sana mkuu...mungu yuko pamoja nawe...mm ya kwangu ilivunjika bila huruma baada ya mke kuanza kusali makanisa hayo anafululiza mwezi mzima eti yupo mkesha!
Post sent using JamiiForums mobile app
Point sana mkuu...nilikuwa nikiona wanashambuliwa nikawa nahamaki saa nyingine napatwa na hasira kusikia wanasemwa vibaya kwani hata mimi ni mpendwa ila nimekuja kugundua kwa wale ninaowajua kuna kaujinga fulani wanao vichwani. Mimi nasema wasemwe tuu hizi tabia ni kweli zipo unakuta wanaolewa na makanisa na kazi za makanisa pamoja na huduma mbalimbali za makanisa badala ya waume wao. Ndoa ya Benny Hinn ilivunjika kwa sababu ya yeye kutokuwa na time na mkewe akaja kukiri mwenyewe 'I WAS MARRIED BY MINISTRY AND I FORGET THAT I HAD MARRIED A WIFE' kabla ya maombi ya wapendwa kuiombea ndoa yake kurudiana, mwangalie na Pastor Chriss Oyakhilome ndoa ilivunjika kifupi hawa dada zetu tabia ni kama hizihizi sasa lazima wafahamu ya kwamba kwa jinsi Mungu anavyotupenda hawezi kusimamia ndoa yenu ivunjike kwa sababu ya ujinga wako kujifanya upo bize sana na kanisa unaacha kuwahudumia watoto, na mumeo kumbuka Mungu ndie aliekupa huyo mume na atakuonesha namna ya kuishi nae usifate mapokeo ya madhehebu yenu. halafu saa nyingine unakuta dhehebu linaongozwa na mchungaji ambaye Un-educated and not civilized anakulazimisha kufanya mambo ya ajabu yanyohatarisha ndoa still unafuata tuu bila kujudge hii ni hatari ndio maana madhehebu mengine Mchungaji lazima awe ana kiwango fulani cha elimu japo sii lazima ila hii huwa inasaidia sana kupunguza ujinga ujinga unaofanyika makanisani saa nyikngine huwa nikiona napatwa na hasira sana wanavyofanya mambo ya ajabu na kufanya jina la Mungu linatukanwa kumbe ni kwa sababu ya ujinga ujinga tuu. hatusemi usifunge kuomba, hatusemi usiende kwenye semina hatusemi usimfate mchungaji unaempenda ila iwe kwa kiasi na ubalance kati ya kanisa na familia ili haya mambo yweze kwenda kwa amani bila ugomvi. Leo hii kila mtu hamtaki mwanamke mlokole kwa sababu hizi wakati nyie ndio mliokuwa wife material. Badilikeni sio wote ila haya yanayosemwa yapo kabisa. Mkipata wanayofanya wanaume walokole yasiyokuwa ya maana nayo yaleteni hapa wabadilike mambo mengine hayahitaji Biblia hata sisi tupo humo ndani na tunaona kabisa hii amefanya ni kwa sababu ya ujinga, hii yuko sawa wala hakuna shida ila wale dada zetu nasema kwa sauti kuu badilikeni.
Soma vzr ujumbe wangu bro nimesisitiza mafundisho sahihi. Unajua dunia ya leo kwenye imani kuna mafundisho fake kibao si ktk ukristo au uislam.Hapana mkuu...nimefululuzia kuona ndoa tano za wanawake wakirokole sasa zinavunjika na ukiangalia tatzzo ni hawa wachingaji wanaosimama makanisani nakuwafundisha wanawake mafundisho ya kishetani...
hapana mkuu habari ya kuwa mpagani hapana Mungu ni mzuri kuliko unavyoweza kufikiri ila namna watu wanavyojiita wenyewe na kufanya matakwa ya wanadamu na sii ya Mungu. unaweza kukumbuka Yesu alikuwa anawaambia mnafanya matakwa ya wanadamu hamfanyi yangu. Mungu anatupenda sana kabla ya kufanya ukimuuliza atakuonesha namna ya kuishi na mkeo hata na mmeo pia. Shida inakuja pale unapopokea pokeo la mtu au la dhehebu. Roho Mtakatifu ni rafiki mzuri mno unaeweza kuwa nae shida tuu ni yale mapokeo ya watu na sii ya Mungu. Mungu yupo mkuu na anaishi mwamini upagani hapana maana when we depart from here there is another world and also there is a promise to live here after. Cha msingi tusome neno na tunsikilize zaidi Mungu anasemaje kuhusu ndoa zetu tuachane na mapokeoPoint sana mkuu...
Wachungaji ufinyu wa akili na mapokeo ya kidini yawafanya wanakengeusha ndoa za watu...mchungaji akifikia hana neno wala hawezi kukemea wanafunzi wake hilo ni bogazi la.mchungaji...ni bora kuwa mpagani tu...
Hiz dini zingine ni matatizo matupu
Sidhani kama kuna kanisa wanalokesha kila Siku. Kingine, uliongea nae? Na kama ndio alisemaje? Kwanini msingekwenda kumuona huyo mchungaji, mkamueleza?mm ya kwangu ilivunjika bila huruma baada ya mke kuanza kusali makanisa hayo anafululiza mwezi mzima eti yupo mkesha!
Post sent using JamiiForums mobile app