Hivi hawa wanaomsifia Magufuli huwa wanalala kweli?

Wengine hawalipwi hizo buku 7! Majority wapo wapo tu hawana cha kufanya!..ndo maana mtu anaanza kujiita Pombe...n the like
Kama ni kweli kuna namna serikali inatakiwa iangalie hili suala kiumakini itakuja kuigharimu taifa huko mbeleni, uwezo wa vijana kufikiria na kujenga hoja hauko sawa kabisa na taifa haliwezi kuendelea likiwa na watu wa namna hii
 
Kama heading inavyojieleza, hivi hawa wanaomsifia magufuli huwa wanalala saa ngapi?

Kwa kipindi hiki ambacho huku niliko jiji ninaloishi liko chini ya zuio la kutoka nje ya nyumba, mitandao imekuwa sehemu yangu kubwa ya kutembelea mda wote kwa vile sina ratiba nyingine tofauti, kwa huko nyumbani Tz nimeshangazwa na vitu kadhaa kwenye mitandao.

Kuna baadhi ya account huko facebook, tweeter, Insta, JamiiForums na site zingine Kuna majina na ID kazi yao ni kumsifu magufuli tu haijalishi ni kuhusu nini tena bila hoja za msingi hawa watu hawako kwa ajili ya chama Wala serikali wao ni magufuli tu.

Cha kushangaza zaidi wako active mda wote yaani 24/7hrs na karibu kila taarifa au thread wao ndio wa kwanza kucomment, kipindi mimi nakuwa nimechoka na upweke wa kujifungia ndani kila nikiingia online naziona hizohizo ID kwenye kila post iwe mchana, adhuhuri, alasiri,usiku wa manane hata asubuhi. Hawa watu wanafanya majukumu yao saa ngapi na wanalala mda gani? na ni Kama wanaambiana yaani wanashambulia kwa pamoja, au ni mtu mmoja anamiliki ID zaidi ya 10? Ina maana hawa jamaa hawalali?

Mimi ninashangaa kwa sababu sijawahi kufikiria Kuna watu wa namna hii yaani uwe online 24hrs kila siku kwa ajili ya mtu tena kwa kuandika matusi kwa kila post? Labda Kama Kuna malipo wanapata, Anyway nimeshangaa tu wakuu

Mimi bado naendelea na Lock-down

Chukua tahadhari, Corona Ipo na ni hatari.
Akina Bia yetu wengi wametoka chattle kweli ipo kazi awamu hii haijiamini hata kidogo.
 
Kama ni kweli kuna namna serikali inatakiwa iangalie hili suala kiumakini itakuja kuigharimu taifa huko mbeleni, uwezo wa vijana kufikiria na kujenga hoja hauko sawa kabisa na taifa haliwezi kuendelea likiwa na watu wa namna hii
Mkuu Lengo kwanza la ccm,ni kuwa madarakani,hiyo ya maendeleo ni by the way.so taifa kuwa na vijana wa hovyo namna hiyo kwao si issue as long as wanaweza kumharibu discussion za watu mitandaoni is oksy
 
Misasa
Bia yetu
Yehodaya
Bukikilo
Elitwege et al
Wanalipwa 7000 kwa siku kwa mwezi 210,000/- na hapo hapo wapange nyumba,walipada,wahonge,wavae,wale nk ndiyo maana hawalali wakiachishwa kazi watakula wapi?

Yehodaya mumewe ni mtendaji wa kijiji..ndo maana anashombo kama zote...yule mie nampendea sehen moja tu...ana uelewa wa mambo ila ni wa hovyo sana coz yuko ccm
 
Back
Top Bottom