Mwamba Usemao Kweli
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 744
- 186
Inasikitisha sana kuona ndani ya jf hakuna watanzania makini wa kujadiliwa katika tasnia ya uongozi wa juu wa nchi yetu kwa mustakabali wa taifa letu.
Bali tumekuwa tukiletewa baadhi ya wana ccm waliojidhihirisha kwa matendo, tabia na hulka zao kuwa ni mafisadi na wezi wa rasilimali za taifa letu kuwa wanafaa kwa nafasi ya urais mwaka 2015. Si hivyo tu bali kwa njia moja au nyengine watu hawa tunaoletewa hapa janvini wamechangia kudhoofisha kwa makusudi juhudi za watanzania waliowengi kujikwamua kutoka katika lindi la umaskini kwa maslahi binafsi.
Kumbukeni kashfa zifuatazo ambazo leo wahusika wanajitanabahisha ndani ya CCM kuwa iko tayari kuwapa uraisi: -
1. EPA.
2. Meremeta.
3. Mwananchi gold.
4. Ununuzi wa rada kwa bei mara 3 ya bei halisi.
5. Ununuzi wa ndege ya raisi kwa bei mara 3 ya bei halisi.
6. Deep green.
7. Ujensi wa benki kuu kwa garama kubwa zaidi duniani kuliko benki kuu yoyote.
8. Kubinafsisha na kuuza viwanda na makampuni ya umma kwa bei ya kutupa.
9. Richmond & Dowans.
10. Umiliki wa migodi ya madini na mikataba ya hovyo isiyoleta tija kiuchumi TZ.
11. Umiliki mbovu wa viwanja vya michezo na sehemu za wazi na kupelekea ujenzi holela mijini na ukosefu wa mipango miji bora.
12. Uuzwaji wa nyumba za umma kwa manufaa ya wachache
13. Kupandisha bei za umeme na uunganishaji wake kiholela kwa manufaa ya wachache
14. Kupandisha garama za ujenzi wa minudombinu ya barabara kwa asilimia 300 kwa manufaa ya wachache.
15. Kubinafsisha reli kwa kampuni ya India (RITES) ilioshindwa kutoa huduma bora.
16. ATC kuuzwa na kuididimiza kiuchumi na ki-huduma
17. Kushindwa kukusanya kodi toka kwa wawekezaji kuboresha maisha ya watanzania.
Kashafa hizi zimechangia sana kuzorotesha uchumi wa taifa letu na kupelekea kukuza umaskini kwa fedha zake kupotea bila kuchangia upatikanaji wa huduma bora za kijamii kwa watanzania.
Nawasihi sana wana jf tujitahidi sana katika dhama hizi ambapo taifa letu limekumbwa na wimbi la wana siasa tumbo kuepuka kuendelea kuwakandamiza watanzania wenzetu kwa kutumia mitandao kama JF kuwalisha uongo na uzandiki wa kuwapigia debe na kuwauza kwa sifa za kupika kwa namna yeyote ile wanasiasa walioshindwa na ambao kwao wamebaki kutumia fedha kujitangaza na kufanya kampeni makanisani na kwenye harambee za kuchangia maendeleo ya taifa letu kuwa wao ndio wanaokubalika na wanafaa kutuongoza.
Ni vema mkafahamu kuwa ni sisi wachache ndani ya taifa letu kwa uewelewa wetu ndo tunaweza kulikomboa taifa letu kutoka katika mikono ya walafi wachache waliozorotesha kwa makusudi huduma za umma katika kupata: -
1. Maji safi si mijini tu hadi vijijini.
2. Elimu bora na bure bila kulipia kote nchini.
3. Afya na matibabu bora bila kulipia.
4. Ajira kwa vijana wetu.
5. Pembejeo kwa wakati bila kutumia gharama kubwa.
6. Ununuzi wa mazao kwa wakati na kwa bei bora kutoka kwa mkulima bila kumdhulumu.
7. Haki mahakamani, polisi na sehemu nyenginezo za umma.
8. Haki katika matumizi ya ardhi vijijini na maeneo yenye rasilimali za madini.
Ni vema tuwakatae watu hawa ambao wamekuwa chimbuko la kuangamiza utaifa wetu na rasilimali za taifa letu. Tuwakatae kwa sauti moja kuwa hawatufai na tuwaogope kama ukoma.
Nawaombeni sana wanaJF mtuletee watanzania wengine tuwajadili wenye mvuto na walio tayari kuwatumikia watanzania wasio na kashfa za ufisadi wenye uadilifu na walio tayari bila kuchoka kuwaondolea watanzania umaskini uliopindukia huko mijini na vijijini.
Nawasilisha kwenu JF kwa manufaa ya taifa letu. Tujaribu kujadili majina kama hapa chini: -
1. Dr. Mwakyembe
2. Dr. Magufuli
3. Balozi Kagasheki
4. Prof. Muhongo
5. Nahodha
Na si kutuletea majina ya watu kama vile: -
1. Lowasa
2. Chenge
3. Ngeleja
Hawa walishashindwa katika nafasi za utendaji za uwaziri na uwaziri mkuu bado mnataka eti wawe rais na mnakaa kabisa na kujadili hapa jukwaani huku mate yakiwatoka kuwa eti washikiki ndani ya CCM. Eti hawana upinzani.
ACHENI HIZO.
Bali tumekuwa tukiletewa baadhi ya wana ccm waliojidhihirisha kwa matendo, tabia na hulka zao kuwa ni mafisadi na wezi wa rasilimali za taifa letu kuwa wanafaa kwa nafasi ya urais mwaka 2015. Si hivyo tu bali kwa njia moja au nyengine watu hawa tunaoletewa hapa janvini wamechangia kudhoofisha kwa makusudi juhudi za watanzania waliowengi kujikwamua kutoka katika lindi la umaskini kwa maslahi binafsi.
Kumbukeni kashfa zifuatazo ambazo leo wahusika wanajitanabahisha ndani ya CCM kuwa iko tayari kuwapa uraisi: -
1. EPA.
2. Meremeta.
3. Mwananchi gold.
4. Ununuzi wa rada kwa bei mara 3 ya bei halisi.
5. Ununuzi wa ndege ya raisi kwa bei mara 3 ya bei halisi.
6. Deep green.
7. Ujensi wa benki kuu kwa garama kubwa zaidi duniani kuliko benki kuu yoyote.
8. Kubinafsisha na kuuza viwanda na makampuni ya umma kwa bei ya kutupa.
9. Richmond & Dowans.
10. Umiliki wa migodi ya madini na mikataba ya hovyo isiyoleta tija kiuchumi TZ.
11. Umiliki mbovu wa viwanja vya michezo na sehemu za wazi na kupelekea ujenzi holela mijini na ukosefu wa mipango miji bora.
12. Uuzwaji wa nyumba za umma kwa manufaa ya wachache
13. Kupandisha bei za umeme na uunganishaji wake kiholela kwa manufaa ya wachache
14. Kupandisha garama za ujenzi wa minudombinu ya barabara kwa asilimia 300 kwa manufaa ya wachache.
15. Kubinafsisha reli kwa kampuni ya India (RITES) ilioshindwa kutoa huduma bora.
16. ATC kuuzwa na kuididimiza kiuchumi na ki-huduma
17. Kushindwa kukusanya kodi toka kwa wawekezaji kuboresha maisha ya watanzania.
Kashafa hizi zimechangia sana kuzorotesha uchumi wa taifa letu na kupelekea kukuza umaskini kwa fedha zake kupotea bila kuchangia upatikanaji wa huduma bora za kijamii kwa watanzania.
Nawasihi sana wana jf tujitahidi sana katika dhama hizi ambapo taifa letu limekumbwa na wimbi la wana siasa tumbo kuepuka kuendelea kuwakandamiza watanzania wenzetu kwa kutumia mitandao kama JF kuwalisha uongo na uzandiki wa kuwapigia debe na kuwauza kwa sifa za kupika kwa namna yeyote ile wanasiasa walioshindwa na ambao kwao wamebaki kutumia fedha kujitangaza na kufanya kampeni makanisani na kwenye harambee za kuchangia maendeleo ya taifa letu kuwa wao ndio wanaokubalika na wanafaa kutuongoza.
Ni vema mkafahamu kuwa ni sisi wachache ndani ya taifa letu kwa uewelewa wetu ndo tunaweza kulikomboa taifa letu kutoka katika mikono ya walafi wachache waliozorotesha kwa makusudi huduma za umma katika kupata: -
1. Maji safi si mijini tu hadi vijijini.
2. Elimu bora na bure bila kulipia kote nchini.
3. Afya na matibabu bora bila kulipia.
4. Ajira kwa vijana wetu.
5. Pembejeo kwa wakati bila kutumia gharama kubwa.
6. Ununuzi wa mazao kwa wakati na kwa bei bora kutoka kwa mkulima bila kumdhulumu.
7. Haki mahakamani, polisi na sehemu nyenginezo za umma.
8. Haki katika matumizi ya ardhi vijijini na maeneo yenye rasilimali za madini.
Ni vema tuwakatae watu hawa ambao wamekuwa chimbuko la kuangamiza utaifa wetu na rasilimali za taifa letu. Tuwakatae kwa sauti moja kuwa hawatufai na tuwaogope kama ukoma.
Nawaombeni sana wanaJF mtuletee watanzania wengine tuwajadili wenye mvuto na walio tayari kuwatumikia watanzania wasio na kashfa za ufisadi wenye uadilifu na walio tayari bila kuchoka kuwaondolea watanzania umaskini uliopindukia huko mijini na vijijini.
Nawasilisha kwenu JF kwa manufaa ya taifa letu. Tujaribu kujadili majina kama hapa chini: -
1. Dr. Mwakyembe
2. Dr. Magufuli
3. Balozi Kagasheki
4. Prof. Muhongo
5. Nahodha
Na si kutuletea majina ya watu kama vile: -
1. Lowasa
2. Chenge
3. Ngeleja
Hawa walishashindwa katika nafasi za utendaji za uwaziri na uwaziri mkuu bado mnataka eti wawe rais na mnakaa kabisa na kujadili hapa jukwaani huku mate yakiwatoka kuwa eti washikiki ndani ya CCM. Eti hawana upinzani.
ACHENI HIZO.