Akhi
JF-Expert Member
- Jul 12, 2021
- 2,835
- 4,607
Acha kunywa Pombe huo ndo ushauri wangu mna mnywaji pombe humfanya awe na kitambiWataalam
Nimekuwa nikijiuliza hivi imeshindikana kweli kufanya surgery ya kuondoa mafuta toka kwenye tumbo? mi naona jinsi yalivyojirundika sehemu moja tumboni kama mnavyotuaminisha kupitia michoro yenu nk ni kazi rahisi zaidi kama imewezekana kuzalisha mwanamke kwa kisu? badala ya sijui kukata utumbo nk???au kuna kitu sijui hapa wataalam?
Nimehangaika sana kupunguza kitambi changu lakini sasa nimekata tamaa baada ya kubugia madawa mbalimbali ya kienyeji,herbal,food suplements , diet,kuacha kula wanga,mafuta ,sukari na nyama nyekundu......Yote haya nimefanya lakini wapi......yaani kuna madawa nikinywa naharisha mafuta mpaka nasikia kizunguzungu...lakini kitambi kinabaki pale pale hata sijui yale mafuta huwa yanapungua kutokeaga wapi.....hii ni pamoja na kufanya mazoezi mepesi.......nilichoshindwa kuacha ni pombe kali - Vodka.....lakini nimejitahidi sana kuacha mavyakula ya ajabu ajabu hasa usiku...lakini wapi.......??...Ttizo kila mtaalam wa mitishamba anakwambia dawa yake ni kiboko lakini wapi! ...nina mwaka wa tano sasa nahangaika na hili tumbo linanyima sana raha wakuu.....
Napokea ushauri wa kitaalam wa aina zote
Asanteni