Hivi gharama ya lodge/guest kuwa kubwa au ndogo inatokana Status/quality ya lodge au sehemu?

Clark boots

JF-Expert Member
Jun 5, 2017
6,384
5,509
Siku chache zilizopita nilikuwa mji fulani hapa Tanzania, hivyo kutokana na mihangaiko yangu kuwa mirefu kidgo nikaamua kuchukuwa room guest nikae siku mbili tatu huku nikimilisha Michakato yangu..

So, actually sipendagi makuu katika maisha yangu ndipo nilipoamua kutafuta guest ya kawaida sana ki-appearance na niliamini itakuwa affordable ukilinganisha na maguest/mahotel makubwa yenye uwekezaji mkubwa.

Ile guest obvious ipo center yaan mjini kabisa ila a according to appearance ni ya kawaida sana na it seem ni ya kitambo kidogo..

Ila kitu kilichonistaajabisha ni Price of room.. Yaan ni more expensive ukicompare na status ya Guest husika..

Hivyo nataka kufahamu, bei ya guest kuwa ndogo au kubwa inatokana na Status au place la jengo husika..?
 
Dah maswali mengine magumu utadhani tunafanya pepa ya PhD ya kemia ya ubanguaji korosho.

Ngoja nikuitie jiwe Chakubanga aje atusolvie hii equation
 
Bei inakua juu au chini kwa factor zifuatazo, kwanza location, hapo tayari ushasema ipo centre kitendo tu cha kuwepo mjini bila kujali uzuri wa jengo au mazingira yake kinaongeza gharama, pili ushindani unaweza kukuta ilipokuwepo hio ushindani si mkubwa, yaani gesti sio nyingi hivo wanajua tu ni lazima utalipia, sababu nyingine na muda ulioenda mfano ukienda muda mmbaya labda usiku, lazima wakukamue bei sababu wanajua hautaweza kuhangaika kutafuta zingine since bado utakua n mgeni wa eneo husika, sababu nyingine pia n gharama za uendeshaji zinaweza kua zipo juu ndio maana wao wanaweka cost zao juu ili kupunguza gape, na sababu ya mwisho ni tamaa yani wanataka faida za haraka ndio maana bei zao zinakua ghali kuliko huduma wanazotoa.
.
Majibu haya n kutokana na uzoefu ninaopata katika safari zangu, na ambazo nilikwishazifanya tayari.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom