Hivi Gesi yetu imeishia wapi?

Wakuu, nilikua nataka kujua hivi hii gesi yetu na mambo ya uchumi wa gesi yameishia wapi?, naona Wakuu wa awamo ya tano hawaongelei kabisa gesi na ukiangalia harakati iliyopo ya kimakakati ya kiuchumi inaashiria hamna gesi katika mikakati hiyo..

Tunajua gesi ingesaidia Sana katika ujenzi wa miundombinu yetu kwa kasi na kuunganisha nchi yetu na kufanya shughuli za uzalishaji kua nafuu na fanisi zaidi huku mitaji ya ndani na nje ikizunguka kwa urahisi zaidi, na mengineo mengi kama uboreshaji elimu na mishahara ya walimu Wetu, vyombo vya usalama, na kuwekeza katika makazi mijini na kuwekeza nje kiasi kingine ill kuepukana na mzunguko mkubwa wa fedha kuliko uzalishaji wa ndani. Haya yalikua matumaini sasa ukweli iko wapi?

ingependa kupata taarifa yeyote ya jambo hili kwa wale wanaojua au wafuatiliaji wa hili jambo pamoja na kuwatarifu wengine wenye kutaka ufahamu kama Mimi. Tujuzane kwa upeo na uelewo mzuri.
Asante.
u mean gesi ya wachina?
 
Bibi aliizuia kwa kufunga koki n bahati mbaya yule bibi alifariki ss mtu mwengine hakuna wakufungilia gesi kufika dar,
 
Mkuu huu uchumi wa gesi asilia upo complex kidogo, kwakuwa sehemu kubwa ya utafutaji na uzalishaji tunategemea kampuni za kigeni ambazo nazo zinataratibu zake hasa katika kuamua nilini waanze uzarishaji, hii kitu huenda inafanya hata viongozi wetu washidwe kuweka bayana nilini tutaanza kunufaika na hii resource ingawa lazima tukiri kwa kiasi fulani tumeanza kunufaika na rasilimali hii kwani kiasi kikubwa cha umeme kinazalishwa na gesi

Serikali iiwezeshe TPDC iweze kusambaza mabomba ya gesi katika nyumba za watu kwa kuanza na mikoa iliyojirani na rasilimali hii, angalau watu waone moja kwa moja manufaa ya hii raslimali.

Mkuu mi naona serikali ianze kupitisha mabomba ya maji ktk nyumba za watu halafi gesi ifuate
 
Hiyo ilikuwa kampeni tu mkuu,hiv sasa tunajenga viwanda,huku vingine vikisimamisha uzalishaji,Pr.Sospeter Muhongo hata hafany makongamano pale udsm
 
Back
Top Bottom