Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,216
- 113,510
Mara baada ya Rais Samia kuchukua madaraka, gazeti la serikali, Daily News, lilichapisha tangazo kutoka STAMICO, la kumpongeza Rais huyo mpya.
Zaidi ya kumpongeza, tangazo hilo hilo pia lilitoa masikitiko ya kufiwa/ kufa kwa Rais Samia Suluhu Hasan!
Lilikuwa tangazo la hovyo kweli. Sijui hata lilipitaje kwenye mchujo wa uhariri.
Daily News lilifungiwa?
Leo serikali imelifungia gazeti la Uhuru kwa kile kinachodaiwa ni kumzulia Rais maneno ambayo hakusema katika mahojiano yake na Salim Kikeke wa BBC!
Maajabu ya mwaka haya!
Kwa nini ninajiwa na hisia za kutilia shaka ufungiwaji huo wa gazeti la Uhuru?
Kati ya kuzuliwa maneno ambayo mtu hajasema na kuzuliwa kifo, kipi kilicho kibaya kukizidi chenzake?
Isije kuwa CCM wanatuchezea akili. Isije kuwa wametengeneza tukio la kujichukulia hatua ili huko mbeleni tukio hilo lije kutumika kama rejea ya kuhalalisha kuwabana mbavu wale wote wanaoonekana kuleta chokochoko.
Twaweza kuambiwa ‘serikali ya CCM haina upendeleo. Hata vyombo vyake vya habari huwa inavifungia’.
Kuna kitu ndani kabisa ya mifupa yangu kinachonambia ‘Ngabu, stuka! Maigizo tu hayo ya kutengeneza mazingira ya kuja kuhalalishia yajayo huko mbeleni’.
Tujiulize: Hivi kwa mfano hilo gazeti la Uhuru lingemzushia mmoja wa viongozi wa upinzani, tuseme lingemzushia Tundu Lissu kifo [kama yeye alivyomzushia yule mlinzi wa Magufuli], serikali ingelifungia kweli? CCM nao wangesitisha uchapaji wake kweli?
Sidhani!!!!
Zaidi ya kumpongeza, tangazo hilo hilo pia lilitoa masikitiko ya kufiwa/ kufa kwa Rais Samia Suluhu Hasan!
Lilikuwa tangazo la hovyo kweli. Sijui hata lilipitaje kwenye mchujo wa uhariri.
Daily News lilifungiwa?
Leo serikali imelifungia gazeti la Uhuru kwa kile kinachodaiwa ni kumzulia Rais maneno ambayo hakusema katika mahojiano yake na Salim Kikeke wa BBC!
Maajabu ya mwaka haya!
Kwa nini ninajiwa na hisia za kutilia shaka ufungiwaji huo wa gazeti la Uhuru?
Kati ya kuzuliwa maneno ambayo mtu hajasema na kuzuliwa kifo, kipi kilicho kibaya kukizidi chenzake?
Isije kuwa CCM wanatuchezea akili. Isije kuwa wametengeneza tukio la kujichukulia hatua ili huko mbeleni tukio hilo lije kutumika kama rejea ya kuhalalisha kuwabana mbavu wale wote wanaoonekana kuleta chokochoko.
Twaweza kuambiwa ‘serikali ya CCM haina upendeleo. Hata vyombo vyake vya habari huwa inavifungia’.
Kuna kitu ndani kabisa ya mifupa yangu kinachonambia ‘Ngabu, stuka! Maigizo tu hayo ya kutengeneza mazingira ya kuja kuhalalishia yajayo huko mbeleni’.
Tujiulize: Hivi kwa mfano hilo gazeti la Uhuru lingemzushia mmoja wa viongozi wa upinzani, tuseme lingemzushia Tundu Lissu kifo [kama yeye alivyomzushia yule mlinzi wa Magufuli], serikali ingelifungia kweli? CCM nao wangesitisha uchapaji wake kweli?
Sidhani!!!!