Hivi gari moja la waziri lingegharamia elimu ya wanafunzi wangapi wa vyuo vya elimu ya juu?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371
Nimesikitishwa sana na taarifa za zaidi ya wanafunzi 4000 kukosa mikopo kwa ajili ya kugharamia elimu yao ya juu.Nii wazi kuwa watoto wa maskini wa nchii hii(umasikini ambao msingi wake ni ufisadi) watashindwa kwenda vyuoni na wachache tu ndio watamudu kujigharamia.

Hivi nini kiwe kipaumbele kati ya elimu na mambo haya linapokuja swala la bajeti
1.Safari za raisi
2.Magari ya kifahari
3.Posho kubwa kupindukia ktk vikao vya bodi mbali mbali,kamati za bunge na sitting allowance nyinginezo
4.Safari za mara kwa mara za watendaji wakuu serikalini
5.Bajeti kubwa za chai na vitafunwa serikalini mfano ikulu.
6.Na anasa nyingine nyingi tu zinazotengewa mabilioni serikalini

Hii serikali yetu isiyo na vipaumbele ni cancer inayotafuna maskini wengi wa nchii hii.

Tunahitaji kujikomboa.
 
Mwaka jana tuligoma UDSM kuwatetea watoto wa maskini waliokosa mkopo, tulipofukuzwa hakuna hata mzaz mmoja wa watoto wa maskn aliyeilaani serikali kwa kutufukuza tukiwa tunawapigania watoto wao. Mwaka huu tena imejirudia. Mimi nasema acheni wakose elimu kwa sababu ya mkopo maana maskini wa nchi hii wanaudhi sana. Hawako tayari kupingana na serikali ya Dhaifu
 
India leo wameandamana kupinga supermarkets kufunguliwa India kwa.sababu other retail shops zingefungwa na hii ingesababisha umasikini kuendelea. Wamekusanyika oppositin part na wafanyakazi,wananchi,railway,schools,banks zilifungwa its all about coorperation tukishikamana twaweza pata all we need kwa sababu hela ipo
 
Back
Top Bottom