Hivi elimu ina nafasi gani katika kuoa na kuolewa?

Haina nafasi yoyote, kinachotakiwa ni mapenzi ya kweli. Ila asilimia kubwa ya dada zetu waliyo na elimu dharau nyingi kwa wanaume hususa muwe na kiwango sawa cha elimu au kidume uzidiwe. ukichunguza kwa umakini ndiyo utagundua wasomi wengi wanawake wanapewa swimbili tu kisha kule au alee mwanawe bila ya kuwa kwenye ndoa.
 
Elimu ina nafasi gani katika kuoa na kuolewa?

Haina nafasi kabisa. Elimu, pesana n.k ni mbwembwe zetu tu binadamu na si zaidi ya hapo!
Kama ingekuwa na nafasi, jiulize watu ambao hawakubahatika kwenda shule igekuwaje?!
 
ikitumika vizuri inasaidia kuimarisha familia bahati mbaya siku hizi ndo inaongeza jeuri,viburi,dharau, maneno,kujiamini kusikokuwa na maana idadi ya wanaume so negative effects zimekuwa nyingi japo ukiwa nje unaweza ona inasaidia kuongeza income kwa familia
 
Elimu ina nafasi kubwa sana katika kuolewa na nafasi yenyewe ni kwamba ukitaka usiolewe wewe na upigishwe mimba tu watu wakukimbie au wakuibie halafu wakukimbie basi kuwa umesoma sana.Ndio maana ukienda kwenye vyuo vyote malecturer wa kike wengi wao hawajaolewa ila wana watoto jamaa wamepiga kiboga wakachukua mshiko wakakimbia kuchua dogodogo zisizosoma huo ndio ukweli wenyewe.
 
elimu kwa bongo na Africa ni tatizo kwa wanawake lakini kwa nchi za wenzetu sio tatizo ni sehemu ya maisha tu
 
baadhi ya wanaume wanaogopa wanawake waliosoma, wanaogopa kuwa challenged, kushirikiana kiuchumi ili kuvuka, wanaogopa wanawake wenye kipato, wanahisi watashindwa kuwacontrol(maana kuna wanaopenda kuombwa hela ya cream, hela ya lotion hela ya pichu)

zaidi ya kufuta ujinga na kuwapa ustaarabu, elimu haina nafasi kubwa saaaana kwenye ndoa, mapenzi ya dhati ndo yana nafasi kubwa na madhubuti, kisha mpunga
 
Wanawake waliosoma hawaolewi sio bongo tu hata huko india pakistan,bangladesh urabuni nk
mwanamke akisoma anataka kuwa sawa na mwanaume sasa wanaume wa2 hawawezi kuongoza
nyumba moja.
 
Elimu ina nafasi kubwa sana katika kuolewa na nafasi yenyewe ni kwamba ukitaka usiolewe wewe na upigishwe mimba tu watu wakukimbie au wakuibie halafu wakukimbie basi kuwa umesoma sana.Ndio maana ukienda kwenye vyuo vyote malecturer wa kike wengi wao hawajaolewa ila wana watoto jamaa wamepiga kiboga wakachukua mshiko wakakimbia kuchua dogodogo zisizosoma huo ndio ukweli wenyewe.
Tatizo sio elimu wala wanawake wasomi, tatizo ni wanaume waliosoma bado hawajaelimika. Wanaume wasomi wanataka wanawake wasiosoma kwa kuwa wanakubali kukanadimizwa. Wanaume hawataki mawazo mbadala toka kwa wake zao. Wanataka wafanye watakavyo bila kuhojiwa na mke wake. Mke aliyeelimika ni lazima atataka ufafanuzi kwa kila jambo linalofanyika ndani ya familia. Iwapo majibu hayataridhisha hata kubali, hapo ndiyo mwanzo wa migogoro.
Elimu humfanya mwenye kuelimika kujiamini zaidi katika maisha, pia kipato pia mfanya mtu kuwa huru na kujiamini. Wanaume wanataka mtu anayemtegemea kwa pesa na amwawazo ili waendeleze mfumo dume. Wanaume wengi ni madikiteta. Wakiweza wanataka wadikteti hata watoto wazaliwe wangapi na kwa nafasi gani.
Kama mambo kama haya hawawezi kuyapata kwa wasomi, basi wakoradhi kuoa hata asiyesoma kabisa. Ukiangalia Maprofesa wengi wameoa wasiofikia kiwango chao cha elimu ikiwezekana anaoa asiyesoma kabisa ambaye atamsujudia kama mume, chanzo cha uchumi, mweneye mawazo pevu na msomi kuliko wote kwenye familia. Hawezi kuulizwa lolote.
Siyo elimu peke yake lakini pia wanaume wanaogopa kuoa mke mwenye kipato kikubwa kuliko yeye. Sababu ni ileile kwamba anakuwa amepunguza utegemezi kwa mume. kutomtegemea mume kunatafsiriwa kama kujivuna. Kuwa tegemezi kunakunyima uhuru. Angalia nchi maskini kama Tanzania, zinazotegemea nchi tajiri hazina ubavu wa kukataa lolote linalosemwa na mtoa misaada. Malawi kwa mfano: ilikataa ndoa za jinsia moja hadi ikawafunga wanaume wawili waliooana, lakini Uingereza ilipinga uamuzi wa mahakama ya Malawi. Kwa kuchelea kunyimwa misaada serikali ya Malawi iliwaachia huru.
Hali kadhalika mwanamke asiyemtegemea mume kwa kila kitu anaonekana tishio kwa mume dikteta
 
haina nafasi kabisa. Elimu, pesana n.k ni mbwembwe zetu tu binadamu na si zaidi ya hapo!
Kama ingekuwa na nafasi, jiulize watu ambao hawakubahatika kwenda shule igekuwaje?!


tuongee ukweli katika hilo,,ni nani yuko tayari kuoa au kuolewa na mtu mjinga,asiejua chochote?asie na shule ya kufuta ujinga japo ya darasa la saba au form four?

After all mke au mume bora ni lazima awe na maarifa japo kwa uchache...!!

Kwa mtazamo wangu me naona ina nafasi kias chake
 
Mambo mengine unaweza kuonekana ni ubaguzi na wengine watasema elimu haina nafasi kwenye kuoa au kuolew na hii itategemea muoji na muoa!

Kwangu mimi elimu ina nafasi kubwa sana, kwakweli kuwa na mtu ambaye hana uwezo wa kuhoji kwanini iwe hivi au hisiwe hivi kwangu ni mzigo! Mwanamke ambaye ana argue na ku reason kwangu mimi ni kipaumbele! Siyo kila kitu ndiyo,ndiyo. Napenda kuona mtu ana hoji ana kushauri.
 
kutegemeana na akili ya wahusika, inaweza kuwa na nafasi ama isiwe na nafasi.
 
kikubwa hapa sio mtu kuwa na reasoning capacity ndo anaogopwa, swala ni je mnafika consensus or nyumba inakuwa kama ukumbi wa debate kila siku wanawake nao hawataki kukubaliana usipokubali jambo lake anaona unakataa kwa sababu yeye ni mwanamke

Hebu turudi nyuma hivi mungu alimwambia Adam nakuletea Eva ili awe nan?
 
Elimu ina nafasi kubwa sana katika kuolewa na nafasi yenyewe ni kwamba ukitaka usiolewe wewe na upigishwe mimba tu watu wakukimbie au wakuibie halafu wakukimbie basi kuwa umesoma sana.Ndio maana ukienda kwenye vyuo vyote malecturer wa kike wengi wao hawajaolewa ila wana watoto jamaa wamepiga kiboga wakachukua mshiko wakakimbia kuchua dogodogo zisizosoma huo ndio ukweli wenyewe.


Hapo kwenye bold unamaanisha hiyohiyo kitu au inatakiwa kurekebishwa?
 
kutegemeana na akili ya wahusika, inaweza kuwa na nafasi ama isiwe na nafasi.

aise haya mambo yana umuhimu wake kama watu wenyewe walivyoelewana. Kwa kizazi cha leo maisha ni tofauti na zamani. Ngoja nikwambie, dingi yangu alikuwa mtumishi na mama akawa mkulima. Dingi alikuwa mkware sana kwani pesa yake nyingi alitumia kunywa na wanawake. Alifika hatua hata kutusomesha hataki. Aise nilipata shida sana lakini chakula kilikuwepo cha kutosha familia. Kuna wakati nililaumu kutosoma kwa mama japo kutuwezesha kwa ada. Ilinibidi nifanye vibarua ili kukidhi ada, na mahitaji mengine thanks God i was clever shule haikunisumbua. Niliapa kwamba sitaweza kuassociate na mtu ambaye hana mwanga na maisha ya sasa. Sisemi kwamba hawafai lakini tafuta mtu ambaye chemistry itakaa vizuri. Ko always nimekuwa sijihusishi na wasichana ninaoona hatutaendana. Onyo: usivamie wasomi kama chemistry haiendani.
 
Elimu ina nafasi kubwa sana katika kuolewa na nafasi yenyewe ni kwamba ukitaka usiolewe wewe na upigishwe mimba tu watu wakukimbie au wakuibie halafu wakukimbie basi kuwa umesoma sana.Ndio maana ukienda kwenye vyuo vyote malecturer wa kike wengi wao hawajaolewa ila wana watoto jamaa wamepiga kiboga wakachukua mshiko wakakimbia kuchua dogodogo zisizosoma huo ndio ukweli wenyewe.
unaeweza ponza watu wakaacha shule kisa ndoa. someni mwaya wadada elimu itawasaidia na familia zenu, men wanawapenda wasosoma ili wawanyanyase na kuwagandamiza
 
:majani7::majani7::majani7::majani7::majani7::majani7::majani7::majani7::majani7::majani7::majani7::majani7::majani7:
 
elimu ina nafasi katika kuoa na kuolewa. maana yake ni kuwa ikiwa mmoja anayo kubwa sana na mwingine kidogo litazuka tatizo la inferiority against superiority... vile vvile tofauti kubwa inasababisha limitation katika mijadala yenu,mambo mengine mtashindwa kujadili kutokana a uelewa. mfano baba ana Phd na mama ni class vii sasa baba anazungumzia mambo fulani yanayohitaji uelewa ataona shida wakati mwingine utajilazimisha kujadili watu badala ya issues. hata hivo usomi wa juu kwa wote unakaribisha mzozo na jeuri hasa kwa mama kwani wakati baba anaekti kama kichwa mama anaweza kukaidi. kwa uzuri baba amzidi kiasi mama
 
Inategemea na vigezo vya muoaji/muolewaji ambavyo vinatofautiana kati ya mtu na mtu. Kwa mfano mwanaume mwingine ambaye ana Masters degree anaweza kuweka vigezo vya kutaka mke ambaye at least amemaliza A' level na mwingine mwenye elimu kama hiyo akawa tayari kumuoa hata aliyeishia darasa la saba.

Elimu ina nafasi gani katika kuoa na kuolewa?
 
Back
Top Bottom