Hivi chagonja anaenda kuchunguza nini songea ilhali majibu anayo tayari

Bramo

JF-Expert Member
Oct 21, 2009
13,160
10,007
Wakuu
IGP Amemtuma ACP Chagonja kwenda kuchunguza kiini cha machafuko ya Songea.
Namnukuu ACP Chagonja kama ifuatavyo Kutoka Mwananchi

" Chagonja akizungumza na Mwananchi jana alisema maandamano hayo hayakuwa ya amani bali ya kihuni kwani yalilenga kuvamia ofisi za serikali ikiwemo Ikulu ndogo na Ofisi ya Mkuu wa mkoa. Chagonja alikuwa akijibu swali lililotaka aeleze endapo haoni kama polisi imetumia nguvu kubwa kutawanya raia waliokuwa wakiandamana kwa amani.

Akaenda mbali zaid
"Maandamano ya amani watu wanavamia Ikulu, maandamano ya amani watu wanazingira ofisi ya mkuu wa mkoa?"
"Sijafika huko ndo naelekea lakini, yale si maandamano ya amani. Yaani wahuni wanataka kuivuruga nchi waachiwe? Kuweni wazalendo, msiwe kama labda ninyi ni waandishi wa BBC kutoka Uingereza, hii ni nchi yenu."


Akaongeza
Alifafanua kwamba, maandamano ya amani yanafahamika kwani watu hulazimika kuomba kibali na kuweka wazi ajenda ya maandamano "Lakini siyo maandamano yale, watu hayakuwa na kibali chochote, wahuni wamejiingiza wanataka kuvuruga nchi tu.".
Atetea Polisi (Wauaji)

Mkuu huyo wa operesheni alitetea polisi akisema,"Usifikirie polisi hawana akili. Haiwezekani watu wazima na akili zao wenye mafunzo wafyatue hovyo risasi za moto kwa raia. Hakuna askari anapenda kuua raia..., lakini watu wanavamia Ikulu, ofisi ya mkuu wa mkoa, magari ya polisi hapo kuna amani kweli?".

Atoa angalizo kwa Media

Alitoa angalizo kwamba ni lazima hata vyombo vya habari, viache ushabiki badala yake viangalie maslahi ya taifa kwani nchi ikivurugika wao pia hawatasalimika na kusisitiza, "Kuweni wazalendo bwana, msifikirie kulishutumu jeshi la polisi tu.".

Source: Mwananchi - 24/2/2012

My Take
Chagonja Tayar jibu analo, so kwenda kwake huko ni Ubadhirifu wa Fedha zetu walipa kodi na kimsingi ni ka aina flan ka ufisadi.
 
Hata waliomtuma wanasubiri nini kumrudisha baada ya kauli yake hiyo!!
 
Kati ya viongozi wa jeshi la polisi wa sasahivi, mimi binafsi namuona chagonja kama moja ya watu bogus sana ndani ya jeshi hilo.

Sina uhakika kama chagonja kasoma sheria, na kwa kuwa ni muajiriwa wa polisi anatakiwa kuzijua sheria na katiba ya nchi, sijui amesoma katiba ganbi inayowataka wananchi kuomba kibali cha maandamano, hadi aseme maandamano yale hayakuwa na kibali.

Na hawa polisisiemu wakae wakijua siku tutakapoiondoa ccm madarakani, wauaji wote wa wananchi watalazimika kusimama kizimbani ili wajibu hizi tuhuma za mauaji dhidi ya raia wasiokuwa na hatia.
 
nimesoma kwenye mwananchi kwakweli ni upotevu wa fedha za umma, maana ameshatoa hukumu yakile anachokwenda kuchunguza, MUNGU tuepushie askari wetu wanaotetea uzalendo wa nchi yao kwakuua raia wao ambao wanajaribu kuwakumbusha viongoz wajibu wao wamsingi
 
Ningekuwa IGP Mwema, ningemwambia tu arudi hata kabla hajafika huko Songea maana ni kama majibu yote anayo. Hivi inakuwa watu wa*****i kama huyu wanapewa jukumu la kufanya uchunguzi kwa issue sensitive kama hii. Ila haistaajabishi, maana huu ndo mtindo wa utawala wa nchi.

IGP kaonyesha kufadhaishwa, huyo Chagonja yeye wala hamnazo kabisa, kwake ni ule msemo wa kawaida wa CMM 'business as usual'-Yana mwisho haya. Ule mcharuko wa kauli pingana za ikulu na bunge juu ya posho, madhara yake sasa yana 'trickle down the ladder'.
 
Back
Top Bottom