Uchaguzi 2020 Hivi CHADEMA walikuwa wanawaambia nini Wananchi wakati wa kampeni?

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wadau, amani iwe kwenu.

Ni dhahiri sasa Tanzania ya Kijani imewezekana. Na hii ni kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanyika ndani ya chama chetu. Viongozi wetu wametupeleka ng'ambo kusoma ili tuendeshe chama kisayansi na kuendesha kampeni kisasa na bila jasho.

Kwenye kampeni zetu wagombea wetu kuanzia ngazi ya Urais, Ubunge na udiwani walikuwa wanahubiri maendeleo, amani, utulivu na umoja wetu. Wamehubiri nini tumefanya ndani ya miaka 5 na nini tumeahidi kufanya katika miaka 5 ijayo. Mgombea wetu wa Urais Dr Magufuli ilipobidi alikuwa anatatua kero za papo kwa papo. Kwa kifupi tuliingia ndani ya nafsi za wananchi.

Kikubwa zaidi yule tuliyemjua ni mwenzetu tulihakikisha anapiga kura na tumefanikiwa katika hilo.

Hawa wenzetu sijui walikuwa wanahubiri nini kwenye kampeni zao licha ya kujisifu walikuwa wamejaza watu na wamefanya mikutano mingi kuliko CCM (HOJA YA UONGO). Mbaya zaidi wale waliowakimbilia kwenye kampeni wamekimbia kwenye kupiga kura. Hawakujitokeza mwisho wa siku CCM tumefanikiwa mbinu zetu kwa zaidi ya asilimia 90. Sasa ni dhahiri tunaenda kukamata mihimili yote ya dola. Hivi 2025 wanasalimikaje kwa mfano.

Hii ndio CCM aliyotuachia baba wa Taifa hayati mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Kumbuka katibu Mkuu aliyemaliza muda wake Abdulrahman Kinana alisema CCM tuna mbinu zaidi ya 200. Mwaka 2015 tulikuja na mbinu ya BAO LA MKONO. Mwaka 2020 tumetumia mbinu ya Ujanifishaji (Tanzania ya Kijani). 2025 tutakuja na kubwa lao.

Nawasilisha.
 
Lissu yule baba muongo jamani sijapata kuona. Eti oohh nitaingiza watu barabarani nikishindwa uchaguzi. Saizi kajifungia chumbani na mke wake wanacheza YOPE.
Hivi wewe ni ukoo wa Lowassa kweli au umeambulia kufanana jina tu!.

Usijekuwa unawapigia debe wasio na habari na wewe au labda ulikuwa housegirl kwenye nyumba yao?! Na ma hg mnavyojua kujipendekeza, mara ushike remote kama upo kijijini kwenu.
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Ni dhahiri sasa Tanzania ya Kijani imewezekana. Na hii ni kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanyika ndani ya chama chetu. Viongozi wetu wametupeleka ng'ambo kusoma ili tuendeshe chama kisayansi na kuendesha kampeni kisasa na bila jasho.

Kwenye kampeni zetu wagombea wetu kuanzia ngazi ya Urais, Ubunge na udiwani walikuwa wanahubiri maendeleo, amani, utulivu na umoja wetu. Wamehubiri nini tumefanya ndani ya miaka 5 na nini tumeahidi kufanya katika miaka 5 ijayo. Mgombea wetu wa Urais Dr Magufuli ilipobidi alikuwa anatatua kero za papo kwa papo. Kwa kifupi tuliingia ndani ya nafsi za wananchi.

Kikubwa zaidi yule tuliyemjua ni mwenzetu tulihakikisha anapiga kura na tumefanikiwa katika hilo.

Hawa wenzetu sijui walikuwa wanahubiri nini kwenye kampeni zao licha ya kujisifu walikuwa wamejaza watu na wamefanya mikutano mingi kuliko CCM (HOJA YA UONGO). Mbaya zaidi wale waliowakimbilia kwenye kampeni wamekimbia kwenye kupiga kura. Hawakujitokeza mwisho wa siku CCM tumefanikiwa mbinu zetu kwa zaidi ya asilimia 90. Sasa ni dhahiri tunaenda kukamata mihimili yote ya dola. Hivi 2025 wanasalimikaje kwa mfano.

Hii ndio CCM aliyotuachia baba wa Taifa hayati mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Kumbuka katibu Mkuu aliyemaliza muda wake Abdulrahman Kinana alisema CCM tuna mbinu zaidi ya 200. Mwaka 2015 tulikuja na mbinu ya BAO LA MKONO. Mwaka 2020 tumetumia mbinu ya Ujanifishaji (Tanzania ya Kijani). 2025 tutakuja na kubwa lao.

Nawasilisha
Magufuli na wapwa zake wanadhani wanaweza kumdhihaki Mungu mpaka unazunguzia uchaguzi wa 20125 wakati tutafanya uchaguzi mwingine tena ulio huru na wa haki kabla ya 2025. Nature inafanya kazi yake na kuna mtu anakwenda kumfuata Mkapa alikokwenda kabla ya hiyo 2025.
 
Back
Top Bottom