Lizaboni
JF-Expert Member
- Feb 21, 2013
- 33,894
- 20,372
Wadau, amani iwe kwenu.
Ni dhahiri sasa Tanzania ya Kijani imewezekana. Na hii ni kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanyika ndani ya chama chetu. Viongozi wetu wametupeleka ng'ambo kusoma ili tuendeshe chama kisayansi na kuendesha kampeni kisasa na bila jasho.
Kwenye kampeni zetu wagombea wetu kuanzia ngazi ya Urais, Ubunge na udiwani walikuwa wanahubiri maendeleo, amani, utulivu na umoja wetu. Wamehubiri nini tumefanya ndani ya miaka 5 na nini tumeahidi kufanya katika miaka 5 ijayo. Mgombea wetu wa Urais Dr Magufuli ilipobidi alikuwa anatatua kero za papo kwa papo. Kwa kifupi tuliingia ndani ya nafsi za wananchi.
Kikubwa zaidi yule tuliyemjua ni mwenzetu tulihakikisha anapiga kura na tumefanikiwa katika hilo.
Hawa wenzetu sijui walikuwa wanahubiri nini kwenye kampeni zao licha ya kujisifu walikuwa wamejaza watu na wamefanya mikutano mingi kuliko CCM (HOJA YA UONGO). Mbaya zaidi wale waliowakimbilia kwenye kampeni wamekimbia kwenye kupiga kura. Hawakujitokeza mwisho wa siku CCM tumefanikiwa mbinu zetu kwa zaidi ya asilimia 90. Sasa ni dhahiri tunaenda kukamata mihimili yote ya dola. Hivi 2025 wanasalimikaje kwa mfano.
Hii ndio CCM aliyotuachia baba wa Taifa hayati mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Kumbuka katibu Mkuu aliyemaliza muda wake Abdulrahman Kinana alisema CCM tuna mbinu zaidi ya 200. Mwaka 2015 tulikuja na mbinu ya BAO LA MKONO. Mwaka 2020 tumetumia mbinu ya Ujanifishaji (Tanzania ya Kijani). 2025 tutakuja na kubwa lao.
Nawasilisha.
Ni dhahiri sasa Tanzania ya Kijani imewezekana. Na hii ni kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanyika ndani ya chama chetu. Viongozi wetu wametupeleka ng'ambo kusoma ili tuendeshe chama kisayansi na kuendesha kampeni kisasa na bila jasho.
Kwenye kampeni zetu wagombea wetu kuanzia ngazi ya Urais, Ubunge na udiwani walikuwa wanahubiri maendeleo, amani, utulivu na umoja wetu. Wamehubiri nini tumefanya ndani ya miaka 5 na nini tumeahidi kufanya katika miaka 5 ijayo. Mgombea wetu wa Urais Dr Magufuli ilipobidi alikuwa anatatua kero za papo kwa papo. Kwa kifupi tuliingia ndani ya nafsi za wananchi.
Kikubwa zaidi yule tuliyemjua ni mwenzetu tulihakikisha anapiga kura na tumefanikiwa katika hilo.
Hawa wenzetu sijui walikuwa wanahubiri nini kwenye kampeni zao licha ya kujisifu walikuwa wamejaza watu na wamefanya mikutano mingi kuliko CCM (HOJA YA UONGO). Mbaya zaidi wale waliowakimbilia kwenye kampeni wamekimbia kwenye kupiga kura. Hawakujitokeza mwisho wa siku CCM tumefanikiwa mbinu zetu kwa zaidi ya asilimia 90. Sasa ni dhahiri tunaenda kukamata mihimili yote ya dola. Hivi 2025 wanasalimikaje kwa mfano.
Hii ndio CCM aliyotuachia baba wa Taifa hayati mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Kumbuka katibu Mkuu aliyemaliza muda wake Abdulrahman Kinana alisema CCM tuna mbinu zaidi ya 200. Mwaka 2015 tulikuja na mbinu ya BAO LA MKONO. Mwaka 2020 tumetumia mbinu ya Ujanifishaji (Tanzania ya Kijani). 2025 tutakuja na kubwa lao.
Nawasilisha.