Elections 2010 Hivi CHADEMA haina wataalamu, au viongozi wake ndiyo wasioambilika?

ACHA KUKURUPUKA wewe, Swali nimeuliza mimi, wewe unaanza kihere here chako. nimekupa na wewe kazi ya kufanya mahesabu ya AHADI ya chama chako jembe na nyundo utueleze kimahesabu kama zinatekelezeka au la. Pili zipo kwenye ilani yenu ya chama au niza mgombea wenu na si za chama. katika mchanganuo wako usisahau na ahadi ya BAJAJ 400 kama zipo ktk ilani yenu au siku mgombea wenu wakati anautubia aliona BAJAJ inapita mbele akaona ni mtaji hivyo akatoa ahadi
Nikisema nawe ni mhuni nitakuwa nimekosea? Soma mara mbili bandiko lako na utajua kwa nini nimediriki kukuita mhuni.
 
Unahitaji kuiedit kazi yako uliyoi paste hapa manake haileti hamu ya kuisomaa, weka paragraphs ivutie mkuu!
 
Dabomani umetumia nguvu kubwa sana kujaribu kuonyesha ahadi za Slaa hazitekelezeki. Hata hivyo, ni kama kumpigia mbuzi gitaa, midundo yako haichezeki. Haichezeki kwa kuwa imekosa ushahidi wa kisayansi. Bahati mbaya kwako ulidhani unahutubia mkutano wa hadhara ambao watu watakusikiliza na kukuacha uende zako. Hapa no mzee. Kwa kifupi ahadi zote za Chadema zinatekelezeka. Mpe kura yako tarehe 31 Oktoba halafu uje umpime kwazo 2015.
 
Dabomani,

Mbona hushangai ahadi ya:

1. Kigoma kuwa Dubai.
2. Mwanza kuwa Carlifonia??
3. Uwanja wa ndege Mbeya, Kigoma, na .................. (hebu ongezeeni).
4. Ongezeko la Mishahara ambalo baadaye wamekana kuwa si kweli.
5. Kuleta maji Tanga wakati Dar penyewe hayapo.
6. Barabara za Fly-oveer Dar na ujenzi wa njia za Rapid Bus ambao waliahidi tangu mwaka 2005.
7. Umeme wa uhakika na tukaishia kupewa RICHIMONDULI.
8. Wanafunzi wote Tanzania kuwa na Laptop wakati umeme hamna.
9. Ameahidi BAJAJI 400 kwa akina mama waja wazito. Hebu muone mama na mtumbo kwenye Bajaji.
10. Katujengea bora shule Tanzania nzima badala ya shule bora. Hii katimiza ahadi.

Mengine mengi watakuja jamaa wengine waongezee.

Naona mkuu umekaa sana Majuu na kusahau kuwa Tanzania iko bado vilevile. Unafikiri huku kila mtu ana Internet. Sanasana ni watu kuwa na simu na siyo Internet. Rudi uone RUMBA la Tanzania ndiyo uanze kukosoa. Wengi wanaoshinda humu sidhani hata watapiga kura. Hivyo kama wahutubia basi mbegu zako zimeangukia kwenye Miiba na Magugu.

Sikonge,

Wana ccm wengi wana makengeza ... wanaona tu upande mmoja
 
Dabomani,
Mkuu wangu kusema kweli sijakuelewa kabisa ktk mada hii unazungumzia vitu vikubwa kwa kutumia mifano midogo sana isiyolingana. Unazungmzia Alibaba.com kama soko kubwa sijui nani alokwambia hivyo ndivyo Utawala bora unavyowaandaa wananchi wake.

Pili, swala la Usafiri wa reli leo hii hatuna kabisa, hivyo kuufikiria tu umuhimu wake unatosha kwa mwenye elimu na msomi kama wewe kukubali haja ya kuwa na usafiri acha hizo ahadi za masaa kuwa kigezo kikubwa cha Upinzani wako. Yaani hapa swala kubwa kwako ni masaa mangapi mtu ataweza kutoka Dar kwenda Mwanza badala ya kuzungumzia Usafiri wa reli ambao kichwa kimoja kinaweza vuta mabehewa 60 hadi 100 yenye mali inayoweza kubebwa na malori 200 kwa usafiri wa siku nne kufika hadi Mwanza..

Sasa hapa napata mshangao mkubwa sana kwa msomi kama wewe kuzungumzia zaidi ahadi ya masaa badala ya kufikiria kwanza uwezekano wa kuwa na usafiri wenyewe na upi unaotufaa kulingana na mahitaji yetu bila kusahau uwezo wetu..

Tatu, umezungumzia swala la Saruji na kusema kwamba Clinker inaagizwa China sijui ndio wanauza bei rahisi, wewe umefanya utafiti na kujua kwamba Tanzania hatu produce Clinker? Je ikiwa Hiyo jasi ndio tunaagiza na sii Clinker kuna uwezekano wa saruji kuuzwa bei ya Tsh. 5000 maanake sijui kama kweli msomi wewe umefanya utafiti wa kutosha. Ebu rudia tena kutafiti kisha rudi na majibu yenye kuleta maana.

Mkuu ni bora zaidi mtu uzungumzie mapungufu ya sera za Chadema kwa kuorodhesha yale yanayowezekana kufanyika na sii habari ya gharama kwani hiyo hiyo cement kutoka nchi jirani inauzwa bei nafuu sana kuliko hiyo inayotengezwa nchini na kwa mfano wako sijui hao wenzetu waliweza vipi kukabiri gharama za Clinker. tena hujaweka gharama zaidi ya walanguzi ambao wanaitoa cement nchi za majirani na kuingiza nchini.

Ifike wakati watu tufikirie zaidi Maendeleo ya nchi kwa hisia za Ushindi na sii kutumia lugha ya KiCCM kwamba HAIWEZEKANI hali kitu kinawezekana kabisa.
 
Katika watu wenye utumwa wa kiakili ni huyu jamaa alieandika this baseless and pointless topic,

yeye kama kapewa hela na kuwekwa pale upanga ili aanze kuandika utumbo tunampa pole. Ukombozi ni lazima na kwa sasa tunayo elimu nzuri ya urai

yote anayosema drkt wa ukweli yanawezekana provided hao waliomtuma kuandika hayo wasiibe kura.

Kwanini tuandikie mate wino upo, tumpe nafasi drkt uone kazi itakavyofanyika, kwanini tuwe na baraza la mawaziri 46???? Eti kisa unalipa fadhili!!!!!! Wakati watanzania milion 42 wanateseka, tunataka drk slaa akabadili katiba ya kinyonyaji, tunataka drkt slaa akatoe elimu bure na afya bure, tunataka drkt slaa akasikie kilio cha watantanzania kwa kurudisha uwajibikaji-sio hao waliokutuma kuandika mtu anaandikwa fisadi weeeeeee rais anajifanya kiziwi na bubu, tunataka rais muwajibikaji hatutaki rais anaewachekea mafisadi, tunataka rais anapanga mipango ya kuwafanya watanzania kuwa na makazi bora, inawezekana kwa serikali inayowajiba acha umbumbumbu, na kujiita wewe mtaalam. Jamani inawezekana tunataka rais anaeangalia mfumuko wa bei sio anaechangia mfumuko wa bei, tunataka rais who can demonstrate walk the talk, tuliambiwa eti ninawafahamu mapapa nitawafikisha mbele ya dola leo hii mtu huyohuyo anawapigia debe mafisadi sijui ramba, chnye, richmond jamani kama kweli unataka kupima wapi kuna wataalamu tulinganishe chadema na ccm? Hata mtu wa mtaani tuuu hawezi kumpeleka mtu mahakamani kwa ufisadi then akaja kumpigia debe, are we real serious????? Wanafungwa watu walioiba kuku hawa wanaombewa kura hivi hii si dharau kweli??? Tuseme kweli?? Labda wafanye vinginevyo lakini hapa hawachomoki kwa drkt slaa -aliepata udkt mwaka 1982 achana na drk za sura, naweza kesha hapa lakini madudu ni mengi tumeyaona -mwalimu nyerere alisema ccm sio baba yetu ni wakati muafaka umefika, katika kitu ambacho drkt slaa amefanikiwa kwa sasa ni elimu ya uraia na kujiamni, you cant fool all people all the time, sawa fanyeni mfanyalo sasa lakini kumbukeni you cant fool all people all the time, we need slaa and people like slaa we know them-mwakyembe good example, magufuli good example but for sure they cant do more ndani ya uchafu tunaouona, if we get a team of peole like tundu lisu, zito, mbowe, mwakyembe, mpandozoe, marando,young fighters like halima mdee, waitara, godbless lema, mwanza man, john mnyika, but also put lipumba as economic advisor-while slaa is presidar, nakwambia patawaka moto -foleni hatutaiona dar, mshahara kima cha chini 350000/=, nyumba nzuri zitajengwa na mifuko ya jamii, afya na shule bure, mikataba ya kinyonyaji mwisho, katiba mpya, na mwisho demokrasia ya kweli na maisha bora.
 
Jamani mambo ya kusema hatuwezi ndo kuendelea kuwa jalala la vifaa vibovu kila mwaka. Tunataka viongozi wabunifu siyo viongozi wenye tamaa, hata kutatua matatizo ya mahitaji ya kila siku hawawezi. Kiongozi anatakiwa kuonyesha njia wapi twende na wapi tusiende kwa wakati muafaka.

Train kwenda mwanza kwa masaa 3 inawezekana, kama haiwezekani tulishajaribu hata hiyo yenye kutumia siku moja? Hebu mtu aseme hapa kuna nini cha kujivunia Tanzania tunachotegemea baada ya muda fulani tutakuwa tumengeneza au tutakuwa tunauza nje?

Ni aibu kuwa wateja kila wakati bila kujiuliza kwa nini hatuuzi? Tuache ubishi, Dr Slaa anaweza kurudisha uzalendo ktk nchi yetu
 

Miongoni mwa wagombea uraisi ambao wamekuwa wakitoa ahadi ambazo kwa mtizamo wangu zina walakini mkubwa, ni Dr. Slaa wa CHADEMA. Miongoni mwa ahadi hizo ni ile ya kuweka treni ya masaa matatu kutoka Mwanza hadi Dar es Salaam, na ile ya kushusha bei ya saruji hadi shilingi 5,000.00 kwa mfuko wa saruji wa kilo 50.
Inawezekana CHADEMA haikuwa na nia ya kutudanganya, lakini wanawezaje wakajitetea kuwa wamekuja na ahadi nzito kiasi hicho bila kufanya utafiti? Tangu kampeni hizi zimeanza chama hiki kimefanya makosa mengi mno ya kiufundi na ya wazi, kiasi kwamba mtu unabaki ukiwa umepigwa na bumbuwazi. Ni vipi chama kichanga kiasi hicho kiwe na matumaini ya kupewa ridhaa ya kuongoza nchi? Ushauri wangu kwa CHADEMA ni kwamba viongozi na wagombea wake wawe wanatoa ahadi baada ya kuzifanyia kazi; vinginevo watagundua kuwa Watanzania wanaowadhania ni wajinga, kumbe ni wajanja kuliko wao.
[/QUOTE]


Wewe ni mjinga kwelikweli ama unataka kuwadanganya watu kwa makusudi. Lazima uwe mnufaika wa uongozi dhaifu na m-bovu ulioko madarakani ama mwenyewe pia ni m-bovu japo wadhani kuwa ni mtaalamu.
Kwanza suala la umbali kutoka Mwanza hadi Dar es Salaam kuwa km 1,200 ni uongo. Kwani ndege kubwa hutumia saa moja na hakuna ndege yenye kasi ya kilomita hizo kwa saa. Huo umbali unaousema wewe ni huu wa njia za treni za mwaka 47. Wala treni ya kasi kiasi hicho usidhani itatumia njia chakavu zilizopo, wala mfumo m-bovu wa umeme uliopo sasa. Ni lazima ziwepo njia mpya tena za mkato na umeme wa uhakika. Hivyo umbali kutoka Dar hadi Mwanza unaweza kupunguzwa kiasi kikubwa. Pili, umeendeleza upotoshaji wako kutaka watu waamini kuwa treni hiyo ni mradi wa miaka mitano. Si kweli, usimuwekee Dr. wa kweli maneno mdomoni mwake – anayo ya kwake makini na ya kutosha. Ukitaka kuwa muongo mzuri (kama unavyojidhania kuwa) basi uwe pia na kumbukumbu. Alichosema Dr (wa ukweli aliyesomea si kupewa kama ruzuku) ni kuwa umefika wakati tuwe na mipango ya maana ya taifa ya muda mrefu (visheni/maono). Hivyo wakati binadamu wenzetu wanafikiria kutua kwenye sayari za mbali basi nasi angalau kwa miaka 15 ijayo tuwe na treni ya kasi hiyo. Ikiwa sasa zipo treni zenye kasi ulizoelezea (km 250 hadi 400 kwa saa) ni dhahiri katika kipindi cha miaka hiyo 15 mambo yatakuwa bora zaidi. Usipoteze muda wako kudanganya kuwa ni ahadi ya miaka mitano, si kweli. Mwaka huu Watanzania tulikwisha kuweka wazi na kukuonya kuwa “hatudanganyiki”!
Pili ni kuhusu sementi. Mpaka sasa ni kiasi kidogo sana cha klinka ambacho kinaagizwa kutoka nje ya nchi. Haifiki hata asilimia tano. Sehemu kubwa inatoka hapahapa nchini na huzalishwa na malighafi zinazopatikana karibu kabisa na viwanda husika. Klinka si malighafi bali ni zao la kati (intermediate product) katika uzalishaji wa sementi. Kiwanda cha Twiga Cement na Tanga ndivyo vina mipango hiyo ya kuagiza klinka lakini ni nyakati za mahitaji makubwa tu. Hivyo ni kiasi kidogo mno. Pia ufahamu kuwa hivi sasa kuna viwanda kadhaa (kule Tanga [Arthi River Mining], Mtwara, Dar es Salaam) ambavyo viko kwenye hatua mbalimbali za ujenzi kwa ajili ya kuzalisha saruji. Kiwanda cha Wazo kina mpango wa kufanya upanuzi wa kiwanda na ukarabati unaendelea sasa kwenye moja ya chungu (500 t/day kiln) cha kuzalishia klinka. Hivyo ni uposhaji mkubwa kuchukua bei ya klinka ya China na kuiweka kuwa ndicho kipimo cha sementi ya Tanzania.
Labda wasomaji wajue tu kuwa hiyo klinka huzalishwa kutokana na madini ya chokaa ambayo kwa lugha za wenzetu huitwa limestone, udongo mwekundu (red soil), mchanga wa mtoni (river sand), (wakati mwingine madini ya chuma), gypsum na vikorombwezo vingine vyenye lengo la kupunguza kiasi cha klinka kwenye sementi. Kwa upande wa Tanga na Mbeya ili kupunguza klinka wao hutumia pozzolana, aina ya klinka ambayo ilitengenezwa zamani na volcano, ambapo wanaweza kutumia hadi asilimia 35. Kwa mfano sementi za Tanga tunazotumia moja (Ordinary Portland Cement) ina klinka 80%, madini ya chokaa 15% na gypsum 5%, nyingine Pozzolana Portland Cement ina klinka 60%, pozzolana 35% na gypsum 5%. Madini yote haya hupatikana kwa wingi mno hapahapa Tanzania. Pozolana inayotumika Tanga sementi hutoka Holili na gypsum hutoka Makanya (Kilimanjaro). Ile pozolana ya Mbeya wanachota karibu kabisa na kiwanda. Twiga sementi wao hupata gypsum yao kutoka Makanya, Lindi (gredi ya juu kabisa) na Itigi.
Ni dhahiri kukiwa na mipango mizuri (kama ya CHADEMA) utashi na nia thabiti (wala si nia zaidi) inawezekana kabisa kuuza mfuko mmoja wa saruji kwa shilingi elfu tano. Kwani wakati Kikwete anaingia madarakani mfuko wa sementi ulikuwa shilingi ngapi? Kwa tarifa yako ilikuwa bei hiyohiyo anayosema Dr. wa kweli. Kuuza kwa shilingi elfu tano ni sawa tu na kuondoa uharibifu wa miaka mitano uliofanywa na serikali mbofu (mkangafu) na dhaifu iliyopo madarakani. Unajua sementi ya Kenya ingeuzwa kiasi gani kama si kodi za kulazimisha inayotozwa? Hivi unajua nyumba bora ina thamani kiasi gani katika kupunguza (adui) maradhi na kustawisha maisha ya Watanzania? Hata kama ikibidi kutoa ruzuku ni sawa. Ruksa!
Tueleze wewe mtaalamu, zile ruzuku wanazopewa makampuni makubwa ya (matajiri) madini kwa njia ya msamaha wa kodi, serikali yako tukufu inazitoa wapi? Kwa nini hasa unapinga hatua makini za kuwakomboa Watanzania? Mwenzetu una nyumba na hutaki na sisi tujenge? Unapodhamiria kujenga taifa kama letu si lazima kila kitu kiwe na mantiki ya kiuchumi. Taifa kwanza!
Sasa lazima tufanye uamuzi. Kuwezeshwa kujenga au kuyawezesha makampuni ya matajiri kupora madini yetu? Kuendeleza reli chakavu au kuanza kufikiria na kutekeleza njia za treni za kasi? Tuchague, maana kupanga ni kuchagua, kila mmoja wetu aweze kutibiwa bila malipo anapougua ama tulipie na serikali ichagie huduma duni za matibabu?. Tarehe 31 Oktoba tuseme kwa sauti ya kusikika kama tunataka watoto wa taifa hili wasome kwa kadri ya akili zao au kwa kadri wa uwezo wa kifedha wa mifuko ya wazazi wao? Hayo ndiyo ya kuamua wala si uwongo uliouweka mtoa kiroja.

Dawa ya Mjinga ni kuumia
 

Miongoni mwa wagombea uraisi ambao wamekuwa wakitoa ahadi ambazo kwa mtizamo wangu zina walakini mkubwa, ni Dr. Slaa wa CHADEMA. Miongoni mwa ahadi hizo ni ile ya kuweka treni ya masaa matatu kutoka Mwanza hadi Dar es Salaam, na ile ya kushusha bei ya saruji hadi shilingi 5,000.00 kwa mfuko wa saruji wa kilo 50.
Inawezekana CHADEMA haikuwa na nia ya kutudanganya, lakini wanawezaje wakajitetea kuwa wamekuja na ahadi nzito kiasi hicho bila kufanya utafiti? Tangu kampeni hizi zimeanza chama hiki kimefanya makosa mengi mno ya kiufundi na ya wazi, kiasi kwamba mtu unabaki ukiwa umepigwa na bumbuwazi. Ni vipi chama kichanga kiasi hicho kiwe na matumaini ya kupewa ridhaa ya kuongoza nchi? Ushauri wangu kwa CHADEMA ni kwamba viongozi na wagombea wake wawe wanatoa ahadi baada ya kuzifanyia kazi; vinginevo watagundua kuwa Watanzania wanaowadhania ni wajinga, kumbe ni wajanja kuliko wao.
[/QUOTE]
 
. Miongoni mwa ahadi hizo ni ile ya kuweka treni ya masaa matatu kutoka Mwanza hadi Dar es Salaam, na ile ya kushusha bei ya saruji hadi shilingi 5,000.00 kwa mfuko wa saruji wa kilo 50.
Tuanze kwanza kuangalia hii ahadi ya treni. Umbali kutokaMwanza hadi Dar es Salaam ni kilometa 1,229. Ili kuwa na treni ya kuweza kusafiri kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza kwa masaa matatu, itailazimu treni hiyo iwe na mwendo kasi wa kilometa 410 kwa saa moja! Hivi sasa treni inayoshikilia rekodi kwa mwendo wa kasi ni ile ya Maglev inayofanya safari zake kati majiji ya Shanghai na Beijing, kule China. Treni hii ina mwendo kasi wa kilometa 431 kwa saa. Treni nyingine maarufu duniani kwa mwendo kasi ni Shinkasen ya Japan, kilometa 260 kwa saa na Eurostar ya Ulaya, kilometa 250 kwa saa!
[

Utashangaa wanaoamini uongo wa Dr Slaa wanasema "HATUDANGANYIKI." Tatizo hapa ni kwamba anayepiga mahesabu ya kiuchumi ya Chadema ni MGOMBEA MWENZA

Tukija kwenye ahadi ya kuuza mfuko wa saruji kwa shilingi 5,000/- tu, hapa napo inabidi tujiulize: Hivi CHADEMA haina wataalamu wa uchumi, au mgombea wao ndiye asiyeambilika?

Hapo sina jibu, ila kama waliweza kuandika historia kwa kumsimamisha mgombea mwenza wa darasa la saba, it is possible kwamba hawana wachumi wakweli.
 
Dawa ya Mjinga,

Labda huyu jamaa asome pia hapa apate kuona kwamba tumekatisha hata production ya Clinker huko Mbeya kutokana na soko na kikubwa zaidi Uongozi mbaya wahao wasomi wetu..Bofya
 
aiseeeeeee ulikuwa na muda kiasi hiki kuandika pumba hizi bora ungeenda kulima anyaway utakuwa umepewa something ili ujipoze mpe hi makamba:blah:
 
Wewe ni mjinga kwelikweli ama unataka kuwadanganya watu kwa makusudi. Lazima uwe mnufaika wa uongozi dhaifu na m-bovu ulioko madarakani ama mwenyewe pia ni m-bovu japo wadhani kuwa ni mtaalamu.
Kwanza suala la umbali kutoka Mwanza hadi Dar es Salaam kuwa km 1,200 ni uongo. Kwani ndege kubwa hutumia saa moja na hakuna ndege yenye kasi ya kilomita hizo kwa saa. Huo umbali unaousema wewe ni huu wa njia za treni za mwaka 47. Wala treni ya kasi kiasi hicho usidhani itatumia njia chakavu zilizopo, wala mfumo m-bovu wa umeme uliopo sasa. Ni lazima ziwepo njia mpya tena za mkato na umeme wa uhakika. Hivyo umbali kutoka Dar hadi Mwanza unaweza kupunguzwa kiasi kikubwa. Pili, umeendeleza upotoshaji wako kutaka watu waamini kuwa treni hiyo ni mradi wa miaka mitano. Si kweli, usimuwekee Dr. wa kweli maneno mdomoni mwake – anayo ya kwake makini na ya kutosha. Ukitaka kuwa muongo mzuri (kama unavyojidhania kuwa) basi uwe pia na kumbukumbu. Alichosema Dr (wa ukweli aliyesomea si kupewa kama ruzuku) ni kuwa umefika wakati tuwe na mipango ya maana ya taifa ya muda mrefu (visheni/maono). Hivyo wakati binadamu wenzetu wanafikiria kutua kwenye sayari za mbali basi nasi angalau kwa miaka 15 ijayo tuwe na treni ya kasi hiyo. Ikiwa sasa zipo treni zenye kasi ulizoelezea (km 250 hadi 400 kwa saa) ni dhahiri katika kipindi cha miaka hiyo 15 mambo yatakuwa bora zaidi. Usipoteze muda wako kudanganya kuwa ni ahadi ya miaka mitano, si kweli. Mwaka huu Watanzania tulikwisha kuweka wazi na kukuonya kuwa "hatudanganyiki"!
Unaweza kuwa ni miongoni mwa walimbukeni wengi huko chadema kwa kutetea upupu huu pasipo udhibitisho rasmi. Umbali toka Dsm mpaka Mza kwa treni ni km 1260 hivi. Tena kumbuka vizuri ni kwa treni! Kwa barabara umbali huo unaweza kupungua kwa asilimia kadhaa, na kwa usafiri wa anga unapungua kwa asilimia kubwa.

Ukipima umbali huo moja kwa moja toka kwenye ramani, utapata kilometa 850.20 hivi. Na sijawahi kuona reli iliyoonyoka toka pointi A hadi B kama ambavyo wewe unavyotaka kutuambia hapa!

Reli ya kati imepita katika mikoa zaidi ya minne(Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga, na Mwanza), sasa wewe na slaa wako mnataka kutuambia kuwa mtajenga reli mpya bila kupita katika mikoa hiyo? Mtaipitisha angani nini? Je wananchi wa mikoa iliyobaki wasahau huduma hiyo muhimu kwao kwa usafiri?

Treni ya sasa yenye kutumia diseli inakwenda kilomita 65 kwa saa, na ina vituo vingi, ndio maana inachukua karibu masaa 39 kufika Mwanza ilhali ndege yenye kutumia injini za jet inachukuwa sio zaidi ya saa moja. Usafiri kwa barabara sasa upunguza umbali, kwani asilimia 90 ya barabara hiyo ipo katika kiwango cha lami, hivyo kuruhusu magari madogo kusafiri zaidi ya kilomita 100 kwa saa, mabasi kilomita 80 kwa saa (ingawa madereva wengi wa mabasi hayo uendesha km 100-120 kwa saa) na malori ya mizigo km 80 kwa saa.
 
Hivi sasa tunaishi katika kipindi ambacho wataalamu na wanahistoria ya maendeleo ya kitekinolojia katika ulimwengu wanakiita 'information age', yaani kipindi cha 'habari na mawasiliano'. Kwa mujibu wa wataalamu na wanahistoria hawa, kipindi hiki kimeanza mwanzoni mwa miaka ya 1990, na kuchukua nafasi ya kipindi kilichotangulia ambacho wenyewe walikiita 'industrial age', yaani kipindi cha 'mapinduzi ya viwanda'.
Tofauti na huko nyuma, hiki ni kipindi ambacho taarifa na habari zinatembea kwa kasi kubwa sana na kuwafikia watu wengi zaidi kuliko muda mwingine wowote ule katika historia ya mwanaadamu. Aidha ni kipindi ambacho taarifa na habari mpya zinazoingia na kusambaa ulimwenguni kila siku ni nyingi mno, kiasi kwamba mtu anayetaka kwenda sambamba na wakati, analazimika awe ni mwanafunzi wa kudumu.
Wataalamu wa tekinolojia ya habari na mawasiliano wanakisia kuwa kila baada ya miezi kumi na nane habari zinazohusu nyanja mbalimbali zinazoingia na kusambaa ulimwenguni zinaongezeka mara dufu!
Maendeleo katika tekinolojia ya computer yaliyopelekea kuvumbuliwa kwa computer ndogo za mezani na mapajani; uvumbuzi wa mtandao wa kidunia wa internet (world wide web) unaowawezesha wamiliki wa computer duniani kote kujiunga na kisha kupokea, kutuma, kubadilishana, na kupashana habari; na ujio wa mawasiliano ya simu za kiganjani, kwa pamoja ndiyo yaliyozaa kipindi hiki.
Kipindi hiki kimezaa mabadiliko makubwa sana katika nyanja zote za maisha. Mifano ni mingi sana inayoweza kutumika kulidhihirisha hili.
Hebu tutazame mifano michache: Kiasili, serikali ni taasisi ambayo ina umbile la piramidi. Juu zaidi kuna raisi, au waziri mkuu, au mfalme, nakadhalika. Chini ya huyu kunaweza kuwa na makamu wa raisi na waziri mkuu, ambao chini yao nao kuna baraza la mawaziri. Mtiririko huu unakwenda mpaka tunampata mtendaji wa mtaa au kijiji, nakadhalika.
Katika umbile la namna hii tunapata kitu kinachoitwa URASIMU. Jambo zito na lenye uwezekano wa kutikisa Taifa zima linaweza kutokea katika ngazi ya kijiji, lakini hadi raisi apate taarifa za jambo hilo, inaweza kuchukua muda mrefu na pengine asipate taarifa hizo kabisa. Kinachotokea ni kwamba mmoja au baadhi ya viongozi walioko kwenye ngazi za kati, kwa ajili tu ya kulinda maslahi yao, au kwa hofu wanaamua kuacha kuendelea kutoa taarifa katika ngazi zinazofuatia juu yao.
Hapa nchini miaka ya nyuma kuna maeneo yalikuwa yanakumbwa na njaa hadi baadhi ya Wananchi wanapoteza maisha yao, lakini viongozi wa juu wa serikali wanaishia kupata taarifa hizo kupitia vyombo vya habari. Hali hii ilijitokeza kwa sababu tu viongozi wa ngazi za chini au waliogopa kutoa taarifa, au kuna ambao katika mnyororo huo wa kupeana taarifa walizembea; na mawasiliano na ngazi za juu yakakatika.
Katika kipindi hiki cha habari na mawasiliano, urasimu wa namna hii unapaswa kuwa historia tu. Pamoja na kwamba umbo la serikali linabaki ni lile lile la piramidi, lakini iwapo kila ofisi ya serikali kuanzia juu hadi chini imeunganishwa kimawasiliano na mtandao wa internet, upashanaji wa habari unabadilika na kuchukua umbo kama la uso wa maji.
Ukidondosha kijiwe katikati ya uso wa maji yaliyotuama, mawimbi yanasafiri kutoka hapo kijiwe kilipodondokea na kuelekea pande zote juu ya uso huo wa maji, tena kwa wakati huo huo. Kama ilivyo kwa mawimbi katika uso wa maji, barua pepe moja iliyoanzia kwa mtendaji wa kijiji kimoja, mathalani kule Rukwa, inaweza kumfikia katibu tarafa, mkuu wa wilaya, mkuu wa mkoa, waziri mkuu, na raisi kwa wakati huo huo mmoja. Hii ina maana kwamba kama serikali haikuchukua hatua zinazotakiwa kwa wakati muafaka, tatizo halitakuwa tena ni la urasimu katika kupeana taarifa, ila litakuwa ni kutokana na sababu nyingine, kama uzembe, nakadhalika.
Hebu sasa tuangalie ulimwengu wa kibiashara. Kwa wafanyabiashara walioridhia kuwekeza muda na kujifunza, kipindi hiki cha habari na mawasiliano ni kipindi ambacho kimezaa fursa zisizo na kifani.
Kwa mfano: Kama una bidhaa unauza, na hujui soko liko wapi, unachotakiwa kufanya ni kujisajili tu katika moja ya masoko makubwa ya kwenye mtandao, mathalani Alibaba.com, na kuorodhesha bidhaa ulizonazo nazo. Kwa uhakika kabisa, kabla ya masaa ishirini na nne kupita, utaletewa orodha ndefu ya wafanyabiashara duniani kote na anuani zao, ambao wanatafuta bidhaa unazouza.
Au mathalani, umebuni mradi mzuri lakini kikwazo chako ni mtaji. Kuna mitandao kadhaa ya wawekezaji ambayo ukishajisajili – kuna gharama kidogo unalipia – unaruhusiwa kuwasilisha muhtasari wa business plan yako, yaani muhtasari wa andiko la mradi wako. Wanachama wa mtandao husika watapata fursa ya kupitia muhtasari huo, na wale watakaovutiwa watawasiliana na wasimamizi wa mtandao, ambao nao watakupatia orodha na anuani za wawekezaji hao ili muweze kuwasiliana na kujadiliana. Mwisho wa yote wawekezaji hao watataka walione andiko lote la mradi wako, na kama umeandika kitu cha uhakika, usishangae kukuta unapata watu kutoka Ulaya, Australia, India, Marekani nakadhalika; ambao wako tayari kutoa fedha zao wawekeze kwenye mradi wako kabla hata hamjaonana uso kwa uso!
Hali iko hivyo hivyo kwa wanaotafuta elimu mbalimbali, mafundi wanaokarabati mashine mbalimbali, madaktari wanaohangaika na magonjwa yanayotatiza, watafiti katika fani mbalimbali, nakadhalika.
Kwa mfano: Mwanafunzi anayesomea shahada ya uzamifu hapa kwetu Tanzania anaweza akapata tabu sana kufanya utafiti wa maandiko (literature search) juu ya fani husika, iwapo tegemeo lake pekee ni hizi maktaba zetu. Hii inatokana na ukweli kwamba maktaba zetu zina upungufu mkubwa wa vitabu na majarida ya kitaaluma, kutokana na gharama kubwa ya kuagizia vitu hivyo. Hata hivyo tatizo la mwanafunzi huyu linaweza likamalizika ndani ya muda mfupi sana kwa kutumia mtandao. Kuna maktaba nyingi katika mtandao zilizosheheni kila aina ya vitabu na majarida ya kitaalamu; unachotakiwa tu ni kujisajili na kufumba na kufumbua, nyaraka katika fani unayotafiti zitakuwa mbele yako kwa mamilioni.
Uzuri wa kipindi hiki ni kwamba siyo rahisi tena kudanganya na kuzuia habari kama ilivyokuwa siku za nyuma. Habari inaweza kutokea katika jiji la Mbeya leo asubuhi, na kwa ajili maslahi fulani fulani, ikamuuliwa kwamba taarifa zile zisifikishwe kwa Wananchi kupitia vyombo vya habari vya kawaida yaani Radio, TV na magazeti. Wakati miaka kumi iliyopita uamuzi huu ungekuwa ni wa busara kwa hao wenye kuutoa, leo hii utakuwa ni uamuzi wa kuchekesha. Utaachaje kuwa ni uamuzi wa kuchekesha wakati huenda hata kabla ya kikao kinachotarajiwa kutoa maamuzi ya kuzuia habari husika isitangazwe kuketi, habari hiyo itakuwa tayari imeshasambaa nchi nzima kwa njia ya SMS na barua pepe?
Hivi sasa tuko katika kipindi cha kampeni za uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 31, 2010. Wagombea mbalimbali wa nafasi za udiwani, ubunge na uraisi wameendelea na kujinadi, na katika kujinadi kwao tumesikia mengi. Uzuri wa kipindi hiki cha habari na mawasiliano ni kwamba, ni rahisi kujua yapi kati ya yanayonadiwa na wagombea yanawezekana; na yapi hayawezekani.
Naomba nisieleweke vibaya. Kila kinachonadiwa kinawezekana, lakini kuwezekana kwenyewe kunategemea na mazingira ya eneo husika na wakati unaohusika. Kuna mambo mengi ambayo yanawezekana Ulaya, Marekani, Japan, na katika nchi nyingine zilizoendelea lakini hayawezekani katika mazingira ya Tanzania ya leo. Kwa mfano mgombea akijinadi kuwa mkimchagua ataweka treni ya chini ya ardhi kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro, moja kwa moja unajua kuwa kwa mazingira ya Tanzania ya sasa mgombea huyu ana walakini. Lakini ahadi hiyo hiyo ikitolewa na mgombea aliyeko Ujerumani, Kanada, au nchi nyingine yoyote iliyoendelea, wala watu wa huko hawatapoteza muda wao kujadili; kwa mazingira ya kwao hilo ni jambo la kawaida kabisa; linawezekana.
Miongoni mwa wagombea uraisi ambao wamekuwa wakitoa ahadi ambazo kwa mtizamo wangu zina walakini mkubwa, ni Dr. Slaa wa CHADEMA. Miongoni mwa ahadi hizo ni ile ya kuweka treni ya masaa matatu kutoka Mwanza hadi Dar es Salaam, na ile ya kushusha bei ya saruji hadi shilingi 5,000.00 kwa mfuko wa saruji wa kilo 50.
Tuanze kwanza kuangalia hii ahadi ya treni. Umbali kutokaMwanza hadi Dar es Salaam ni kilometa 1,229. Ili kuwa na treni ya kuweza kusafiri kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza kwa masaa matatu, itailazimu treni hiyo iwe na mwendo kasi wa kilometa 410 kwa saa moja! Hivi sasa treni inayoshikilia rekodi kwa mwendo wa kasi ni ile ya Maglev inayofanya safari zake kati majiji ya Shanghai na Beijing, kule China. Treni hii ina mwendo kasi wa kilometa 431 kwa saa. Treni nyingine maarufu duniani kwa mwendo kasi ni Shinkasen ya Japan, kilometa 260 kwa saa na Eurostar ya Ulaya, kilometa 250 kwa saa!
Katika Tanzania ya leo ahadi ya Dr. Slaa ni kiini macho kwa sababu nchi hii kwa sasa hata uwezo wa kuwapatia Wananchi wake wote milo mitatu kwa siku haina; achilia mbali ukweli kwamba zaidi ya asilimia 40 ya bajeti ya nchi inategemea zaidi wahisani. Sasa kama hao wanaotufadhili wenyewe bado treni hiyo ya mwendo kasi wa kilometa 410 kwa saa hawajawa nayo, sisi tunategemea treni hiyo tuitoe wapi?
Tukija kwenye ahadi ya kuuza mfuko wa saruji kwa shilingi 5,000/- tu, hapa napo inabidi tujiulize: Hivi CHADEMA haina wataalamu wa uchumi, au mgombea wao ndiye asiyeambilika? Katika uzalishaji wa saruji, kuna malighafi muhimu inayoitwa CLINKER. Hivi sasa Tanzania ina uwezo mdogo sana wa kutengeneza malighafi hii; na viwanda vyote vya saruji nchini inabidi kuiagiza kutoka nje ya nchi.
Nchi maarufu kwa uzalishaji na ambayo inaiuza malighafi hii kwa bei rahisi kuliko nchi zote ni China. Katika masoko ya China, kilo 50 ya Clinker inauzwa kiasi cha shilingi 3,902/- kwa sasa. Hii ina maana kuwa pamoja na gharama za usafirishaji hadi katika bandari ya Dar es Salaam, gharama za kuipakua, kuihifadhi, kuitoa, na hatimaye kuisafirisha hadi kiwandani, malighafi hiyo inaweza kufikia gharama ya shilingi 4,500/-; bila hata kulipiwa ushuru wa forodha.
Malighafi hii ikishafika kiwandani inatakiwa sasa ichanganywe na malighafi nyingine zinazopatikana nchini, mathalani 5% - 8% jasi (gypsum), kabla ya kutiwa kwenye mtambo wa kusagia ili kupata saruji yenye ulaini unaotakiwa. Iwapo kilo 50 ya malighafi hizi inafikia shilingi 500/- tu kwa mfano, hii ina maana kuwa hata kabla ya kuinjikwa kwenye mtambo wa kusagia, tayari saruji ghafi yetu imeshatugharimu shingi 5,000/-.
Katika gharama hii ongezea gharama ya nishati inayotumiwa katika mtambo, gharama za kuiweka saruji iliyo tayari kwenye vifungio, gharama za upakiaji na usafirishaji hadi kwa mawakala, na gharama za utawala; ambazo kwa mfano tu, tuseme ni shilingi 500/-. Sasa hata kabla kiwanda hakijaweka faida yake na kulipa kodi yoyote ile ya serikali, tunaona kuwa tayari gharama ya mfuko mmoja ishafika shilingi 5,500/-. Ukiweka faida ya kiwanda ambayo ni asilimia kati ya 7 na 9, utagundua kuwa mfuko mmoja wa saruji kwa mahesabu ya chini kabisa ambayo hayajumuishi kodi yoyote ya serikali ni shilingi 5,940/- kwa bei ya kiwanda. Ongeza na bei ya mawakala wasambazaji wa kiwanda na wauzaji wa jumla na rejareja, utagundua kuwa hata bila kulipiwa kodi yoyote ile, haiwezekani saruji ikauzwa chini shilingi 6,500/- kwa mfuko wa kilo hamsini.
Njia pekee ambayo Dr. Slaa ataweza kutuuzia mfuko wa saruji kwa shilingi 5,000/- ni iwapo tu serikali yake itakuwa inatoa ruzuku kwa wazalishaji wa saruji. Swali linakuja:Ruzuku hiyo itatoka wapi?
Narudia tena: Hiki ni kipindi cha habari na mawasiliano. Ni kipindi kigumu sana kudanganya, na hasa lengo linapokuwa ni kuudanganya umma. Inawezekana CHADEMA haikuwa na nia ya kutudanganya, lakini wanawezaje wakajitetea kuwa wamekuja na ahadi nzito kiasi hicho bila kufanya utafiti? Tangu kampeni hizi zimeanza chama hiki kimefanya makosa mengi mno ya kiufundi na ya wazi, kiasi kwamba mtu unabaki ukiwa umepigwa na bumbuwazi. Ni vipi chama kichanga kiasi hicho kiwe na matumaini ya kupewa ridhaa ya kuongoza nchi? Ushauri wangu kwa CHADEMA ni kwamba viongozi na wagombea wake wawe wanatoa ahadi baada ya kuzifanyia kazi; vinginevo watagundua kuwa Watanzania wanaowadhania ni wajinga, kumbe ni wajanja kuliko wao.
Nimeshindwa kusoma. Ni ndefu sana na Maelezo ni mengi na tangu mwanzo haionekani wataka kusema nini hasa kiasi kwamba imeninyima ladha ya kuisoma.
 
Nimeshindwa kusoma. Ni ndefu sana na Maelezo ni mengi na tangu mwanzo haionekani wataka kusema nini hasa kiasi kwamba imeninyima ladha ya kuisoma.
Mkuu MF
Kama umeshindwa kuisoma yote, nini sababu ya msingi ya kukoti jamvi lote hilo? Si ungeandika tu kwamba umeshindwa kusoma? Kajamvi haka kanakutia uvivu wa kusoma? Vipi umeshamaliza kusoma sera na ilani ya Chadema?
 
Mkuu MF
Kama umeshindwa kuisoma yote, nini sababu ya msingi ya kukoti jamvi lote hilo? Si ungeandika tu kwamba umeshindwa kusoma? Kajamvi haka kanakutia uvivu wa kusoma? Vipi umeshamaliza kusoma sera na ilani ya Chadema?

Mkuu Kibunango, kwa hili niko na Mchukia Fisadi...hii posting inatia kizunguzungu kuisoma. Imenichukuwa muda kupata point iliyokusudiwa. Kusoma Ilani nadhani ni tofauti na kusoma postings za JF, ilani unaweza kuisoma kipengele kimoja kwa siku.
 
Mwenye uvumilivu wa kuusoma mpaka mwisho huo upupu na kukubaliana nao, ampigie kura Kikwete. Sisi tulio na kiu ya maendeleo tutampigia kura Dr. Slaa.
 
Back
Top Bottom