Hivi, CCM tunamtapeli na kumlaghai nani kuhusu kuichukia rushwa uchaguzini?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Kisiasa, unapoisha uchaguzi mmoja maandalizi ya uchaguzi mwingine huanza. Maandalizi ya uchaguzi wa mwaka huu 2020 (kuihusu CCM pekee) yalianza tangu mwaka 2015. Makada walijipanga kutetea majimbo na kata na wengine wakitamani kuzipoka kata na majimbo kutoka kwa wasasa. Maandalizi ya kiuchaguzi hayakufanyika kwa wapinzani tu. Wao waliminywa vya kutosha na kutisha na kulazimishwa kufanya mambo yao ya kisiasa kimyakimya na sirini kama kuuza gongo, bangi au ngada.

Makada wa CCM, kabla ya maigizo yaliyoanzishwa jana ya kutoa namba ya simu ya kuripoti vitendo vya rushwa, walishatoa rushwa na kujijenga ipasavyo. Tazama ayafanyayo Naibu Spika Dr. Tulia kule Mbeya. Amekuwa akijibanza kwenye taasisi yake ya Tulia Trust kugawa rushwa na kusaka ushawishi ili aweze kugombea na kushinda jimbo la Mbeya Mjini linaloshikiliwa na CHADEMA. Mtazame Silvestry Koka wa Kibaha Mjini. Ameshagawa baiskeli na pikipiki kwa makada wa CCM tayari kutaka kuutetea ubunge wake. Majimbo yote hali ipo hivyo, wataripotiwa wangapi? Watafanywaje?

Rushwa, as always, imeota mizizi na kutamalaki ndani ya CCM. Rushwa ndiyo inayowapa ushindi makada ndani ya CCM na hata kwenye uchaguzi mkuu. Rushwa ni njia pekee ya kuibuka kidedea huku ukichekelea ndani ya CCM. Mafao ya Ubunge mara baada ya kuvunjwa kwa Bunge ndiyo hutumika kugawa mahela kwa makada na wananchi na kuwawezesha watu kutetea viti vyao. Ni vichekesho, utapeli na ulaghai kusema kuwa CCM inachukia rushwa. Sisi wanaCCM tunajua ukweli huo. Hakuna haja ya kudanganyana.

Kazi ya kupambana na kuzuia rushwa ni ya TAKUKURU. Lakini, wakati kama huu wa uchaguzi, CCM ndiyo huwakingia vifua makada wake wanaotiwa mbaroni kwa rushwa na kuwaharibia kazi TAKUKURU. Inashangaza kutapeli na kulaghai wananchi kuwa chama chetu cha CCM kinachukia na kupambana na rushwa. Ni ajabu inayofaa kuingia kwenye kitabu cha maajabu ya kidunia.Wananchi wamekosa nini hadi wadanganywe na kulaghaiwa kiasi hiki? Kinaendelea nini kwenye kukamatwa kwa Rage kule Tabora?

Uchaguzi ndani ya CCM bila rushwa hauwezekani!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Nzega, Tabora)
 
Kisiasa, unapoisha uchaguzi mmoja maandalizi ya uchaguzi mwingine huanza. Maandalizi ya uchaguzi wa mwaka huu 2020 (kuihusu CCM pekee) yalianza tangu mwaka 2015. Makada walijipanga kutetea majimbo na kata na wengine wakitamani kuzipoka kata na majimbo kutoka kwa wasasa. Maandalizi ya kiuchaguzi hayakufanyika kwa wapinzani tu. Wao waliminywa vya kutosha na kutisha na kulazimishwa kufanya mambo yao ya kisiasa kimyakimya na sirini kama kuuza gongo, bangi au ngada.

Makada wa CCM, kabla ya maigizo yaliyoanzishwa jana ya kutoa namba ya simu ya kuripoti vitendo vya rushwa, walishatoa rushwa na kujijenga ipasavyo. Tazama ayafanyayo Naibu Spika Dr. Tulia kule Mbeya. Amekuwa akijibanza kwenye taasisi yake ya Tulia Trust kugawa rushwa na kusaka ushawishi ili aweze kugombea na kushinda jimbo la Mbeya Mjini linaloshikiliwa na CHADEMA. Mtazame Silvestry Koka wa Kibaha Mjini. Ameshagawa baiskeli na pikipiki kwa makada wa CCM tayari kutaka kuutetea ubunge wake. Majimbo yote hali ipo hivyo, wataripotiwa wangapi? Watafanywaje?

Rushwa, as always, imeota mizizi na kutamalaki ndani ya CCM. Rushwa ndiyo inayowapa ushindi makada ndani ya CCM na hata kwenye uchaguzi mkuu. Rushwa ni njia pekee ya kuibuka kidedea huku ukichekelea ndani ya CCM. Mafao ya Ubunge mara baada ya kuvunjwa kwa Bunge ndiyo hutumika kugawa mahela kwa makada na wananchi na kuwawezesha watu kutetea viti vyao. Ni vichekesho, utapeli na ulaghai kusema kuwa CCM inachukia rushwa. Sisi wanaCCM tunajua ukweli huo. Hakuna haja ya kudanganyana.

Kazi ya kupambana na kuzuia rushwa ni ya TAKUKURU. Lakini, wakati kama huu wa uchaguzi, CCM ndiyo huwakingia vifua makada wake wanaotiwa mbaroni kwa rushwa na kuwaharibia kazi TAKUKURU. Inashangaza kutapeli na kulaghai wananchi kuwa chama chetu cha CCM kinachukia na kupambana na rushwa. Ni ajabu inayofaa kuingia kwenye kitabu cha maajabu ya kidunia.Wananchi wamekosa nini hadi wadanganywe na kulaghaiwa kiasi hiki? Kinaendelea nini kwenye kukamatwa kwa Rage kule Tabora?

Uchaguzi ndani ya CCM bila rushwa hauwezekani!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Nzega, Tabora)
Hao wanaotoa rushwa wanapoteza bure fedha zao

Wagombea wateule wa CCM wameshafanyiwa vetting na orodha ipo CC ya chama.
Wapo baadhi ya watu wataombwa na chama wagombee ubunge kutokana na umuhimu wao.
Wabunge wa sasa ni wachache sana watarudi hawafiki 20%

Bunge lijalo litaitwa bunge la maendeleo..... na Spika hatatokana miongoni mwa wabunge.

Dr Tulia ataendelea na unaibu spika.

Maendeleo hayana vyama!
 
Hao wanaotoa rushwa wanapoteza bure fedha zao

Wagombea wateule wa CCM wameshafanyiwa vetting na orodha ipo CC ya chama.
Wapo baadhi ya watu wataombwa na chama wagombee ubunge kutokana na umuhimu wao.
Wabunge wa sasa ni wachache sana watarudi hawafiki 20%

Bunge lijalo litaitwa bunge la maendeleo..... na Spika hatatokana miongoni mwa wabunge.

Dr Tulia ataendelea na unaibu spika.

Maendeleo hayana vyama!
I see
 
Hao wanaotoa rushwa wanapoteza bure fedha zao

Wagombea wateule wa CCM wameshafanyiwa vetting na orodha ipo CC ya chama.
Wapo baadhi ya watu wataombwa na chama wagombee ubunge kutokana na umuhimu wao.
Wabunge wa sasa ni wachache sana watarudi hawafiki 20%

Bunge lijalo litaitwa bunge la maendeleo..... na Spika hatatokana miongoni mwa wabunge.

Dr Tulia ataendelea na unaibu spika.

Maendeleo hayana vyama!
Tuondelee propaganda hapa.

Article 84 (1) URT Constitution requires; A speaker shall be elected from persons who are members of parliment, or who are qualified to be members of parliament.

Sasa huyo wa kwenu mtamtoa wapi?!
 
Hao wanaotoa rushwa wanapoteza bure fedha zao

Wagombea wateule wa CCM wameshafanyiwa vetting na orodha ipo CC ya chama.
Wapo baadhi ya watu wataombwa na chama wagombee ubunge kutokana na umuhimu wao.
Wabunge wa sasa ni wachache sana watarudi hawafiki 20%

Bunge lijalo litaitwa bunge la maendeleo..... na Spika hatatokana miongoni mwa wabunge.

Dr Tulia ataendelea na unaibu spika.

Maendeleo hayana vyama!

Litaitwa bunge la maendeleo ili kuhadaa umma, lakini lengo hasa litakuwa ni kumuongezea Magufuli muda wa kukaa madarakani zaidi ya 10yrs.
 
Tuondelee propaganda hapa.

Article 84 (1) URT Constitution requires; A speaker shall be elected from persons who are members of parliment, or who are qualified to be members of parliament.
Rushwa ziko Ufipa kwa akina Maselle!

Sasa unachobisha nini hapo kwa Spika?........ su lugha ya kisheria imekutatiza bwashee?
 
Rushwa ziko Ufipa kwa akina Maselle!

Sasa unachobisha nini hapo kwa Spika?........ su lugha ya kisheria imekutatiza bwashee?
Ulivyosema Spika hatatokana miongoni mwa wabunge unamaanisha hata wabunge wa kuteuliwa, coz nao ni wabunge pia, sijui kama unafahamu hilo?!
 
Kisiasa, unapoisha uchaguzi mmoja maandalizi ya uchaguzi mwingine huanza. Maandalizi ya uchaguzi wa mwaka huu 2020 (kuihusu CCM pekee) yalianza tangu mwaka 2015. Makada walijipanga kutetea majimbo na kata na wengine wakitamani kuzipoka kata na majimbo kutoka kwa wasasa. Maandalizi ya kiuchaguzi hayakufanyika kwa wapinzani tu. Wao waliminywa vya kutosha na kutisha na kulazimishwa kufanya mambo yao ya kisiasa kimyakimya na sirini kama kuuza gongo, bangi au ngada.

Makada wa CCM, kabla ya maigizo yaliyoanzishwa jana ya kutoa namba ya simu ya kuripoti vitendo vya rushwa, walishatoa rushwa na kujijenga ipasavyo. Tazama ayafanyayo Naibu Spika Dr. Tulia kule Mbeya. Amekuwa akijibanza kwenye taasisi yake ya Tulia Trust kugawa rushwa na kusaka ushawishi ili aweze kugombea na kushinda jimbo la Mbeya Mjini linaloshikiliwa na CHADEMA. Mtazame Silvestry Koka wa Kibaha Mjini. Ameshagawa baiskeli na pikipiki kwa makada wa CCM tayari kutaka kuutetea ubunge wake. Majimbo yote hali ipo hivyo, wataripotiwa wangapi? Watafanywaje?

Rushwa, as always, imeota mizizi na kutamalaki ndani ya CCM. Rushwa ndiyo inayowapa ushindi makada ndani ya CCM na hata kwenye uchaguzi mkuu. Rushwa ni njia pekee ya kuibuka kidedea huku ukichekelea ndani ya CCM. Mafao ya Ubunge mara baada ya kuvunjwa kwa Bunge ndiyo hutumika kugawa mahela kwa makada na wananchi na kuwawezesha watu kutetea viti vyao. Ni vichekesho, utapeli na ulaghai kusema kuwa CCM inachukia rushwa. Sisi wanaCCM tunajua ukweli huo. Hakuna haja ya kudanganyana.

Kazi ya kupambana na kuzuia rushwa ni ya TAKUKURU. Lakini, wakati kama huu wa uchaguzi, CCM ndiyo huwakingia vifua makada wake wanaotiwa mbaroni kwa rushwa na kuwaharibia kazi TAKUKURU. Inashangaza kutapeli na kulaghai wananchi kuwa chama chetu cha CCM kinachukia na kupambana na rushwa. Ni ajabu inayofaa kuingia kwenye kitabu cha maajabu ya kidunia.Wananchi wamekosa nini hadi wadanganywe na kulaghaiwa kiasi hiki? Kinaendelea nini kwenye kukamatwa kwa Rage kule Tabora?

Uchaguzi ndani ya CCM bila rushwa hauwezekani!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Nzega, Tabora)
Hii Mambo ya kuhonga ili utetee kiti na madaraka ilimgharimu sana ndugu Richard Nixon Miaka ya 1970s kwenye issue ya Watergate scandal Hadi kwa aibu akajiuzulu ... Ilibaki kidogo apigwe ndani we sema rais aliyefuata alimwifadhi tu
 
Ulivyosema Spika hatatokana miongoni mwa wabunge unamaanisha hata wabunge wa kuteuliwa, coz nao ni wabunge pia, sijui kama unafahamu hilo?!
Hata wewe kama una sifa za kibunge yaani unajua kusoma na kuandika unaruhusiwa kugombea Uspika bwashee siyo lazima uwe mbunge!

Naibu Spika ndio lazima awe mbunge.
 
Kisiasa, unapoisha uchaguzi mmoja maandalizi ya uchaguzi mwingine huanza. Maandalizi ya uchaguzi wa mwaka huu 2020 (kuihusu CCM pekee) yalianza tangu mwaka 2015. Makada walijipanga kutetea majimbo na kata na wengine wakitamani kuzipoka kata na majimbo kutoka kwa wasasa. Maandalizi ya kiuchaguzi hayakufanyika kwa wapinzani tu. Wao waliminywa vya kutosha na kutisha na kulazimishwa kufanya mambo yao ya kisiasa kimyakimya na sirini kama kuuza gongo, bangi au ngada.

Makada wa CCM, kabla ya maigizo yaliyoanzishwa jana ya kutoa namba ya simu ya kuripoti vitendo vya rushwa, walishatoa rushwa na kujijenga ipasavyo. Tazama ayafanyayo Naibu Spika Dr. Tulia kule Mbeya. Amekuwa akijibanza kwenye taasisi yake ya Tulia Trust kugawa rushwa na kusaka ushawishi ili aweze kugombea na kushinda jimbo la Mbeya Mjini linaloshikiliwa na CHADEMA. Mtazame Silvestry Koka wa Kibaha Mjini. Ameshagawa baiskeli na pikipiki kwa makada wa CCM tayari kutaka kuutetea ubunge wake. Majimbo yote hali ipo hivyo, wataripotiwa wangapi? Watafanywaje?

Rushwa, as always, imeota mizizi na kutamalaki ndani ya CCM. Rushwa ndiyo inayowapa ushindi makada ndani ya CCM na hata kwenye uchaguzi mkuu. Rushwa ni njia pekee ya kuibuka kidedea huku ukichekelea ndani ya CCM. Mafao ya Ubunge mara baada ya kuvunjwa kwa Bunge ndiyo hutumika kugawa mahela kwa makada na wananchi na kuwawezesha watu kutetea viti vyao. Ni vichekesho, utapeli na ulaghai kusema kuwa CCM inachukia rushwa. Sisi wanaCCM tunajua ukweli huo. Hakuna haja ya kudanganyana.

Kazi ya kupambana na kuzuia rushwa ni ya TAKUKURU. Lakini, wakati kama huu wa uchaguzi, CCM ndiyo huwakingia vifua makada wake wanaotiwa mbaroni kwa rushwa na kuwaharibia kazi TAKUKURU. Inashangaza kutapeli na kulaghai wananchi kuwa chama chetu cha CCM kinachukia na kupambana na rushwa. Ni ajabu inayofaa kuingia kwenye kitabu cha maajabu ya kidunia.Wananchi wamekosa nini hadi wadanganywe na kulaghaiwa kiasi hiki? Kinaendelea nini kwenye kukamatwa kwa Rage kule Tabora?

Uchaguzi ndani ya CCM bila rushwa hauwezekani!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Nzega, Tabora)
Kwa kadri ya kumbukumbu zangu hakuna mwanaccm aliyegawa rushwa kama Tulia Ackson , hizi porojo za Polepole zimeshangaza wengi sana !
 
Tuondelee propaganda hapa.

Article 84 (1) URT Constitution requires; A speaker shall be elected from persons who are members of parliment, or who are qualified to be members of parliament.

Sasa huyo wa kwenu mtamtoa wapi?!
Hakuwa anafahamu.
 
Ulivyosema Spika hatatokana miongoni mwa wabunge unamaanisha hata wabunge wa kuteuliwa, coz nao ni wabunge pia, sijui kama unafahamu hilo?!
Spika si lazima awe mbunge, anatakiwa awe na sifa kwa mujibu wa Katiba, ila Naibu wake ndiyo anapaswa kuwa mbunge, awe wa kuchaguliwa au kuteuliwa.
 
Hii Mambo ya kuhonga ili utetee kiti na madaraka ilimgharimu sana ndugu Richard Nixon Miaka ya 1970s kwenye issue ya Watergate scandal Hadi kwa aibu akajiuzulu ... Ilibaki kidogo apigwe ndani we sema rais aliyefuata alimwifadhi tu
Umeisoma wapi hii mkuu, au ni utafiti mpya ulioufanya na kugundua sababu hii ndio iliyosababisha aondolewe madarakani?

Kama wewe ni mwalimu unawalisha ndimu vijana nao wanakuwa na elimu potofu kama uliyonayo wewe.

Haya ndio matatizo yanayoiandama Tanzania kwa kasi sasa, maanake serikali yenyewe ndio kimekuwa kiwanda cha kusema uongo.

Sasa hata wananchi wenyewe tunawaunga mkono kwa kusema uongo.
 
Back
Top Bottom