Hivi CCM nani ni msafi kama hata Jangwani ilisha uzwa ?

Chifu Ihunyo

Member
Jul 3, 2006
63
10
Jangwani nayo imebinafsishwa

Mikwara yote ya kusafisha eneo la Jangwani kuwaokoa walio mabondeni na mafuriko ya mara kwa mara kumbe ni danganya toto.

Eneo hilo linadaiwa kuwa tayari lina magabacholi wanne waliolinasa tangu mwaka 2004 tangu enzi za Mzee wa Jiji Yusufu Makamba.

Serikali ya Mkuu mpya wa Dar, Abbas Kandoro baada ya kumalizana na hali ya uwanja wa fisi kwa kuwatimua wenye gesti, na vichagudoa vidogo (kiumri), ilihamia bonde la Jangwani na kubomoa nyumba kibao za wakazi wa mitaa hiyo.



Sasa imeibuka kuwa serikali imeshasukuma viwanja hivyo kwa
wafanyabiashara wenye nazo tangu mwaka 2004 na imekuwa ikitafuta kisingizio cha mafuriko kama chanzo cha kuwatimua waliojenga maeneo hayo.

Mwenyekiti wa mtaa wa Jangwani Mohamed Bendera amekiri kuwepo kwa kimbembe hicho pamoja na kulalamika kuwa kesi yao ya kupinga kutimuliwa eneo hilo bado iko Mahakama Kuu na haijamalizika.

Baadhi ya wanaodaiwa kuhusishwa na sakata la uuzaji wa eneo hilo ni pamoja na Katibu wa sasa wa CCM, Yusufu Makamba na Spika wa Bunge Samuel Sitta akiwa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji.

Hadi sasa nyumba 70 zimeshapigwa tindo huku wakazi wa eneo hilo wakilalamikia uonevu huo wakidai kuwa walipatiwa eneo hilo na aliyekuwa Rais wa kwanza J. K Nyerere mwaka 1974 na kuwapatia huduma safi ya visima vya maji.wengine.
 
Chifu , hapa kuna wana CCM kama Mzee Es hebu mwache atueleze habari za Chama chake .
 
Nimewasikia wazee ninaamini kinachofanyika hapo Jangwani ni sawa kabisa na mambo yanayofanyika huko majuu, si tunasikia kuwa wazungu wakitaka kujenga malls, huwa wanahamisha wananchi na kuwalipa?

Jangwani hapana tofauti yoyote na mahali palipokuwa Drive-In cinema, ambako sasa umejengwa ubalozi wa US na kuliletea taifa ajira ya karibu wananchi 5,000, na mapesa mengi sana kwa serikali kwa njia mbali mbali, sheria inasema ardhi yetu ni mali ya serikali, sasa kama serikali inaona kuna umuhimu wa kuitumia ardhi yoyote for the good of the people, basi ina wajibu wa kutekeleza bila ya kusita, inapopita reli ya TAZARA yalifanyika hayo hayo wananchi walibomolewa nyumba wakalipwa tukasikia kelele na vilio, lakini leo reli yetu imara inaendelea na kuliletea taifa letu mambo mengi muhimu kwa wananchi wengi kuliko wale wachache waliokuwa wanakaa pale,

Now after that, kama kuna deal ambazo zimefanywa huko Jangwani bila ya kupitia njia maalumu zilizowekwa na serikali za kisheria, hilo ni tatizo la viongozi wezi na sio CCM kama chama, mbunge wa upinzani alipokatiwa mpango wake kwenye issue ya bunge ya Kitine sio kwamba chama kizima cha Chadema kilikuwa kinahusika, hapana alikuwa ni yeye tu Kaburu, na Mzee Mapesa sio mara moja au mbili amehusika na kukatiwa mpango, sasa huwezi kulaumu UDP yote, HAPANA,

Siwatetei viongozi wabovu hapana, ila kuilaumu CCM yote kwa makosa ya viongozi wawili kama kweli wamefanya unayoyasema, ni lugha nzito kidogo katika siasa. Lakini serikali yoyote duniani kisheria ina haki ya kuchukua ardhi yoyote ile iliyoko katika nchi ile for the good of the peole at large,

ni RUKHSA kisheria!
 
Mzee ES,

Bravo, umenena hapa kuhusu Kaburu, nina uhakika hata CCM hawamuhitaji kabisa maana aliyoyafanya yalikuwa ya kusikitisha kwa maadili ya uongozi uliotukuka, sifikiri JK anahitaji mtu kama huyu? CCM in vijana safi saana wanaoweza kusukuma gurudumu mbele na si huyu.
 
Yombayomba CCM ama JK kama wanaweza kuwa na watu kama Masha , Kirimagi , Kapuya nk na wako karibu a JK nini Kaburu ?
 
Mzee Es nakubaliana na hoja yako ya kuwhamisha watu na kuwalipa nakuwaeleza ukweli kwa nini mambo yanatokea namna ile .Je wamepwa taarifa za uwazi ? Au Makamba alitumia vitisho kuwaondoa kijanja ? hayakuanza jana ni muda sasa je kwa nini msiwaambie ukweli wananchi wakajua kama ianavyotakiwa ?
 
Mzee Makamba amezidi kwa kamba, hivi kiwanja cha BAKWATA kule chang'ombe kiliishia wapi?
 
Wazee wangu nimewasikia,

Ninaomba tukubaliane kuwa kama mnayosema ni ya kweli basi tatizo ni lile lile la viongozi wabovu na utekelezaji,

yes kisheria, Wanachi wanatakiwa kutangaziwa kwanza, baadaye kufanyika kikao cha public na serikali, ambapo wananchi wanatoa maoni yao na serikali inatoa yake, baadaye kamati independent ambayo inayafuatilia kwa makini malumbano ya serikali na wananchi wa eneo hilo, inakaa chini na kutoa ripoti yao ambayo ndiyo inakuwa the final, na ikibidi kunafanyika kikao kingine cha dharura tena baina ya wananchi na serikali,

sasa kama haya hayakufanywa, then kweli kuna tatizo lakini sio la CCM nzima, hapana ni viongozi wanaohusika tu,

Halafu ngoja niongeze, ninasema kwamba JK, anaweza kuwa na matatizo fulani kiuongozi sawa na yeye ni binadamu kama sisi wengine na mapungufu yetu, lakini ninataka ndugu zangu niwaambie kitu kimoja, kuhusu nidhamu kwa viongozi siadhani kama ana mchezo nalo, nimemuona kwa macho yangu akimuwashia Mzee Nchimbi na Masha, wakati alipowaita mtandao mmoja baada ya mwingine kwa wakati mbali mbali, nimemsikia akimuambia Nchimbi kuwa "......Wewe nasikia unalalamika huko mitaani kuwa sikukupa uwaziri, ukifanya mchezo nitakutoa hata huo unaibu, nataka kazi..........", sasa hamuwezi kuniambia kuwa huyu rais anataka mchezo,

leo mawaziri wote wamenywea kama wamelowa mvua, kwa hiyo ndio bado CCM tuna matatizo ya uongozi, lakini so is upinzani!
 
ardhi ni ya serikali !!

acheni ccm wauze ardhi yenye gesi na madini kwa wawekezaji kwa niaba ya wananchi...

ccm oye!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom