Regia Mtema
R I P
- Nov 21, 2009
- 2,970
- 863
Ni ukweli usiopingika kwamba miaka ya hivi karibuni (Miaka 40 iliyopita) Waafrika tulikuwa na desturi ya kukuagua bikira kwa mabinti ama wasichana waliokuwa wakiolewa.Siku ya harusi ilikuwa ni lazima Bwana na Bibi harusi wafanye tendo la ndoa hata kama walikuwa hawajisikii kufanya hivyo,na tendo hili halikuwa siri kwani ilikuwa ni lazima shuka jeupe litandikwe ili kuona kama kuna bikira kwa mwanamke na kama damu haikuonekana kwenye shuka basi binti alionekana kwamba hafai na alichwa kabisa bila huruma tena kwa maneno makali.Ilkuwa ni aibu kubwa binti kukutwa hana bikira lakini utamaduni huu kwa miaka ya sasa hakuna kabisa.
Swali langu kwani bikira ina faida gani mpaka wazee wetu walikuwa hawana utu kiasi hiki?na je kwanini bikira kwa binti tu vipi kwa mwanaume?
Swali langu kwani bikira ina faida gani mpaka wazee wetu walikuwa hawana utu kiasi hiki?na je kwanini bikira kwa binti tu vipi kwa mwanaume?