Hivi bado Watanzania tunajidanganya mfumo wa siasa uliopo utadumisha amani na umoja wa kitaifa?

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,142
18,769
Amani na umoja wa Watanzania, ni sifa ambayo ilijulikana juu ya Watanzania duniani kote. Kwa miaka mingi sana Tanzania ilikuwa haitajwi na vyombo vya habari kama BBC na CNN kwa kuwa hatukuwa na habarai mbaya ambazo vyombo vya magharibi hupenda kuzitangaza juu ya nchi zinazoendelea na masikini. Tanzania wakati fulani ilikuwa ndio kisiwa cha kukimbilia wananchi wa nchi jirani wanapokuwa na matatizo.

Lakini mambo yalianza kubadilika taratibu, na katika awamu hii ya tano chini ya Raisi Magufuli, tumefikia hatua mbaya ambayo hatujawahi kufikia katika historia yote ya siasa za Tanzania. Kwa sababu za kisiasa, watu wanatekwa, wanauwawa, ofisi za serikali na vyama zinachomwa moto, chuki kati ya watanzaia ambao tullitana ndugu huko nyuma inazidi kukua kwa sababu tu za ufuasi tofauti wa vyama, hata tumefikia kuitana "adui" na sio ndugu tena!

Tunakwenda wapi?

Hivi kweli, iwe wewe ni mfuasi wa CCM, au chama cha upinzani, unaona yanayotokea Tanzania ni sehemu tu ya ushindani wa kiasiasa? Ni wendawazimu na ulevi gani umetuingia hadi tumefikia kuruhusu wajinga wachache waamue kuharibu uhusiano na undugu na umoja wetu kwa sababu tu za uchu wao wa madaraka na kujiona wao ndio wanajua kuliko sisi wengine wote?

Watanzania tufike mahali tujiulize, tunataka kufikia mahali tuwe na vurugu ndani ya nchi kati yetu wenyewe kama ilivyokuwa DRC? Zimbabwe? South Sudan? Rwanda? Burundi? Hivi tunataka kuonja machungu ya kuvunjika kwa amani kati yetu weyewe, tumekinai amani yetu kiasi hicho?

Natoa wito kwa Watanzania wote, uwe CCM au vyama vya upinzani, wakati wa kuvumilia kutenganishwa umekwisha, na sasa tukatae kugawanywa na watu wachache ambao wanajifanya wapo kwa maslahi yetu kumbe wanataka tu kututumia. Kama ikibidi, tufikie mahali tuwakane hawa wanasiasa wote, iwe CCM, iwe vyama vya upinzani, na kuonyesha kwamba tunataka kuanza upya katika misingi ambayo inatuweka pamoja kama Watanzania bila kujali huu ushabiki wa kitoto wa kisiasa uliopo sasa, ambao hatima yake huko mbele ni mbaya tu. Tufikirie sana tunaandaa mazingira ya namna gani wa ajili ya watoto wetu. Tuachane na ushabiki wa kisiasa wa kilevi tu kama watu tusio na akili timamu.

Ifikie mahali tuone kwamba mfumo wa kisiasa uliopo sasa umefeli, si upande wa CCM, si upande wa upinzani, na sasa tunataka kuwa na mwanzo mpya wa mfumo wa kisiasa hapa nchini ambao utatuunganisha kama ndugu badala ya kututenganisha na kutugombanisha. Kama ikibidi kuviua CCM na vyama vingine vyote vilivyopo ili tuanza upya, basi acha hilo litokee. Tukubali ukweli kwamba kama nchi yetu kwa miaka mingi imeshindwa kuendelea kwa kuwa ilifunikwa na ufisadi wa kutisha - hao ni CCM waliosababisha, na bado tunafikiri leo watabadilika? Na kama CCM waliendelea kutawala nchi kwa kifisadi bila bugudha, basi vyama vya upinzani navyo vimeshindwa katika kuidhibiti CCM na kuhakikisha Tanzania inaongozwa kwa misingi ya utawala bora. Upinzani ifikie wakati wakiri kushindwa, na CCM wakiri kuwa wao ndio wameharibu nchi yetu.

Tusiwaone watu hawa kama wakombozi, wote wana damu ile ile ya ufisadi, ya kutudangnaya, ya kutugombanisha, ya kushindwa kutuletea maendelea, ya kushindwa kuwasaidia watanzania wengi wanaokosa huduma za msingi za afya, maji, elimu nk. Wote wamefeli vibaya. Wamepimwa na hawafai. Wote wanajifanya wana akili kutuzidi watanzania tusio viongozi.

Tuamke!!!!
 
Demokrasia ina mipaka yake

Tusiharibu Tunu za Taifa letu kwa kisingizio cha demokrasia

Hata kwa Mabeberu wana mipaka ya demokrasia tusidanganyane
 
IMG_20191004_103744.jpg
 
Yaani CCM imevuruga uchaguzi unatuambia tuwakane na waliodhurumiwa?

Bandiko lako lina hila! Chama tawala na "vyombo" vyake ndivyo vnataka kutuchimbia kaburi!

Kuongea kwa ujumla tu ni kulifumbia macho tatizo
 
Demokrasia ina mipaka yake

Tusiharibu Tunu za Taifa letu kwa kisingizio cha demokrasia

Hata kwa Mabeberu wana mipaka ya demokrasia tusidanganyane
yes Tunu za taifa ni pamoja na kuwaita watendaji ikulu na kuwaamrisha waharibu form za wagombea wa upinzani.
 
yes Tunu za taifa ni pamoja na kuwaita watendaji ikulu na kuwaamrisha waharibu form za wagombea wa upinzani.
Mkuu Daudi, tumefikia hatua mbaya sana, na katika hii vita ya mfumo wa kisiasa hakuwezi kutokea mshindi na wala CCM wasijione wao ni washindi kwa sasa. CCM wanapaswa kuelewa kwamba kadiri unavyoendelea kumfanya mtu mwingine mnyonge wako, siku zote atakuwa anapanga namna ya kubadilisha status quo na kukulipizia kisasi, na iko siku atakuja na namna ya kukuumiza tu. Na siku akikushinda atakundamiza haswa, then we start all over again.

Nakumbuka hii philosophy mwaka 1948 Israel na Waarabu walipolazimishwa kugawana lile eneo. Waarabu mwanzoni walikuwa wanawanyanyasa sana Israel ambae wakati huo alionekana mnyonge sana. Lakini sasa uonevu wa Waarabu kwa Israel ndio uliomfanya Israel ajenge nguvu, na hatimaye kuweza kuwageuzia kibao Waarabu. Hadi leo kuwasuluhisha hawa wawili wakae kwa amani ni tatizo kubwa. Ndivyo ilivyo kwa CCM na upinzania kwa sasa. Labda siku moja upinzani utakuwa na nguvu ya kutosha ya kushinda, lakini bado Tanzania kama Taifa tutakuwa na tatizo lilelile tulilonalo sasa, la upande mmoja kumkandamiza mwingine.
 
Yaani CCM imevuruga uchaguzi unatuambia tuwakane na waliodhurumiwa?

Bandiko lako lina hila! Chama tawala na "vyombo" vyake ndivyo vnataka kutuchimbia kaburi!

Kuongea kwa ujumla tu ni kulifumbia macho tatizo
Hapana Mkuu. Nafikiria kwa mbali zaidi. Huu uhasama hauwezi kwisha kwa upinzani kushinda. Leo hii Chadema wakishinda na CCM kuwa mpinzani, kwa upande wa Tanzania kama Taifa hakuna atakaekuwa ameshinda. Tutarudi kule kule kwenye mazingira ambapo CCM walikandamiza upinzani.

Ona watu kama kina Mwita Waitara, Mtatiro. Walikuwa upinzani, wakaingia CCM. Utadhani wao ndio wangekuwa na busara zaidi wakijua ubaya wa kundamiza wanasiasa wenzao, lakini wapi.

Kwa hiyo tatizo ni misingi inayounda mfumo wa vyama vilivyopo - misingi ya kuwaona walioko chama kingine ni maadui. Hilo ndio tatizo. Na kamwe usidhani wapinzani wao ni malaika kwa kuwa tu kwa sasa wao ndio wanakandamizwa. Na nitakuwa mtu wa kwanza kukiri kwa sasa wapinzani wanakandamizwa na kunyanyaswa sana na CCM, na hata wanauwawa. Lakini unafikiri siku wapinzani wakichukua nchi tutakuwa tumemaliza tatizo la wanasiasa wa upinzani kukandamizwa na hata kuuwawa? Be frank and tell me.

Tunatakiwa tuanze upya.
 
Hapana Mkuu. Nafikiria kwa mbali zaidi. Huu uhasama hauwezi kwisha kwa upinzani kushinda. Leo hii Chadema wakishinda na CCM kuwa mpinzani, kwa upande wa Tanzania kama Taifa hakuna atakaekuwa ameshinda. Tutarudi kule kule kwenye mazingira ambapo CCM walikandamiza upinzani.

Ona watu kama kina Mwita Waitara, Mtatiro. Walikuwa upinzani, wakaingia CCM. Utadhani wao ndio wangekuwa na busara zaidi wakijua ubaya wa kundamiza wanasiasa wenzao, lakini wapi.

Kwa hiyo tatizo ni misingi inayounda mfumo wa vyama vilivyopo - misingi ya kuwaona walioko chama kingine ni maadui. Hilo ndio tatizo. Na kamwe usidhani wapinzani wao ni malaika kwa kuwa tu kwa sasa wao ndio wanakandamizwa. Na nitakuwa mtu wa kwanza kukiri kwa sasa wapinzani wanakandamizwa na kunyanyaswa sana na CCM, na hata wanauwawa. Lakini unafikiri siku wapinzani wakichukua nchi tutakuwa tumemaliza tatizo la wanasiasa wa upinzani kukandamizwa na hata kuuwawa? Be frank and tell me.

Tunatakiwa tuanze upya.
Bado haiko sawa! CHDEMA hawajawahi shinda!!

Moja ya mazuri ya vyama kupishana na kuachiana ni kufundisha! CCM inatakiwa ikae kando ijifunze ubaya na taabu ya kuwa mpinzani, warekebishe makosa yao.

Wapinzani wakishinda watakuwa na uchungu wa kutaabika watajitahidi kutofanya makosa ili waendelee!

Kimsingi wote wanatakiwa kuongoza kwa adabu, kwakuwa watajua wakikosea hawachaguliwi tena!

CCM wanawajibika kwa taabu zetu, hawewezj kukwepa
 
Back
Top Bottom