Zero Hours
JF-Expert Member
- Apr 1, 2011
- 12,948
- 18,648
Mara ya Mwisho mimi kusikia kijana au kiongozi yeyote wa CCM kuihoji au kukosoa serikali ilikuwa ni mwaka Juzi. Na hiki kitendo kilifanywa na Mbunge Bashe kabla hajapewa unaibu waziri akituhumu kuwa kwenye list ya wanaotaftwa na wasiojulikana sababu ya kukosoa serikali. Baada ya yeye kuingia kwenye system ( ya kutokuongea ukiwa unakula) na yeye kawa muimba nyimbo za sifa na Utukufu.
Mifano ipo mingi sana ya namna hii ukiangalia apo nyuma hasa awamu ya JK. Vijana wengi walihoji na kukosoa mwenendo wa serikali yao. Wengi walihoji hasa juuu ya Ufisadi na Matumizi mabaya ya kodi za watanzania.
Cha kushangaza, baada ya hawa vijana Type ya " Polepole" kuingia kwnye system na wao wakafyata mkia.
Sasa swali ni hili.
Hivi Baba wetu wa taifa angekuwa kama hawa vijana wa sasa wa CCM ( kigogo anawaita MATAGA), je Tungepata uhuru au Tungepataje uhuru?
Mnafikiri mabeberu hawakutafta njia tofauti za kumdhuru au kumhonga Nyerere ili aache chokochoko za kupigania uhuru? Kumbuka Baba yetu wa Taifa alisomeshwa na hawa Mabeberu mpaka wakamfadhili na kumsomesha chuo cha Edinburgh nchini Uingereza ( 1952) lakini hakuwa mnafiki alipigani uhuru wa Watanganyika na kuhakikisha wanatuachia nchi yetu.
Ukiangalia hata mandela naye ivyo ivyo. Alikuwa mwanasheria na maisha mazuri tu ila alipigania uhuru wa nchi yake ingawa aliteswa sana na Mabeberu.
Uzalendo wa Baba yetu wa Taifa ndyo uliotufanya tupate uhuru. Ila Tafsiri ya uzalendo wa baba wa Taifa sio huu wa vijana wa CCm wanaotaka kuaminisha Watanzania.
Uzalendo Sio Kuipenda CCM,
Uzalendo Sio Kusifia Serikali,
Uzalendo Sio Kubeba Ilani ya CCM,
Uzalendo Sio Kuvaa Bendera ya Taifa,
Uzalendo Sio Kunyamazia unyanyasaji.
Uzalendo sio kunyamazia Ufisadi.
Uzalendo ni kuipenda, kuithamini na kujitoa kwa ajili ya nchi yako kwa msingi wa kabila, utamaduni, siasa au historia.
Ukiangalia hii Tafsiri ya Uzalendo, kupata kijana au Kiongozi CCM mwenye huu uzalendo utamtafta kwa Toshi.
Mifano ipo mingi sana ya namna hii ukiangalia apo nyuma hasa awamu ya JK. Vijana wengi walihoji na kukosoa mwenendo wa serikali yao. Wengi walihoji hasa juuu ya Ufisadi na Matumizi mabaya ya kodi za watanzania.
Cha kushangaza, baada ya hawa vijana Type ya " Polepole" kuingia kwnye system na wao wakafyata mkia.
Sasa swali ni hili.
Hivi Baba wetu wa taifa angekuwa kama hawa vijana wa sasa wa CCM ( kigogo anawaita MATAGA), je Tungepata uhuru au Tungepataje uhuru?
Mnafikiri mabeberu hawakutafta njia tofauti za kumdhuru au kumhonga Nyerere ili aache chokochoko za kupigania uhuru? Kumbuka Baba yetu wa Taifa alisomeshwa na hawa Mabeberu mpaka wakamfadhili na kumsomesha chuo cha Edinburgh nchini Uingereza ( 1952) lakini hakuwa mnafiki alipigani uhuru wa Watanganyika na kuhakikisha wanatuachia nchi yetu.
Ukiangalia hata mandela naye ivyo ivyo. Alikuwa mwanasheria na maisha mazuri tu ila alipigania uhuru wa nchi yake ingawa aliteswa sana na Mabeberu.
Uzalendo wa Baba yetu wa Taifa ndyo uliotufanya tupate uhuru. Ila Tafsiri ya uzalendo wa baba wa Taifa sio huu wa vijana wa CCm wanaotaka kuaminisha Watanzania.
Uzalendo Sio Kuipenda CCM,
Uzalendo Sio Kusifia Serikali,
Uzalendo Sio Kubeba Ilani ya CCM,
Uzalendo Sio Kuvaa Bendera ya Taifa,
Uzalendo Sio Kunyamazia unyanyasaji.
Uzalendo sio kunyamazia Ufisadi.
Uzalendo ni kuipenda, kuithamini na kujitoa kwa ajili ya nchi yako kwa msingi wa kabila, utamaduni, siasa au historia.
Ukiangalia hii Tafsiri ya Uzalendo, kupata kijana au Kiongozi CCM mwenye huu uzalendo utamtafta kwa Toshi.