Warumi 13:1-7 maneno ya Mungu yafuatayo yameandikwa:
"Kila mtu na atii mamlaka inayotawala, kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu, nazo mamlaka zilizopo zimewekwa na Mungu. 2Kwa hiyo yeye anayeasi dhidi ya mamlaka inayotawala anaasi dhidi ya kile kilichowekwa na Mungu, nao wale wafanyao hivyo watajiletea hukumu juu yao wenyewe. 3Kwa kuwa watawala hawawatishi watu wale wanaotenda mema bali wale wanaotenda mabaya. Je, wataka usimwogope mwenye mamlaka? Basi tenda lile lililo jema naye atakusifu. 4Kwa maana mwenye mamlaka ni mtumishi wa Mungu kwa ajili ya mema. Lakini kama ukitenda mabaya, basi ogopa, kwa kuwa hauinui upanga bila sababu. Yeye ni mtumishi wa Mungu, mjumbe wa Mungu wa kutekeleza adhabu juu ya watenda mabaya. 5Kwa hiyo ni lazima kutii wenye mamlaka, si kwa sababu ya kuogopa adhabu iwezayo kutolewa, bali pia kwa ajili ya dhamiri.
6Kwa sababu hii mnalipa kodi, kwa maana watawala ni watumishi wa Mungu, ambao hutumia muda wao wote kutawala. 7Mlipeni kila mtu kile mnachodaiwa. Kama mnadaiwa kodi lipeni kodi, kama ni ushuru, lipeni ushuru, astahiliye hofu, mhofu, astahiliye heshima, mheshimu".
Naomba mnisaidie kwa mujibu wa maagizo hayo hapo juu, katika hili valangati kati ya Kanisa la Kakobe na Serikali kupitia TANESCO na Wizara ya Nishati na Madini, je hivi Askofu Zakaria Kakobe yuko sahihi kukaidi na kutembeza ubabe wa kuwalazimisha wafuasi wake wafanye vitimbwi wanavyovifanya hata kuwapiga watumishi wa TANESCO ambao wako pale kutoa huduma ya umeme? Je hayo maagizo na amri zilizomo ndani ya mistari hiyo ya Warumi kweli Kakobe anatii? Mimi naona anaongozwa na ubinafsi. Na kwa hili Mungu atamwadhibu.
"Kila mtu na atii mamlaka inayotawala, kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu, nazo mamlaka zilizopo zimewekwa na Mungu. 2Kwa hiyo yeye anayeasi dhidi ya mamlaka inayotawala anaasi dhidi ya kile kilichowekwa na Mungu, nao wale wafanyao hivyo watajiletea hukumu juu yao wenyewe. 3Kwa kuwa watawala hawawatishi watu wale wanaotenda mema bali wale wanaotenda mabaya. Je, wataka usimwogope mwenye mamlaka? Basi tenda lile lililo jema naye atakusifu. 4Kwa maana mwenye mamlaka ni mtumishi wa Mungu kwa ajili ya mema. Lakini kama ukitenda mabaya, basi ogopa, kwa kuwa hauinui upanga bila sababu. Yeye ni mtumishi wa Mungu, mjumbe wa Mungu wa kutekeleza adhabu juu ya watenda mabaya. 5Kwa hiyo ni lazima kutii wenye mamlaka, si kwa sababu ya kuogopa adhabu iwezayo kutolewa, bali pia kwa ajili ya dhamiri.
6Kwa sababu hii mnalipa kodi, kwa maana watawala ni watumishi wa Mungu, ambao hutumia muda wao wote kutawala. 7Mlipeni kila mtu kile mnachodaiwa. Kama mnadaiwa kodi lipeni kodi, kama ni ushuru, lipeni ushuru, astahiliye hofu, mhofu, astahiliye heshima, mheshimu".
Naomba mnisaidie kwa mujibu wa maagizo hayo hapo juu, katika hili valangati kati ya Kanisa la Kakobe na Serikali kupitia TANESCO na Wizara ya Nishati na Madini, je hivi Askofu Zakaria Kakobe yuko sahihi kukaidi na kutembeza ubabe wa kuwalazimisha wafuasi wake wafanye vitimbwi wanavyovifanya hata kuwapiga watumishi wa TANESCO ambao wako pale kutoa huduma ya umeme? Je hayo maagizo na amri zilizomo ndani ya mistari hiyo ya Warumi kweli Kakobe anatii? Mimi naona anaongozwa na ubinafsi. Na kwa hili Mungu atamwadhibu.