Hivi askofu Kakobe yuko sahihi?

Marigwe

JF-Expert Member
Nov 28, 2009
228
18
Warumi 13:1-7 maneno ya Mungu yafuatayo yameandikwa:

"Kila mtu na atii mamlaka inayotawala, kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu, nazo mamlaka zilizopo zimewekwa na Mungu. 2Kwa hiyo yeye anayeasi dhidi ya mamlaka inayotawala anaasi dhidi ya kile kilichowekwa na Mungu, nao wale wafanyao hivyo watajiletea hukumu juu yao wenyewe. 3Kwa kuwa watawala hawawatishi watu wale wanaotenda mema bali wale wanaotenda mabaya. Je, wataka usimwogope mwenye mamlaka? Basi tenda lile lililo jema naye atakusifu. 4Kwa maana mwenye mamlaka ni mtumishi wa Mungu kwa ajili ya mema. Lakini kama ukitenda mabaya, basi ogopa, kwa kuwa hauinui upanga bila sababu. Yeye ni mtumishi wa Mungu, mjumbe wa Mungu wa kutekeleza adhabu juu ya watenda mabaya. 5Kwa hiyo ni lazima kutii wenye mamlaka, si kwa sababu ya kuogopa adhabu iwezayo kutolewa, bali pia kwa ajili ya dhamiri.
6Kwa sababu hii mnalipa kodi, kwa maana watawala ni watumishi wa Mungu, ambao hutumia muda wao wote kutawala. 7Mlipeni kila mtu kile mnachodaiwa. Kama mnadaiwa kodi lipeni kodi, kama ni ushuru, lipeni ushuru, astahiliye hofu, mhofu, astahiliye heshima, mheshimu".

Naomba mnisaidie kwa mujibu wa maagizo hayo hapo juu, katika hili valangati kati ya Kanisa la Kakobe na Serikali kupitia TANESCO na Wizara ya Nishati na Madini, je hivi Askofu Zakaria Kakobe yuko sahihi kukaidi na kutembeza ubabe wa kuwalazimisha wafuasi wake wafanye vitimbwi wanavyovifanya hata kuwapiga watumishi wa TANESCO ambao wako pale kutoa huduma ya umeme? Je hayo maagizo na amri zilizomo ndani ya mistari hiyo ya Warumi kweli Kakobe anatii? Mimi naona anaongozwa na ubinafsi. Na kwa hili Mungu atamwadhibu.
 
Japo binafsi nafikiri neno hilo linahitaji tafsiri sahihi, nayo ni hii
Wanaohitaji heshima wapeni heshima, wanahitaji kuogopwa na muwaogope.
Swali ni je, kikwete na serikali yake wanahitaji kuheshimiwa au kuogopwa?.

My take: kakobe is leading a bunch of hyptonized cheap to go citizen of bongo into a river full of crocodiles.
This is such a small issue to print tshirts for. What is kakobes's patriotism?
How many scandals is this governmet hovering in and yet this guy has no guts to say something about.

I remain to be corrected. But not with any of them, I mean them. Yes.
 
Kama unatumia biblia kuhalalisha uharamia wa serikali na yeye atatumia biblia hiyo hiyo kuhalalisha uwepo wake pale serikali iliyo dhalimu si mtumishi wa Mungu
 
Ndugu Luteni. Fine then should they (the government and Kakobe) engage in a war of quotes and misquotes as you are purpoting?
 
kilijadili hili swala linahitaji hekima zaidi kwa sababu serikali inahitaji heshima yake na watumishi wa mungu wana heshima zao na kakobe katoa hoja ya msingi ya kwann umeme ucpite pale na tanesco awatoi sababu za msingi zaidi ya kushinikiza bila kuangalia madhara yatakayo wapata watu
 
Madhara gani? yeye kakobe kajenga kufuata kanuni na taratibu za ujenzi? nini maana ya kuwa na eneo linaitwa reserve kwa ajili ya huduma mbalimbali za jamii? Hata chakula unachokula kina madhara shauri ni kiasi tu. Tunahitaji maendeleo ya mwili ili tusiwe na visasi vya kutupeleka motoni.Tunachekesha zaidi tunapodhani kwamba ni serikali au tanesco inafanya ubabe. ni wangapi watafaidika na huduma hiyo ya umeme?Viwanda vingapio vitaweza kuacha kutumia majenereta ya kufua umeme na hivyo kupunguza ghrama za uzalishaji. heb u tutazame haya mambo kiundani zaidi wala si ushabiki wa kisiasa na uroho wa kuzungumza tu kujaza watu
 
kakobe yuko sahihi, kulikuwa na alternative ya kupitisha upande wa pili na aliwaambia lakini hawakusikia, ,Kumbukeni mtumishi wa Mungu Eliya aliizuia mvua kwa miaka kwasababu ya kiburi cha mfalme na watu wake, ni zaidi sana wakati huu. Unajua wakati mwingine hakuna haja ya kugombana na watumishi wa Mungu ,hawa ndiyo wanaosimama kama Musa na kufanya maombi ili Mungu airehemu nchi yetu tukigombana nao nani ataiombea nchi kama hasira ya Mungu ikishuka kama wakati wa wana wa Israel?

Viongozi wa serikali tunawatii wanapotuelekeza katika mema lakini katika mabaya hatuwatii hata kidogo, mkumbukeni Daniel, Meshaki ,Shadraki na Abedinego walikataa amri ya Mfalme na Mungu akawa upande wao.
 
Wakuu naamini mko sahihi kujadili lakini nahisi tunarudi nyuma ambapo maamuzi na utekelezaji ushafanyika na hakuna namna ya kurejesha nyuma tena maamuzi.
Tuongelee sasa kuhusu umeme kukatika katika na kuwa ktk mgao wa kichinichini baada ya miaka 5 ya kuahidiwa kuwa tatizo la umeme litakuwa historia
 
Msanii, kwenye hili, hakuna kurudi nyuma, kama kule Kalenga, walipitisha juu ya makaburi ya wahenga, umeme ukagoma kuwaka, wakauchepusha ng'abo ya barabara, wakayakwepa makaburi, wakarudisha baada ya makaburi, ukawaka!.<br />
<br />
Swali ni jee umeme umegoma kuwaka?. Kama kweli umegoma, hii ni proof Mungu wa Kakobe ndie Mungu wa Kweli kama alivyowafanyia, Shadrack, Meshaki na Abernedgo.<br />
<br />
Nami sasa najiandaa kujiunga huko rasmi, na tutaanzisha forum ya Miujiza &quot;Miracles!&quot;.<br />
 
kwani kakobe ni mtumishi wa mungu?! mtumishi wa mungu ni PAPA peke yake sijasikia akifanya ushirikina wa kutoa misukule..
kuhusu umeme kakobe kachemka! alitoa mfano wa makaburi sijui ya wapi akidai serikali iliogopa nguvu za giza nguzo za umeme zikavuka ng`ambo, na yeye anataka wafanye vile kwake, kakobe amekaa kibiashara zaidi.. :confused2:
 
Kakobe ni mjasiriamali kama wenzake kina Gwajima na Mama Lwakatare...yule mwenzao kule Kenya anajiita Mheshimiwa, Mchungaji, Dokta Margaret Wanjiru, kaingia kwenye siasa kaiba kura akawa mbunge akapewe uwaziri msaidizi, Mungu kamuumbuwa kashindwa kesi ya uchaguzi mahakamani...mtaji wa hadaa umepunguwa kwake...masikini hoi nafsi yake!
 
Back
Top Bottom