Hivi aliyeruhusu wanafunzi wa sekondari kuvaa hijabu alijua madhara yake?

Status
Not open for further replies.

britanicca

JF-Expert Member
May 20, 2015
15,635
29,967
Suala la hijabu kuvaliwa shuleni sisi wanaoona mbali tulishajua litaleta matatizo, hasa kwa wanafunzi wanaokua tena ni wa kike.

Madhara yake wameshaanza kuzificha mimba, nywele chafu na wengine wamesuka. Pia inaondoa uniformity kwa wanafunzi.

Halafu pia nasikia maeneo mengine hata wakatoliki wameanza kudai nao kuvaa baadhi ya ishara za kikatoliki shuleni. Vipi kila dini ikidai haki hiyo hata asiyekuwa na dini akisema aende na Tunguli zake?

Tutafakari upya juu ya hijabu kuvaliwa shuleni kwa shule za Serikali.

Britanicca

Mtoa post nilitegemea sana unakuja na hoja ya maana na msingi ambayo ingetazamwa kama sehemu ya GT katika Jamiiforums lakini ajabu umekuja na mambo ya kitoto sana labda kwa sababu ya chuki zako binafsi za kidini.

kuficha mimba hakuhusiani na mavazi na kumbuka kwamba mimba haifichwi kwa mavazi itaonekana tu,ima nyumbani au hata shuleni,suala la mimba haliendi peke yake kwa mtazamo wa mavazi,hata dalili ni ishara tosha ya kumjua mjamzito,labda iwe kwamba kiumri ama kiufahamu wa akili yako huyajui haya mambo.

Uchafu ni asili ya mtu,kama wewe ni mchafu ni mchafu tu hata uwe vipi,hata uvae vipi,hata uwe nani utabaki kuwa mchafu.

kumbuka moja kati ya masuala makubwa katika dini ya uislamu ni usafi,usafi ni sehemu ya imani ya muislamu.

Unatutia mashaka na kiwango chako cha uelewa wa neno UNIFORMITY,inawezekana lkabda ni kwa sababu neno hili ni lugha ya kigeni ana pia hufahamu tafsiri hali ya maana yake,kwa muonekano wowote ule ambao utakubaliwa kuwa sehemu ya uniform,basi hautabadilishwa hadi mtu awe nje ya makubaliano ya kiuniform.
hivi uliwahi tumia uwezo wako wa kufikiri kisha ukajiuliza kuhusu maana na matumizi ya tunguri kisheria ?
 
Kuvaa hijab ni jambo1 na kutumia hijab kufanya maovu ni ishu nyingine acha chuki mkuu..
Inamaana watu wasipewe leseni za bodaboda eti kwa sababu baadhi ya watu wachache wanafanyia ualifu?

Km kuna hiyo shida ni tatizo la wazazi na walimu kutokuwa makini na kazi yao ya ulezi.

NB: acha chuki.

Sent using Jamii Forums mobile app
Inabidi wawe uniform siyo mambo ya kutofautiana
 
Kuvaa hijab ni jambo1 na kutumia hijab kufanya maovu ni ishu nyingine acha chuki mkuu..
Inamaana watu wasipewe leseni za bodaboda eti kwa sababu baadhi ya watu wachache wanafanyia ualifu?

Km kuna hiyo shida ni tatizo la wazazi na walimu kutokuwa makini na kazi yao ya ulezi.

NB: acha chuki.

Sent using Jamii Forums mobile app
Jamaa umetoa hoja nzuri sana.
Mjadala uendelee.
 
wavae hata wasabato na ambao hawana dini, la msingi ni kwamba mwanamke anatakiwa kusitirika.

kuhusu usafi hata kama angekuwa anatembea uchi hali hio isingethibitika.

la mwisho ondoa hio kutu kwenye moyo wako maana hutafaidika na lolote lile aidha kwa kupinga au kuwadhulumu wanaojisitiri kwa kumuogopa Mola wao.
 
Status
Not open for further replies.
15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom