Historia ya Wachagga: Koo, Kabila na Falme-Mangi

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Baada ya kuona swali la JMushi ambalo ni kilio cha kusikia kuwa Babu yake Mangi Sina alikuwa msaliti, kauli ambayo JMushi anasema ilitolewa na John Mnyika, nimeonelea nifungue hii thread ili wenye kumbukumbu za kihisoria kuhusu ujenzi wa Kabila la Wachaga, koo na himaya za Mangi kutokana na mgawanyiko wa Wachaga, iwe ni Machame kwa Shangali, Kibosho kwa Sina, Marangu kwa Mareale, iwe ni Mangi Rindi, Meli, Pfumba, Molelia na wengine.

Aidha kutokana na kuongezeka kwa tuhuma za ukabila na hasa kusemekeana Chadema ni cha Wachaga na kuna ubaguzi kati ya Wamachame ambako Mwenyekiti wa Chadema Mbowe anatoka, dhidi ya Wachaga wengine, Kibosho, Uru, Vunjo, Kilema, Rombo nk. ni muhimu tupitie historia ya wachaga kwa manufaa yetu sote, tuijue hii jamii, na ni jinsi gani ilivyoweza kuwa kubwa na kuwa na umahiri katika masuala ya biashara na elimu.

Natumaini JMushi atatumia fursa hii kujifunza kuhusu Kabila lake na historia yake pamoja na mahusiano kati ya makundi ya wachaga na hivyo kutoa majibu ya maswali aliyonayo hasa kuhusu uadui kati ya Mangi Meli na Mangi Sina.

Naomba kufunga ukumbi kwa majadiliano na kuelimishana.
 
Nitashukuru kwa darasa waungwana.
Ahsante sana Rev Kishoka...Na pia tunaomba Mnyika ambaye anagombea huko Ubungo uliko...Ajitahidi kuja hapa na kukusikiliza ili atowe ufafanuzi ili na mimi nielemishwe.
Once again nashukuru sana na ninategemea nafasii hii itatumika kutuelemisha.
 
Mushi,

Ikifuata Wikipedia ukatafuta Chaga, utapata historia ndogo ya Uchaga na walikotoka.

Hata hivyo naambatanisha hii makala niliyoipata Harvard university inaweza kukusaidia.
 

Attachments

  • Vifo vya Watoto Kilimanjaro 1894-1935.pdf
    121.4 KB · Views: 1,030
Mchungaji...Shukran...Naomba pia usisahau kuwa madhumuni halisi ya wewe kuanzisha thread hii ni baada ya kudai kuwa mimi kuliuliza suala hili kwenye ile thread nyingine haikufaa.
Na hivyo basi ningeomba Mnyika ajaribu kutowa maelezo ya kihistoria ili wengine wetu tuweze kuelewa kuwa usaliti huo wa Sina ni upi.
Siko hapa kuchaguwa upande upi ni mzuri ama upi ni mbaya...Inawezekana kweli ni msaliti na mimi sijui...Hivyo maelezo yangesaidia kwani ndio kuelimishana huko pamoja na kujengana kwa kuthamini na kueleweshana kuhusu historia ya Taifa letu kwa ujumla...Taifa nalo litanufaika pia na historia ya usaliti huo.....Usaliti ambao kwa kweli ni muhimu Mnyika auweke wazi kwani alisema ulisababisha damu ikamwagika dhidi ya Mdachi.
Ahsante.
 

THE CHAGGA AND THEIR CHIEFS History of the Chagga People of Kilimanjaro. By KATHLEENM . STAHL. The Hague: Mouton, I964. Pp. 394, maps. 32 Guilders.

This book is the result of four years' work, of which eighteen months were spent in fieldwork among the Chagga. It was written at the invitation of the Chagga Trust, which evidently supplied interpreters and arranged interviews with the Chagga elders. The complexity of the task can be gauged from Mrs Stahl's remark that in Chaggaland the 'historical units' are the 133 mitaa, or parishes, of which about I00 represent the now submerged petty kingdoms of former days. In one sense it is a disappointing book. There is, for example, the whole gamut of questions concerning the historical relations of the Chagga with the neighbour-ing peoples of East Africa.

Chagga traditions of origin are extremely varied, and suggest a long process of accretion of population from almost all of the surround-ing regions-Kamba, Teita, Pare, Shambaa, Masai, Arush, and even Nyamwezi. The occurrence of Ntemi, the Nyamwezi word for chief, in the early stages of several of the Chagga dynastic genealogies suggests that the idea of chieftainship may have reached the Chagga directly or indirectly from that source. Other ideas and techniques, such as the elaborate system of irrigation practised by the Chagga from their mountain streams, or the stone fortifications, as yet imperfectly explored but belonging apparently to a comparatively early phase of their political history, raise equally interesting problems of origin, for all of which Mrs Stahl has very little to add to the comments of earlier writers. Her book is concerned almost entirely with the internal history of the Chagga people. The reader must go with her to the mountain; it will not be brought to him.

Moreover, what chiefly interests her in Chagga history is the nineteenth and twentieth centuries, especially the history of the last hundred years during which traditions can be checked to some extent from written documents. This is not to say that her approach is European-centred, very much the reverse. The central message of her book is the essential continuity of Chagga political history from the pre-colonial to the colonial period. In the pre-colonial period the political history of Chaggaland was that of perennial intrigue and rivalry for position of the leading Chagga states. In this basic competition external factors played a role, but only a subordinate role. The successful Chagga chief was the one who could most effectively manipulate the outsider and use him against his rivals. In the early nineteenth century, before the advent of the main external factors, Kibosho was the leading Chagga state, and in Mrs Stahl's view it still is the natural centre of Chaggaland. But the outside world has always failed to realize this fact, because the external factor has always been manipulated by one of the other states. In the third quarter of the nineteenth century it was Rindi of Moshi who manipulated the Arabs and Swahili and used them to build up a completely spurious picture of his own pre-eminence. At the end of the nineteenth century it was Marealle of Marangu who manipulated the Germans and used them in the most unscrupulous possible way to destroy his rivals. In the second quarter of the twentieth century it was Abdiel of Machame who best understood how to manipulate the British. Though the chiefs lost their sovereignty after I886, [says Mrs Stahl] those of them who won the favour of the European administrators were afforded a steadily opening field of new opportunities. .... It is arguable that Mangi Abdiel of Machame in I946 enjoyed more power than the greatest sovereign ruler, Mangi Sina of Kibosho, had done until the time of his conquest by the Germans in 1891.... Political life continued to centre on the devising of intimate stratagems.... Intimidation continued, chiefs still dispatched their enemies by violence and the murderers were not brought to task.... The Chaggae employed whole new range of political gambits centring on the Boma. The chiefs kept themselves apprised of what was going on there through many informatory channels, from scouts posted as household servants upwards, and there was little that escaped them, whether it was set down in confidential files or in open ones .... All this is no doubt true, and it is a part of the truth which has seldom been appreciated by historians of the colonial period. But it is not the whole truth, and one feels that Mrs Stahl's preoccupation with the internal politics of the Chagga chiefdoms has prevented her from seeing something of more importance -namely the effect of the colonial period on the Chagga people as a whole. While the colonial period lasted, chiefs appeared to be as important as they had been of old, and their ways changed less than those of ordinary people. But the rise of nationalism and of independent African governments has revealed the hollowness of most chiefly survival through the colonial period, and has under-lined the fact that what really mattered during the colonial period was not what went on in the palace but what went on in the mission school. And about this Mrs Stahl has practically nothing to say.


This is a book review, lakini nadhani kama jmushi na wengine mkikipata kitabu chenyewe itakuwa vizuri zaidi. Maana huyu reviwer amegusia tu nini kilichomo na ambacho hakiko kwenye kitabu chenyewe. Mhh sijui maktaba zetu tutakuwa nacho?
 
Lakini si mnaelewa kwamba nchi yetu haina ukabila? sasa mjadala huu usije ukageuka kwa namna yoyote ile, maana mkishajua matabaka ya wachaga mnaweza kugeukia kwa wahaya, wasukuma, wapare na ... mwisho watanganyika!
 
Lakini si mnaelewa kwamba nchi yetu haina ukabila? sasa mjadala huu usije ukageuka kwa namna yoyote ile, maana mkishajua matabaka ya wachaga mnaweza kugeukia kwa wahaya, wasukuma, wapare na ... mwisho watanganyika!

Kosa kubwa la Watanzania ni kukwepa kuangalia na kujifunza kutoka ukweli wa mambo. Hili ni somo kwetu, hata kama ni chungu kama ndimu.

Angalia kukwepa kukaa chini na kujadili kasoro za muungano wa Tanganyika na Zanzibar zilipotufikisha.
 
Lakini si mnaelewa kwamba nchi yetu haina ukabila? sasa mjadala huu usije ukageuka kwa namna yoyote ile, maana mkishajua matabaka ya wachaga mnaweza kugeukia kwa wahaya, wasukuma, wapare na ... mwisho watanganyika!

Mjadala huu hauwezi kwenda huko...Mjadala huu utalisaidia Taifa kwani liko njia panda kwa kutokujuwa historia yake toka MKOLONI aje na toka machifu hao wapambane na UKOLONI.

Mjadala huu hauwezi kuharibika kwani sisi ni wana jf...Na tunaweza kuitumia fursa hii ya forum hii kuweka mambo sawa.

Hadi sasa maelezo ninayopata yanaonyesha kuwa Sina alikuwa SHUJAA NA KAMANDA WA AFRIKA!

Hakutaka UBAGUZI na kusema ukweli makabila mengine yalishikiana na mkoloni kupigana na Sina.

Lakini bado kweli alitetea uhuru....Kuitwa Msaliti na Mnyika ambaye ni SAUTI NZITO YA CHADEMA ndio swala ambalo tunaomba tuelimishwe...Hatusemi kuwa machifu hawa ni perfect...NO!

Mbona ndugu zetu wengine waliwaita viongozi wao kwa maana ya UTEMI?

Ofcourse maana halisi ya Mangi ni THE PLANNER...Kwa maana hiyo yeye licha ya uongozi...Pia hu plan namna ya ku move forward.

Kama yukitumia ile spirit ya wale machifu wetu kuja pamoja..Basi kwasasa tumeshajuwa mipaka ya Taifa ama Bara letu...Na kwa hiyo sasa hvi si kutetea KINGDOM TENA...BALI UHURU WA MWAFRIKA.

Kwa wale wafuatiliaji wa historia ya wachagga...Wameanzia toka hata Afrika ya magharibi...Bantu.

Halafu kwa mfano mimi binafsi asili yangu ni mixer ama ni wahamiaji wa kimasai kutoka eneo la oldonyo sambu.

Na kwahiyo hata Sina mwenyewe ambaye alikuwa na sifa ya KU PROTECT MALI ZA NCHI....Alikuwa ni mpiganaji mwenye asili ya UMASAI.

Ni vyema kuweka Historia wazi ili hata kama kweli kuna mambo ya rumours ndiyo yawekwe pembeni.

Kwa mfano Sina alikuwa na sifa ya Giantism na hata wazungu huko Europe walikuwa wakimzungumzia na ilibidi kuwatumia wengine kumbana kama alivyofanya Rindi ku collaborate na waarabu ama Marealle ku collaborate na wajerumani nk.

Mimi Rafiki yangu mkubwa hata kule kwenye facebook ni mjukuu wa mangi Shangali wa machame...Sasa wale wanaotaka kuleta ukabila ama vijimaneno vya chuki vya kujipendekeza na kuharibu usalama wa Taifa ni watu kama kina Mnyika..Halafu yeye yuko kimnya akiitumia karata ile ile a kuvuruga attention kwa kusema amemtumia message RA...!

Ni vyema kuja pamoja kama Taifa na wana wa Afrika katika ujenzi wa Bara letu...Na hata kama tukishirikiana na wageni...Basi ushirikiano huo uwe wa manufaa kwa wananchi.

Bado naendelea kufuatilia maoni na Historia zaidi ili kujuwa hasa nini kiliendelea katika nchi yetu na ni kwanini tuko hapa tulipo.

Na pia wale wanaosema kuijadili issue hii ni UKABILA basi wamekosea...Nafikiri wamesahahu hata watoto wa JK walishasema na wao ni UKOO WA CHIFU.

Mimi sikusema ni UKOO WA CHIFU na wala sikuwa na mpango huo..Lakini baada ya ile makala ya MASHUJAA WA TANZANIA NA Kauli ya Mnyika..Basi ni wazi kuwa mjadala huu ni muhimu.
 
Swala lako JMushi ni kuelewa historia ya wachaga au wapi Mnyika amequote katika hiyo statement yake? Vinginevyo thread imeanzishwa haitakidhi matakwa yako mpaka Mnyika ajibu.
 
Lakini bado kweli alitetea uhuru....Kuitwa Msaliti na Mnyika ambaye ni SAUTI NZITO YA CHADEMA ndio swala ambalo tunaomba tuelimishwe...Hatusemi kuwa machifu hawa ni perfect...NO!
Mushi,

Nafikiri inabidi umuulize Mnyika kama alitoa tamko hili kuwa Mangi Sina ni msaliti kwa kutumia nafsi yake binafsi au kama kiongozi wa Chadema.

Humtendei haki Mnyika au Chadema ukiwajumuisha pamoja na kuwaita wazushi kwa maoni yako kuwa Mangi Sina alikuwa msaliti.
 
Mushi,

Nafikiri inabidi umuulize Mnyika kama alitoa tamko hili kuwa Mangi Sina ni msaliti kwa kutumia nafsi yake binafsi au kama kiongozi wa Chadema.

Humtendei haki Mnyika au Chadema ukiwajumuisha pamoja na kuwaita wazushi kwa maoni yako kuwa Mangi Sina alikuwa msaliti.


Mchungaji unajichosha bure tu endelea na mambo yako mengine!!
 
Mushi,

Nafikiri inabidi umuulize Mnyika kama alitoa tamko hili kuwa Mangi Sina ni msaliti kwa kutumia nafsi yake binafsi au kama kiongozi wa Chadema.

Humtendei haki Mnyika au Chadema ukiwajumuisha pamoja na kuwaita wazushi kwa maoni yako kuwa Mangi Sina alikuwa msaliti.

Sawa...Aje kusema kama ni usemi wake binafsi...Hata hivyo wale waliomsapoti kama kina MKJJ na Wembe Mkali labda wanaweza kumsaidia...Ila ni muhimu sana na yeye akaja hapa na kutowa ufafanuzi kwasababu ya nafasi yake kwenye jamii...

John Mnyika
user_offline.gif

John Mnyika has no status.
JF Senior Expert Member
Join Date: Fri Jun 2006
Location: Tanzania
Posts: 627
Rep Power: 24
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_highpos.gif
reputation_highpos.gif
reputation_highpos.gif

Thanks: 6
Thanked 276 Times in 97 Posts
Credits: 62,420


icon1.gif
Ya Kale Ni Dhahabu
Chambelecho cha maadhimisho ya Siku ya Mashujaa: Tunu yangu kwa wakina Kinjeketile

Na John John Mnyika

Kamaradi Kinjeketile na mashujaa wenzako popote mlipo! Hii ni tunu kwenu. Hidaya kwenu mliomwaga damu wakati mapambano kadhaa na Mreno na Mwarabu. Tuzo kwenu nyinyi mliopigana na Ujerumani wakati wa utawala na mliomwaga damu katika vita vya dunia. Heko ninyi ambao damu ilisafisha safari ya kumng’oa Nduli Amin. Heri wewe Sethi Benjamini na wote waliopotesha maisha katika hekaheka za kueneza Azimio la Arusha. Kumbukumbu kwenu mliotoa damu katika mikikimikiki ya mfumo wa vyama vingi kutoka Zanzibar mpaka bara. Damu yenu iliyomwagika haizoleki, ukiwa mlioucha hauzoeleki lakini fikra mlizosimamia hazizeeki. Mapambano bado yanaendelea!

Kwako Bushiri bin Salim wa Tanga, suriama wa kiarabu na kiafrika, pamoja na nia yako tenge ya kulinda maslahi katika biashara ya utumwa ulimwaga damu kwa kunyogwa Pangani baada ya kuongoza maasi makali dhidi ya kuingia kwa ukoloni wa Kijeruamani-damu yako ilimwagika pamoja na damu za wapiganaji wa Pwani, Morogoro mpaka uhehe. Ewe Mtemi Meli, uliowashinda wadachi mpaka mwenzio Sina alipokusaliti hatimaye wewe na mashujaa wenzako mkamwaga damu kaskazini mkilinda uhuru.Wewe Chifu Mkwawa, tunakukumbuka uliovyowaunganisha wahehe-toka Kalenga, Tosamaganga mpaka ulipoamua kuimwaga damu yako mwenyewe kuliko uhuru upotee mikononi mwako. Mtemi Isiki wa Tabora uliendesha mashambulizi ya kishujaa, hatimaye ukaamua kumwaga damu yako na ya familia yako kwa kujilipua na baruti ili tu usipate aibu ya uhuru kuchukuliwa mbele ya macho yako. Ewe Mtemi Makongoro wa Musoma, ulipambana kwa ushujaa mpaka ilibidi kikosi cha wanamaji kiletwe kupitia miji ya Mombasa na Kisumu kukumaliza.

Nakutunuku Kinjeketile kwa kuongoza vita vya kutisha vya Maji Maji kwa miaka kadhaa vilivyoanzia vilima vya Matumbi karibu na Kilwa. Nyinyi mlitaka kumwondoa mkoloni kwa nguvu na mlikuwa tayari kumwaga damu kuliko kuendelea kuishi bila ya uhuru. Mapambano yenu yalisambaa maeneo mengi ya ardhi yetu. Ninyi mlikuwa mashujaa kweli kweli mliojua umuhimu wa imani na falsafa katika mapambano-mkawapa watu ujasiri kwa dawa ya “Kugeuza risasi, Kuwa maji”. Pamoja na kushindwa vita na wazalendo zaidi ya laki moja kupoteza maisha katika wakati ambao ardhi ilikuwa na watu wachache yapo mapigano ambayo mlishinda. Pamoja na machifu 47 wa Kingoni kunyongwa damu yenu ilileta mabadiliko katika utawala. Kwa vyovyote vile damu nyingi kiasi hiki iliyomwagika kwa sababu ya kudai uhuru haiwezi kupuuzwa. Hivyo waraka huu ni tunu kwenu. Mapambano bado yanaendelea!

Nawaandikia waraka huu ninyi wahenga mashujaa muweze kurejea na kurekebisha historia. Najua mnaweza msirudi kimwili, lakini ni vyema kiroho mkandelea kuwa nasi. Fikra zenu za kimapambano hazipaswi kupotea. Kumbukumbu zenu za kishujaa hazistahili kufutika. Taifa lisilo na historia haliishi, linakufa. Kupotosha historia ya mashujaa ni kinyaa. Karibu kila eneo katika nchi yetu yupo shujaa ambaye anaweza kukumbukwa laiti kama historia zenu zingejulikana kizazi hata kizazi na kuwa chimbuko la kujiamini, kujithamini na uzalendo miongoni mwa Watanzania.

Julai 25 ilikuwa siku nyingine ambapo tulifanya maadhimisho ya kinafiki ya siku ya mashujaa. Mtanishangaa kwa kutumia dhana kali- “UNAFIKI”. Namaanisha!. Ni dhana ambayo mnaifahamu na hamkuipenda. Ndio maana hamkutaka kuishi katika unafiki wa kukubaliana ama kutumiwa na watawala. Mkaamua kupambana! Mkamwaga damu mkiukimbia unafiki. Sasa tunawakumbuka! Lakini nasema tena, tunawakumbuka kwa kufanya maadhimisho ya kinafiki ya siku ya mashujaa. Ndani ya dhana ya unafiki kuna tabia nyingi, mojawapo ni kunena tofauti na matendo na kutenda tofauti na kauli. Na ndiyo tabia tunayoifanya wakati wa maadhimisho ya siku ya mashujaa. Ndio maana nasema, tunafanya maadhimisho ya kinafiki.

Labda ni waambie wakina Kinjeketile, nini tulifanya huku kama ishara ya kuuadhimisha ushujaa wenu. Siku chache zilizopita 25 Julai, tulijumuika chini ya Amiri Jeshi Mkuu, kwa sasa ni Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Yeye mwenyewe hakuwepo, alituma mwakilishi wake. Tulielezwa kwamba Rais yupo kwenye ziara ya kikazi Ujerumani!

Usiku mmoja kabla tuliwasha mwenge wa uhuru pale Mnazi mmoja. Halafu asubuhi yake gwaride lilijipanga kuwapokea wageni wa Kitaifa. Zikatolewa salam za Rais na wimbo wa Taifa ukapigwa kwa heshima yenu. Kikundi cha Buruji kikapiga “last post” na gwaride likaweka silaha begani. Askari sita waliojipanga vyema wakapindua silaha zao chini na baadae mizinga ikapigwa kwa ajili yenu huku watu wote wakiwa kimya. Gwaride likafanya “present arms” na kikundi cha buruji kikapiga “reveilles”. Gwaride likateremsha silaha na kufungua miguu.

Halafu silaha za asili ambazo nyingine nyinyi mashujaa mlizitumia zikawekwa kwenye mnara pamoja na maua. Baadhi ya silaha zilizowekwa ni pamoja na mkuki, ngao, sime, shoka, pinde na mishale. Hizi ni kumbukumbu sanifu za mapambano mliyoyafanya.

Hatimaye zikafuata sala na swala kutoka kwa viongozi wa dini wakiwakilishwa na sheikh, mchungaji, padri na maraji wa wahindu. Ingawaje sikumwona kiongozi wa dini ya jadi-ambao najua baadhi yenu nyinyi mashujaa na wahenga mliwaamini. Pengine dini za jadi zilitoweka na damu zenu. Gwaride likatoa tena heshima na wimbo wa taifa kupigwa ukafuatiwa na itifaki za viongozi wa kitaifa kuondoka. Wakabaki polisi kuzilinda silaha za kumbukumbu ya mashujaa mpaka jioni na hatimaye mwenge wa uhuru ukazimwa kama ishara ya mwisho wa maadhimisho ya kumbukumbu yenu ninyi mashujaa. Niwaulize wakina Kinjeketile, haya siyo maadhimisho ya kinafiki ya mashujaa? Pengine mtanijibu hapana!.

Ngoja niwaeleze masuala kadhaa halafu niwaulize tena. Siku hizi kuna kitu kinaitwa Bunge, hiki ni chombo cha juu chenye uwakilishi wa wananchi ambacho kunafanya maamuzi mbalimbali ambayo mengine huwa sheria. Chombo hiki ni kama yale mabaraza ya jadi yaliyokuwepo wakati wenu. Wiki iliyopita bunge lilijadili kuhusu maadhimisho ya vita vya Maji Maji ambavyo nyinyi wakina Kinjeketile mliviongoza. Miaka mia moja imepita toka damu yenu azizi ilipomwagika katika mapambano hayo ya kumwondoa mkoloni.Ungekuwepo najua ungekuwa Mbunge wa Kilwa, ungeshangaa sana-Eti maadhimisho ya vita mlivyovianza Kilwa na mapambano ya mwisho yakawa Songea, yanafanyika kinyume chake! Maadhimisho yameanzia Songea na waziri ameahidi pengine yataishia Kilwa. Chacha Wangwe, mbunge wa CHADEMA (wakati wenu hakukuwa na vyama vya siasa vyenye majina haya) jimbo la Tarime, yeye akahoji-kwanini bendera ya taifa isiwekwe rangi nyekundu kama ishara ya kuwakumbuka nyinyi mashujaa wetu? Naibu waziri wa habari na michezo, Mheshimiwa Emanuel Nchimbi-yeye akajibu, hakukuwa na sababu ya rangi nyekundu kuwekwa kwenye bendera ya Taifa kama ishara ya kuwakumbuka mashujaa. Eti, historia ya uhuru wa nchi yetu inaamuliwa kuanzia mkoloni wa mwisho aliyetutawala ambaye ni Muingereza. Sasa kwa kuwa tulipata uhuru wetu kwa amani bila kumwaga damu chini ya uongozi wa mwalimu Nyerere basi hakukuwa na sababu ya kuweka rangi nyekundu. Enyi mashujaa Kinjeketile na wenzako tunaowakumbuka leo mnakubaliana na jibu hili?

Ndio maana nikasema ni maadhimisho ya kinafiki. Tunanena tofauti na matendo. Nimesema awali, tunaanza maadhimisho ya leo kwa kuwasha mwenge wa uhuru halafu baadae tunaweka silaha za jadi. Kinjeketile na wenzako, iulizeni serikali- kama uhuru wetu tuliupata kwa amani, iulizeni serikali kwanini tunawasha mwenge wa uhuru na baadaye kuweka silaha za jadi? Tunanena tofauti na tunavyotenda? Iulizeni serikali, je harakati za mwisho za uhuru ni kipimo pekee cha historia ya nchi na hivyo kuwa kigezo pekee cha kuamua alama za nchi ikiwemo bendera?

Enyi mashujaa mlioambana kuulinda uhuru wetu dhidi ya wakoloni kuingia kuanzia wakati wa Mreno, Mwarabu na Mjerumani na kumwaga damu, mnakubaliana na majibu haya? Kushindwa kwenu na hatimaye ukoloni kuingia hakuondoi historia kuwa mlimwaga damu kwa ajili ya kulinda uhuru wa ardhi hii tukiyoirithi!

Enyi mashujaa mliopambana kuondoa ukoloni hususani ule wa Ujerumani mkamwaga damu, mnakubaliana na kumbukumbu hii? Kwamba mliyoyafanya si historia kuu kama historia ya uhuru toka kwa Mwingereza?

Enyi mashujaa, waulizeni wataalamu wa historia-baada ya Ujerumani kushindwa na makoloni yake yote kuwekwa chini ya halmashauri ya mataifa na baadaye baraza la udhamini, Tanganyika ikiwekwa chini ya uangalizi wa Uingereza-si kwamba tulikuwa katika hatua za mwisho kabisa za kupewa uhuru ambao tayari tulishaupata kwa damu? Waulizeni pia, hakuna damu yoyote iliyomwagika wakati wa Mwingereza? Je, historia ya nchi yetu iliyojikita katika kipenzi chetu Nyerere imewajumuisha mashujaa wote wa ardhi hii?

Nasema kwa damu-kuanzia ushindi pamoja na kushindwa dhidi Mjerumani ambao ulileta mabadiliko katika mfumo wa utawala sanjari na mashujaa ambao walikuwa mstari wa mbele katika jeshi la Mwingereza na washirika wake katika vita dhidi ya Mjerumani, vile vita vya dunia ambavyo vilipiganwa pia katika ardhi yetu? Wakina nani walimwaga damu zaidi katika kile kinachoitwa ukombozi ulioletwa na majeshi ya mfalme Afrika (KAR) kama si nyinyi babu zetu?

Hojini serikali, hivi bendera hii ni ya Tanganyika au Tanzania? Jibu la Nchimbi limetolewa katika muktadha wa historia ya Tanganyika, Ingekuwa vipi jibu lingetolewa mintaarafu bendera ya Tanzania ambayo ilipatikana kutokana na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ilihali visiwani kuna historia ya damu kumwagika ama kumwagwa wakati wa mapinduzi? Kama kweli tuna serikali ya mapinduzi Zanzibar na utawala wa Chama cha Mapinduzi(CCM), je ni mapinduzi yasiyo na ‘rangi nyekundu’?

Tunatenda tofauti na kauli! Tunafanya maadhimisho ya kinafiki. Wakina Kinjeketile tunawakumbuka kwa kuwa mlimwaga damu kupinga ukoloni na unyanyasaji. Mtuulize wajukuu zenu, je tunawaadhisha kwa kuendelea kupiga vita yale mliyoyakataa? Kwa hali ilivyo, wapo wanaotenda yale mliyoyakataa pamoja na kuwa wote kwa kauli tunawaenzi ninyi mashujaa. Tunapaswa sasa kuweka fikra zenu katika vitendo kwa ajili ya ukombozi wa taifa letu. Mwalimu Nyerere alikumbuka fikra zenu akatamka na kutenda kwamba uhuru, si uhuru wa maneno. Ni uhuru dhidi ya ujinga, uhuru dhidi ya maradhi, uhuru dhidi ya umaskini na baadaye akaongezea uhuru dhidi ya rushwa ama ufisadi. Enyi wahenga mashujaa, shukeni katika nyoyo za watoto na wajuu zenu, mtufanye kutokana na maadhimisho ya mwaka huu tuweke dhamira ya kupigana vita kwa zana kisasa kuleta mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli, kuleta haki na maisha bora. Hii ndiyo hidaya kwa damu yenu azizi. Sio siri, kwa sera bila silaha, mapambano bado yanaendelea!

Mwandishi wa makala hii ni mwanaharakati na mwanasiasa kijana anayepatikana kupitia mnyika@yahoo.com na 0744 694 553

Kumbukumbu toka:http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_13.html
__________________
Kizazi Kipya, Maisha Mapya
New Generation, New Life

Mabadiliko ya Kweli, Uhuru wa Kweli
Real Change, Real Freedom

John Mnyika

The Following 3 Users Say Thank You to John Mnyika For This Useful Post: mpaka kieleweke (26th July 200, Mzee Mwanakijiji (25th July 200, wembemkali (28th July 200
 
Nimesoma taratibu na kuona tatizo la Jmushi ni nini; Ni wazi kauli hii ndio msingi wa madai yake:

Ewe Mtemi Meli, uliowashinda wadachi mpaka mwenzio Sina alipokusaliti hatimaye wewe na mashujaa wenzako mkamwaga damu kaskazini mkilinda uhuru.

Sasa kwa mtu anayesoma anaweza kuelewa kitu kimoja kuhusu kauli hii ya Mnyika.

a. Kwamba Mangi Sina alimsaliti Mangi Meli.
b. Usaliti huo inawezekana kuwa kulikuwa na kitu wafanye (Sina na Meli) ambacho mmoja wao aliendelea kukifanya au aliacha kukifanya na mwingine akaona amegeukwa.

Sasa vyovyote vile, jibu la swali la Jmushi liko kwenye historia. Inaonekana Mnyika amesema kitu ambacho ni kama accepted historical fact kuwa Mangi Sina alimsaliti Mangi Meli.

Hivyo, ni jukumu la Mushi sasa kwenda kwenye historia na kumuonesha Mnyika kuwa hilo si kweli; siyo kutaka maelezo ya Chadema, Mnyika, na watu waliosema "thanks" kwa Mnyika kwa post yake nzima na siyo kamstari kamoja.

Jmushi, fanya research nyepesi tu uoneshe kuwa hakukuwa na usaliti kati ya Meli na Sina na Mnyika ataonesha wa kwake.
 
Wachagga kutoka Rombo asili yao ni Kenya, wachagga wa Marangu asili yao ni Kenya kabila la kikuyu, Wachagga wa Machame asili yao ni wamasai,wachagga wa Rombo useri asili yao ni wakamba kutoka kenya, n.k...
 
Nimesoma hili:

Mangi Sina of Kibosho
in the same area, [Kilimanjaro region] and in permanent competition with Mangi Rindi, Mangi Sina had by 1870 developed a great large army and was active in agriculture and cattle raids. He was still in control of his empire at the unfortunate arrival of the Germans in 1891, which broke down most of Chagga lifestyle through "colonisation".


Rindi
Mangi Rindi of the a subgroup of the Chagga was another major chief ruling in the Kilimanjaro region in 1860, making the now, city of Moshi an important base for ivory and game trading with Zanzibar. He manipulated and signed a Treaty with the Germans in 1885 and the cityMoshi became their headquarters and most important economic and political centre. - Wikipedia..
 
Nimesoma taratibu na kuona tatizo la Jmushi ni nini; Ni wazi kauli hii ndio msingi wa madai yake:



Sasa kwa mtu anayesoma anaweza kuelewa kitu kimoja kuhusu kauli hii ya Mnyika.

a. Kwamba Mangi Sina alimsaliti Mangi Meli.
b. Usaliti huo inawezekana kuwa kulikuwa na kitu wafanye (Sina na Meli) ambacho mmoja wao aliendelea kukifanya au aliacha kukifanya na mwingine akaona amegeukwa.

Sasa vyovyote vile, jibu la swali la Jmushi liko kwenye historia. Inaonekana Mnyika amesema kitu ambacho ni kama accepted historical fact kuwa Mangi Sina alimsaliti Mangi Meli.

Hivyo, ni jukumu la Mushi sasa kwenda kwenye historia na kumuonesha Mnyika kuwa hilo si kweli; siyo kutaka maelezo ya Chadema, Mnyika, na watu waliosema "thanks" kwa Mnyika kwa post yake nzima na siyo kamstari kamoja.

Jmushi, fanya research nyepesi tu uoneshe kuwa hakukuwa na usaliti kati ya Meli na Sina na Mnyika ataonesha wa kwake.

Mzee MKJJ Shukran...Naona hujafurahishwa mimi kusema umekubali kuwa Sina ni msaliti kwa kutowa asante baada ya maelezo kuwa Sina alimsaliti Meli hadi akamwaga damu.
Naomba kuelimishwa kwenye hilo...Na ndio maana halisi ya mada hii...Kauli ya kutaka kunifanya nionekane sijasoma historia si nzuri.
Ila tunaweza tukaelimishana kwa manufaa yetu wenyewe na kizazi kijacho...Ni muhimu kujuwa historia ili kutambuwa tulikotoka...Tulipo...Na ni direction gani tuchukuwe towards THE FUTURE.
 
Back
Top Bottom