FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 92,881
- 109,188
Ubishi mwingine hata hauna maana yoyote, kama kitu hukijui lazima uchangie?
Inafahamika mavazi rasmi ya wanaume waislamu ni kanzu. Sasa watamfundishaje mwalimu kuvaa vazi ambalo hata wao wenyewe hawalivai? Nyerere kuvaa kaptula unashangaa nini wakati ndiyo ilikuwa sare ya wafanyakazi wa serikali enzi za mkoloni.
Soma vizuri historia utaona kwamba kaptula ndio yalikuwa mavazi rasmi ya kiofisi enzi hizo, sio unabisha ilimradi uonekane unajua kumbe huelewi kitu!
Lilikuwa sio vazi rasmi bali ni umwanjomwanjo wa kutaka ujulikane kuwa unafanya kazi kwa wazungu. Kwengine lilikuwa uniform. Kwa Nyerere kama ilikuwa ni "official" au "un official" alikuja Dar na kaptura, sijui kuna tatizo lipi mnaloliona kama alikuja Dar na kaptura na hapo ndipo alipovuliwa hiyo kaptura, wazee waliovaa kaptura Dar walizivaa kwa occassion zake na si kila pahala na kila wakati kama ilivyokuwa kwa Nyerere, ndio lilikuwa vazi lake kabla ya kuvuliwa.
Kama ni usomi kuvaa kaptura kwa wakati huo basi tusikatae kama alikuwa hajavaa kaptura na tusikatae kuwa alivuliwa hizo kaptura na wazee wa Dar. Sioni cha kubisha ni nini hapo, whatever reasons may be the answer will remain to be kavuliwa kaptura na wazee wa Dar.