Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Ubishi mwingine hata hauna maana yoyote, kama kitu hukijui lazima uchangie?

Inafahamika mavazi rasmi ya wanaume waislamu ni kanzu. Sasa watamfundishaje mwalimu kuvaa vazi ambalo hata wao wenyewe hawalivai? Nyerere kuvaa kaptula unashangaa nini wakati ndiyo ilikuwa sare ya wafanyakazi wa serikali enzi za mkoloni.

Soma vizuri historia utaona kwamba kaptula ndio yalikuwa mavazi rasmi ya kiofisi enzi hizo, sio unabisha ilimradi uonekane unajua kumbe huelewi kitu!

Lilikuwa sio vazi rasmi bali ni umwanjomwanjo wa kutaka ujulikane kuwa unafanya kazi kwa wazungu. Kwengine lilikuwa uniform. Kwa Nyerere kama ilikuwa ni "official" au "un official" alikuja Dar na kaptura, sijui kuna tatizo lipi mnaloliona kama alikuja Dar na kaptura na hapo ndipo alipovuliwa hiyo kaptura, wazee waliovaa kaptura Dar walizivaa kwa occassion zake na si kila pahala na kila wakati kama ilivyokuwa kwa Nyerere, ndio lilikuwa vazi lake kabla ya kuvuliwa.

Kama ni usomi kuvaa kaptura kwa wakati huo basi tusikatae kama alikuwa hajavaa kaptura na tusikatae kuwa alivuliwa hizo kaptura na wazee wa Dar. Sioni cha kubisha ni nini hapo, whatever reasons may be the answer will remain to be kavuliwa kaptura na wazee wa Dar.
 
Naona wengine hawataki tu kumuelewa Mag3. Ni hivi:
  1. Mwaka 1957, kulikuwa na watanganyika waafrika 8,665,336 nchi nzima.
  2. Wasukuma walikuwa asilimia 12.6 ya watanganyika waafrika, kwa hiyo walikuwana idadi ya 1,091,832.
  3. Mwaka huo huo, mji wa Dar es Salaam ulikuwa na watu 128,742; Tanga 38,053; Mwanza 19,877;Tabora 15,361; Moshi 13,726; Arusha 10,038 na Bukoba 5,276.
  4. Mwaka huo ni asilimia 4.4 ya wakazi wa Tanganyika ndio waliokuwa wanaishi mijini.
  5. Kutokana na ukweli huu, hao watu ambao Mohamed Said anawapigia debe waliokuwa wakiishi kwenye kitongoji kimoja tu cha mji wa Dar es Salaam wasingeweza kufanya lolote hata kama waswahili wote wa Dar es Salaam, Tanga na Tabora wangewaunga mkono.
  6. Miaka ile huku walikokuwa wakiishi watanganyika wengi, mswahili alikuwa anachukuliwa kama mtu asiyeweza kuaminika ndiyo maana wakina Sykes wasingeweza kuwashawishi watu wa huko kuungana nao. Mtu ambaye wangemwamini ni mshamba mwenzao na hasa kama atatambulishwa na watu wa kwao wanaowaamini. Mtu mwenye sifa hii alikuwa Julius Kambarage Nyerere na pengine Oscar Kambona. Sehemu za pwani, Bibi Titi Muhamed alichangia mno kuvuta wanawake na wame zao kuingia TANU.
Ndi maana, tunawashangaa watu wanaotaka kutuambia kuwa bila hao jamaa wa gerezani na misheni kota, mpambano usingefanikiwa. Ni matusi makubwa.

Amandla.....
Naomba kukuuliza maswali...wewe ni muingereza,mjerumani au mfaransa? Mswahili ni mtu wa aina gani kwa tafsiri yako?
 
Ndivyo nnavyo amini, kuwa alikuja hajui kuvaa suruali na hao wazee wa Dar. ndio waliomfunda. Lakini Mohamed Said kishasema tuyaache haya tuchukuwe hii fursa adhim kujuwa ukweli uko wapi na porojo ziko wapi.

Kwa vile ni imani siwezi kukupinga maana wapo wanaoamini kabisa kuwa mwezi umetengenezwa kwa jibini na kuwa yupo kiumbe ambaye nusu ni mtu na nusu samaki!
 
Duuuh!! Facts na research!!

Kwanza sensa siyo fact, ni estimate inayobase na raw data. TZ hatuna fact; kwa sababu hatuna true information kwa sababu hatuna IT. Facts unahitaji kuwa na IT in order kuwa na true information. Unaposema TZ kuna watu Million 40 ni estimate na SIYO facts. Population haina facts bali ina estimate.

Research ina base na credible sources ambazo walengwa wanazitumia kwa ajili ya kusatisfy their arguments. Wewe na wenzako, pamoja na Mwkjj mnatumia sources ambazo zina pro-Nyerere kusatisfy argument mnazoziweka.
Kama mngekuwa mnatumia sources ambazo hazina base ya upande mmoja, basi msingekuwa na ubishi na hoja ambazo MS anajaribu kuelezea. Sources za MS zipo credible zaidi kwa sababu anatumia information direct kutoka kwa wale walioshiriki ktk Uhuru.
Sources zenu, zipo upande mmoja kwa sababu mnatumia data kutoka serikalini, au Pro-Nyerere ambazo tayari zipo FILTER ktk kuelezea ukweli.
Niweke sawa na kwa lugha rahisi kabisa isiyoleta utata na kubadilli mada. Mlima kilimanjaro upo Tanzania- Facts.
Kwanini Klimanjaro, kagera na Mbeya watu wanaelimu kuliko sehemu nyingine- yatakauwa matokeo ya research.

Baada ya hapo nifafanulie Pro-Nyerere ni akina nani na je ndio Pro-TANU?

Maiaka 10 iliyopita CCM ilikuwa madhalimu walio kandamiza waislam. Hiyo kauli imeishia wapi? si ndio ilikuwa kauli mbiu ya kuunga mkono falsafa ya 'Haki- Sawa' ya CUF. Lini uswahiba umerudi na ni kwa historia gani tofauti na ile iliyowakandamiza.

Kama source za Mohamed ni credible kama unavyodai, kwanini hakumhoji Fundikira, Rais wa EAMWS na right hand man wa Nyerere?
Kwanini hakumhoji mama Maria Nyerere kuhusu samaki aliopelekewa na marhum mzee Kiyate.
Kwanini hakumhoji marhum Rajab Diwani na Kitundu mapema(anasema alifariki masaa machache kabla ya mahojiano).
Kwanini hamhoji Sakim Ahmed Salim au Butiku wa NF

Kama ni credible, kwanini asikanushe au kukubali ushiriki wa Wanawake wa Pare katika kuanzisha chem chem ya kisiasa.
Kwanini asikanushe au kukubali uwepo wa harakati nje ya Dar es salaam kama Mwanza n.k
Kwanini majina ya akina Kisenge na Mashambo waliokuwa na hadhi katika TANU hayajitokezi
Kama ni credible kwanini asihoji namba za mtihani wizara husika
Kwanini asihoji madiwani wa kariakoo na gerezani waliobadili majina ya wapigania uhuru.
Kwanini asimhoji Silvano aliyeandika kitabu anacho kinukuu mara zote
Kwanini hakumhoji marhum Kawawa kama mwislam na mshiriki wa Nyerere, na mbona ushiriki wa Kawawa kama kiongozi katika vyama vya wafanyakazi hauonekani licha ya kuwa alikuwa Mwislam.

Soma post yangu ya awali, Mohamed anakiri kwa maneno kuwa 'anahadithia' maneno aliyosikia ili aweke sawa historia ya Waislam. Amekiri hivyo, sasa wewe unaposema ya Tanganyika umeitoa wapi zaidi ya Mohamed wenyewe.

Nina uhakika hujasoma vitabu vya Mohamed au makala zake. Nasema hivi kwasababu ametumia neno 'Inasemekana' mara nyingi sana. Credibility ya source zake iko wapi?

Unaweza kuwa na credible source halafu useme inasemekana!!! Inasemekana kutoka kwa nani maana yeye amesikia na hivyo ilipaswa aseme nimeambiwa. Ukishasema 'inasemekana' hiyo ni third party. Credibility ipo wapi.

Narudia, data na info zingine tunazofanyia kazi zimeletwa na 'credible' source kama aliyofanya Mohamed na Mdondoaji. Kwanini tulaumiwe kwa kuuliza au kuhoji.
 
Vazi la watu wa pwani likijulikana na unalijuwa, kuvaa kaptura haikuwa fashion kama unavyotaka ieleweke au ni maendeleo, hapana. Ilikuwa ni vazi la wafanyakazi kwa wazungu uwe msomi au si msomi. Kumbuka kufanya kazi kwa mzungu wakati huo ilikuwa tayari "brain washed" kuwa ni sifa, na utajitofautisha vipi kuwa wewe ni mfanyakazi wa Mzungu> uvae kaptura. Wazee wangu ni watu wa Dar na sijawaonapo wakivaa kaptura makazini mwao. Na hao wazee wa Dar. walikuwa wakitoka tu makazini huzivuwa hizo kaptura, wataendaje msikitini na kaptura?

Naomba turudi kwenye mada, lakini hili la kaptura nna uhakika nalo lilikuwa ni umanamba na "identity" ya ufanya kazi kwa wazungu. Sio Fashion.

Sasa kama unafahamu kwamba wazee wako wa dsm nao walikuiwa wanavaa kaptura isipokuwa walizivua ili waingie msikitini(hapa bila shaka walivaa kanzu na si suruali). Kwahiyo hoja ya Nyerere kuvaa kaptura inakuwa na uzito gani kama ilikuwa ndo uniform enzi hizo na hata wazee wako walivaa?

Kama mnajenga hoja ya Nyerere kuvaa kaptura ilikuwa ni ushamba au identity ya umanamba basi hata wazee wako wa dsm nao walikuwa manamba!
 
Lilikuwa sio vazi rasmi bali ni umwanjomwanjo wa kutaka ujulikane kuwa unafanya kazi kwa wazungu. Kwengine lilikuwa uniform. Kwa Nyerere kama ilikuwa ni "official" au "un official" alikuja Dar na kaptura, sijui kuna tatizo lipi mnaloliona kama alikuja Dar na kaptura na hapo ndipo alipovuliwa hiyo kaptura, wazee waliovaa kaptura Dar walizivaa kwa occassion zake na si kila pahala na kila wakati kama ilivyokuwa kwa Nyerere, ndio lilikuwa vazi lake kabla ya kuvuliwa.

Kama ni usomi kuvaa kaptura kwa wakati huo basi tusikatae kama alikuwa hajavaa kaptura na tusikatae kuwa alivuliwa hizo kaptura na wazee wa Dar. Sioni cha kubisha ni nini hapo, whatever reasons may be the answer will remain to be kavuliwa kaptura na wazee wa Dar.

Yani wewe unatapatapa na historia ya wazee wa gerezani dsm, unafinyangafinyanga tu hata hueleweki.

Wazee wako waliokuwa wakivaa kanzu na misuli walipata wapi ujasiri wa kumfundisha Nyerere kuvaa suruali ambayo wao wenyewe hawaivai?
 
Sasa kama unafahamu kwamba wazee wako wa dsm nao walikuiwa wanavaa kaptura isipokuwa walizivua ili waingie msikitini(hapa bila shaka walivaa kanzu na si suruali). Kwahiyo hoja ya Nyerere kuvaa kaptura inakuwa na uzito gani kama ilikuwa ndo uniform enzi hizo na hata wazee wako walivaa?

Kama mnajenga hoja ya Nyerere kuvaa kaptura ilikuwa ni ushamba au identity ya umanamba basi hata wazee wako wa dsm nao walikuwa manamba!

Sababu yote uiletayo iwe ndio hivyo, ukweli utabaki kuwa Nyerere kaja na Kaptura na ukweli utabaki wazee wa Dar ndio waliomvuwa kaptura amma kwa kupenda kwake amma kwa kutokupenda kwake, waliomuona akija Dar enzi hizo walimuona kaja na kaptura.

Sioni kuna tatizo lipi ikiwa Rais wa kwanza wa Tanzania ikijulikana kuwa alikuja Dar na kaptura? Tunaongelea Historia hapa na ushahidi wa picha nimeuweka hapo juu, wenzake wooote wakiwa na suruali yeye alikuwa kavaa kaptura. Rejea picha hapo juu. Na wala sijasema kuwa wazee wote wa Dar walikuwa hawavai kaptura, nimesema wako waliokuwa wakizivaa kwa (occassion) munasaba unaohusiana na kuvaa kaptura, amma makazini kwao amma kwa kujionesha kuwa wanafanya kazi kwa wazungu. Nyerere alikuja Dar na kaptura na wazee wa Dar wakamvuwa kaptura. Kuna uwezekano kuwa ilikuwa haina haja tena ya kuji "identify" kama ni mfanya kazi wa wazungu kwa maslahi ya kugombea madaraka, Jee, tatizo ni lipi? Historia ibaki kuwa historia ya ukweli na hili la kaptura lina ushahidi kamili.
 

Mwanakijiji,

Maneno ya kumkashifu Nyerere yalikuja baadae sana na yalitokana
na watu waliompokea Dar es Salaam wakawanae baga kwa bega
hadi akafika alipofika.

Baada ya hapo ikawa sasa Nyerere kasahau hisani aliyotendewa.
Akawa anasikika akisema yeye kaikuta TAA imekufa akaifufua,
Dossa alikuwa akimwendesha, TAA kilikuwa chama cha starehe.

Nyerere mwaka 1963 akalivunja Baraza la Wazee wa TANU chini ya
uenyekiti wa Iddi Tulio. Nyerere akawakamata masheikh wengine
hata hawakuwa katika siasa kama Maalim Matar (rafiki kipenzi wa
Abdulwahid) akawatia kizuizini kwa kosa la "kuchanganya dini na siasa."

Nyerere akavunja jumuia za Kiislam kama EAMWS, Al Jamiatul Ismaiyya na
nyinginezo.

Wazee wakapigwa marufuku hata kufika TANU office kama wenyewe
walivyopenda kuita.

Nyerere akajiweka mbali na wale wazee na watu wengine aliokuwanao
katika harakati.

Iddi Tulio kagongwa na gari kafa. Nyerere hakuhudhura maziko yake.
Mshume Kiyate kaugua hadi kafa hakwenda hospitali wala hakuhudhuria
mazishi yake, Sheikh Mohamed`Ramia, Jumbe Tambaza...

Wazee wetu hawakupendezwa na mambo haya.

Chuki ikajengeka dhidi yake.

"Huyu si huyu Nyerere aliyeletwa kwetu na Abdu Sykes kavaa kaptula?

Wazee wakawa wakikutana pembeni wanazungumza lugha hizo.

Ndiyo hadi leo tumefika hapa.

Ni mengi tutaelezana taratibu.

Kila jambo lina sababu yake.

Mohamed
Mohamed,
Mwalimu aliweka ndani watu wengi tu. Sio hao "Waislamu" wako uliowataja pekee. Kwa nini hauwataji hao wengine wenye majina ya kikristo nadhani ni katika kuimarisha hoja yako. Jana, katika kipindi cha WOSIA WA BABA, katika moja ya hotuba zake nzuri, Mwalimu alieleza jinsi alivyoifahamu TAA na hatimaye kujiunga nayo kupitia kwa mzee mmoja aliyeitwa Mwangosi na Mzee KaselaBantu ambao wewe hauwataji sana wala kuwapa uzito kama akina Sykes.
Punguza UDINI na chuki zako kwa Mwalimu. Historia ya nchi hii haikupi nafasi uibadili na hatimaye ukubali kwamba Mwalimu ndiye alikuwa Rais wa Kwanza wa Tanganyika na hatimaye Tanzania. Labda nikuulize swali moja Mohamed; ulipata kuonana na kuongea na Mwalimu ukamuuliza juu ya haya unayoyasimulia?
 
Yani wewe unatapatapa na historia ya wazee wa gerezani dsm, unafinyangafinyanga tu hata hueleweki.

Wazee wako waliokuwa wakivaa kanzu na misuli walipata wapi ujasiri wa kumfundisha Nyerere kuvaa suruali ambayo wao wenyewe hawaivai?

Tazama picha hapo juu halafu useme ni nini hicho? Usiandikie mate na wino upo, wangapi katika hiyo picha waliovaa kaptura? mimi namuona mmoja tu "The Odd one out" Nyerere.
 
ujinga uliokuwepo hapa ni kutanabaisha dini na harakati za uhuru badala kutanabaisha watu, kama alivyo sema mwana kijiji, ukiongelea pwani wakati huo wengi wao walikuwa waislamu, mbeya wanyakyusa na wasafa, iringa wahehe na wabena, ukienda tabora wnyamwezi(wengine wakatoliki, waislamu, wapagani, morovian) nk
na kama nia ni kuongelea dhuluma, basi ni vizuri mtu aseme tu kwamba watu wa pwani walinyimwa shule, halafu watu wanao dai shule za agakhan zilikuwa za waislamu ni watu wa kuchekesha saana, kwani ile shule ni kwa ajili ya waismailia na si waislamu wa ngozi nyeusi, na hata leo hii ukienda pale utaona hao waisimaili ndio idadi kubwa 80% then wanafuatia wengine iwe mpagani, kafiri na muislamu (sunni au Shia)
ukija uelewa wa hao wazee wangu wa gerezani, labda kutokana na mawasiliano ya redio simu, tv, nk mtu alikuwa hajafika mza, tabora, pare, meru, moshi nk, yeye atakacho kiona kizuri ni kile anacho kiona na bahati mbaya au nzuri wazee wangu wa gerezani walikuwa wanawaona wana gerezani wenzao tu, ni sawa sawa na mtu mweupe/mzungu ambaye hajafika afrika anapokuwa na dhana kwamba weusi tunaishi juu ya mti.
baru baru anazungumzia mwandishi bora ni yule anaye weka reference, lakini hiyo reference inatakiwa isiwe biased, kwa mfano mwandishi kaongea na wazee wakee gerezani, je baada ya hapo kaenda kuhoji wengine? au sample yake ndio hiyo biased? halafu lengo lake ni nini? kurekebisha historia iliyo pindishwa au ambayo haija tambua mchango wa blah blah blah? je historia ya nchii hii haiwatambui sykes au Abdulwahid in particular? je historia haimtambui Bibi Titi?
 
Tazama picha hapo juu halafu useme ni nini hicho? Usiandikie mate na wino upo, wangapi katika hiyo picha waliovaa kaptura? mimi namuona mmoja tu "The Odd one out" Nyerere.
Faiza,
Naamini wewe ni zaidi ya hii hoja ya Nyerere na kaptula.
 
Faiza,
Naamini wewe ni zaidi ya hii hoja ya Nyerere na kaptula.

Mkuu hiyo picha imewekwa purposely, kuna watu hapa wanajaribu kwa kila njia kuonyesha kwamba Nyerere si lolote wala chochote bila wazee wa dsm.

Na mzee mohamed amesema hapa kwamba hoja ya Nyerere na kaptura ilianzishwa na wazee wa dsm baada ya uhuru ikiwa ni dhihaka kwa Nyerere kutokana na hisia kwamba Nyerere ana chuki na uislamu na waislamu.

Ni picha ngapi alipiga Nyerere pamoja na wapigania uhuru wengine lakini mbona haziwekwi hapa?

Anyway tuendelee na mambo mengine hili la kaptura linaeleweka na si hoja ya msingi.
 
Huyo shehe wako kakudanganya, mimi ninavyo wajua waisilamu hawana mchezo wakidai hoja yao hatakama haina msingi, wako tayari hatakufa kusimamia anochokiamini hata kama ni ushenzi, yuko teyari kukuua ili usimsumbue, kama huyo shehe wako angekuwa hai nadhani kwa sasa angeshakuwa chriatian tena born again.

Siku hizi kuna usemi unaosema pata pesa tujue tabia yako lakini zamani kulikuwa na usemi usemao fungua kinywa chako tujue upeo wako. Asante kwa kutujulisha wewe ni nani
 
Confidence comes not from always being right but from NOT FEARING TO BE WRONG: Peter T. mcintyre

Kitu kimoja nilicho na hakika nacho kwa asilimia 100% ni kwamba wale wote wenye mapenzi ya kweli kwa taifa letu la Tanzania wanasita sana kuchangia hii hoja inayofinyangwafinyangwa na huyu anayejiita Mohamed Said. Bila kumung'unya maneno nayaita madai ya Mohamed Said la kutoa elimu ya historia ya kweli ni porojo hatari iliyojaa uchochezi ambayo lengo lake hasa ni kuleta uhasama wa kidini miongoni mwa wananchi. Sijui anachotegemea kufaidika nacho kwa kupanda hii mbegu ya hatari ambayo nina hakika mtu kama Mohamed Said anajua fika madhara yake.

Mohamed Said ni kama kipofu ambaye baada ya kusimuliwa na wazee kwamba tembo ni mnyama mkubwa kuliko wanyama wengi anapata nafasi ya kumpapasa tembo. Kwa bahati mbaya anaupapasa mguu wa tembo na si mwili wote halafu katika imani yake anadai anao uwezo wa kutoa somo kuhusu umbo la mnyama tembo na ushuhuda wake, kuwa tembo ni kama gogo la mti mkubwa, ndio ukweli na anayesema tofauti hajui kitu. Watu wote wanaolalamikiwa na Mohamed Said kuwa walisahauliwa, wengi wao walikuwa wakazi wa Dar es Salaam eneo la Gerezani.

Kabla ya uhuru Tanganyika iligawanywa katika majimbo makuu manane na katika majimbo yote hayo, jimbo la pwani kwa ujumla lilikuwa moja ya majimbo yaliyokuwa nyuma kimaendeleo kiuchumi, kielimu na kisiasa na hiyo ni licha ya kuwa makao makuu ya serikali ya kikoloni yalikuwa Dar es Salaam. TAA ilianzishwa na watumishi wa serikali (civil servants) na kwa wakati wote kazi kubwa ya TAA ilikuwa ni kulalamika ikidai haki ya wafanyakazi bila upendeleo na hasa ubaguzi wa rangi katila utumishi kubwa ukiwa uonevu dhidi ya wazawa, mtu mweusi.

Jimbo la Ziwa ni moja ya majimbo yaliyokuwa mbele kiuchumi, kielimu na kisiasa na kama kuna kitu kinaweza kudaiwa kuwa kilisahaulika katika harakati ya kupigania uhuru ni mchango wa Jimbo la Ziwa (Bukoba, Mwanza, Mara na Shinyanga) Jimbo la Ziwa ndilo lililoongoza kwa idadi ya watu, idadi ya makabila, idadi ya mali asili na idadi ya machifu ambao nafasi yao ilikuwa kubwa tu katika kuhamasisha watu. Moja wa watu ambao mchango wao nitautaja kidogo tu ingawa alifanya jitihada kubwa labda zaidi ya wazee wa Mohamed Said ni Paul "Kishamapanda" Bomani.



Historia ya harakati za uhuru ni zaidi ya porojo za Mohamed Said, watu walipigania uhuru kama Watanganyika na bila kubaguana kikabila, kidini wala kijinsia. Ndio maana mimi sitaki kabisa kuwa na majibizano na huyu Mohamed Said moja kwa moja ila kwa kuwa hoja ileletwa JF, akae tayari kupewa somo kuhusu umbile zima la mnyama tembo na sio mguu moja wa tembo alioupapasa. Hapa mimi nitaongea sana kuhusu mchango wa Jimbo la Ziwa na baadaye kuonyesha jinsi maadui wa nchi yetu wanavyowatumia kidini watu kama huyu Mohamed Said.



Baadaye nitaeleza jinsi Mkoa wa Mara yenye makabila karibu hamsini yalivyoweza kushirikiana bila mfarakano na kuitikia mwito wa Mwalimu Nyerere katika hizo harakati za kudai uhuru. Je mwamko wa wakazi wa jimbo la Ziwa ulikuwaje na mapokezi gani aliyapata kila wakati Mwalimu aliporudi kwenye hili jimbo ambalo idadi ya wakazi wake kwenye miaka ya 50s ilikuwa mara tatu ya majimbo mengi Tanganyika kama Pwani. Pia nitaonyesha ni wakati gani walianza kuyasikia hayo majina anayodai Mohamed Said ya wazee wa Gerezani Dar es Salaam !
 
Kwa vile ni imani siwezi kukupinga maana wapo wanaoamini kabisa kuwa mwezi umetengenezwa kwa jibini na kuwa yupo kiumbe ambaye nusu ni mtu na nusu samaki!

Kweli kabisa wala si uongo na picha huwepo za huo mwezi wa jibini kama ilivyo picha ya Nyerere hapo juu na kaptura katika kundi la watu waliovaa sarawili.
 
Asante Mungu JF inaelekea kurudi kwenye hadhi yake mijadala ya aina hii ndiyo ilinifanya nikajiunga na hili jamvi lakini kuanzia mwaka 2010 tulivamiwa na kundi la wahuni wasiopenda mijadala yenye afya bali matusi na kejeli.

Mzee Mohamed Said,Fundi Mchundo,Jasusi,FaidaFoxy,WildCard,Mzee Mwanakijiji,Mwita Maranya,Nguruvi3,Mag3 na wengine wote niliowasahau kwa bahati mbaya tafadhali sana tujiepushe na lugha za kuudhi,kejeli au matusi kwa faida ya mjadala.Niseme kweli nimejifunza mambo mengi kupitia kwenu na nina hakika wako wengi pia kupitia michango yenu wamefaidika sana.
 
ujinga uliokuwepo hapa ni kutanabaisha dini na harakati za uhuru badala kutanabaisha watu, kama alivyo sema mwana kijiji, ukiongelea pwani wakati huo wengi wao walikuwa waislamu, mbeya wanyakyusa na wasafa, iringa wahehe na wabena, ukienda tabora wnyamwezi(wengine wakatoliki, waislamu, wapagani, morovian) nk
na kama nia ni kuongelea dhuluma, basi ni vizuri mtu aseme tu kwamba watu wa pwani walinyimwa shule, halafu watu wanao dai shule za agakhan zilikuwa za waislamu ni watu wa kuchekesha saana, kwani ile shule ni kwa ajili ya waismailia na si waislamu wa ngozi nyeusi, na hata leo hii ukienda pale utaona hao waisimaili ndio idadi kubwa 80% then wanafuatia wengine iwe mpagani, kafiri na muislamu (sunni au Shia)
ukija uelewa wa hao wazee wangu wa gerezani, labda kutokana na mawasiliano ya redio simu, tv, nk mtu alikuwa hajafika mza, tabora, pare, meru, moshi nk, yeye atakacho kiona kizuri ni kile anacho kiona na bahati mbaya au nzuri wazee wangu wa gerezani walikuwa wanawaona wana gerezani wenzao tu, ni sawa sawa na mtu mweupe/mzungu ambaye hajafika afrika anapokuwa na dhana kwamba weusi tunaishi juu ya mti.
baru baru anazungumzia mwandishi bora ni yule anaye weka reference, lakini hiyo reference inatakiwa isiwe biased, kwa mfano mwandishi kaongea na wazee wakee gerezani, je baada ya hapo kaenda kuhoji wengine? au sample yake ndio hiyo biased? halafu lengo lake ni nini? kurekebisha historia iliyo pindishwa au ambayo haija tambua mchango wa blah blah blah? je historia ya nchii hii haiwatambui sykes au Abdulwahid in particular? je historia haimtambui Bibi Titi?

Jamani kuna tatizo hapa, ishu sio kuyakataa anayosema Mohamed, ishu ni kuwa yapo mengi kuhusu taifa hili ambayo hatuyajui na yanajulikana na wachache miongoni mwetu. Basi kila mmoja aliandike lake analolifahamu ile wengine nao pia wapate kufahamu na pengine kujua Nyerere aliyakuasanyaje yote hayo pamoja akayazika na kujenga taifa lisilo na historia ndogondogo labda ambazo zisingetuwezesha kuwa wamoja kama tulivyo leo. Kama yapo yasemwe, yaandikwe tuyafahamu na eti si kumwambia mwingine asiseme kwa kuwa wewe hujayasema unayoyafahamu. Ajabu na kweli hata Bibi Titi Mohamed nae ametoa malalamiko ya kusahauliwa waliopigania uhuru kikwelikweli. Malalamiko yake yapo katika kitabu chake kiitwacho WANAWAKE WA TANU, kilichochapishwa na E&D VISION PUBLISHER kikiwa kimedhamioniwa na TGNP. Ukiemda E&D pale Afrika Sana Sinza utakipata au ukienda TGNP utakipata. Kama hata BIBI TITI alilalamika ni wazi kuna tatizo hapa. Kuna Tatizo kama lile alilolizungumza Jaramongi Odinga katika Not Yet Uhuru na kuna Tatizo kama lile alilochagiza Ngugi katika vitabu vyake A grain of Wheat na MATIGARI. Tufungue macho tuone ni jinsi gani tutaweza kuliingiza hili ndani yetu na kusema hili ni tatizo kisha tulitafutie tiba. Hatuwezi kulitibu kama hatujajua hili ni tatizo
 
Asante Mungu JF inaelekea kurudi kwenye hadhi yake mijadala ya aina hii ndiyo ilinifanya nikajiunga na hili jamvi lakini kuanzia mwaka 2010 tulivamiwa na kundi la wahuni wasiopenda mijadala yenye afya bali matusi na kejeli.

Mzee Mohamed Said,Fundi Mchundo,Jasusi,FaidaFoxy,WildCard,Mzee Mwanakijiji,Mwita Maranya,Nguruvi3,Mag3 na wengine wote niliowasahau kwa bahati mbaya tafadhali sana tujiepushe na lugha za kuudhi,kejeli au matusi kwa faida ya mjadala.Niseme kweli nimejifunza mambo mengi kupitia kwenu na nina hakika wako wengi pia kupitia michango yenu wamefaidika sana.


Ngongo,

Tuko pamoja binafsi Insha Allah nitaeleza yote kama nilivyoyapokea kutoka
kwa wazee wangu na kama nilivyojifunza kwa lugha safi na ya kupendeza.

Naya fanya haya yote kwa heshima ya wazee wangu ambao wengi wametangulia
mbele ya haki.

Nina hakika wagelikuwa hai wangefurahi kuwa mwishowe historia yao ilikuja andikwa.

Mohamed
 
Mohamed,
Mwalimu aliweka ndani watu wengi tu. Sio hao "Waislamu" wako uliowataja pekee. Kwa nini hauwataji hao wengine wenye majina ya kikristo nadhani ni katika kuimarisha hoja yako. Jana, katika kipindi cha WOSIA WA BABA, katika moja ya hotuba zake nzuri, Mwalimu alieleza jinsi alivyoifahamu TAA na hatimaye kujiunga nayo kupitia kwa mzee mmoja aliyeitwa Mwangosi na Mzee KaselaBantu ambao wewe hauwataji sana wala kuwapa uzito kama akina Sykes.
Punguza UDINI na chuki zako kwa Mwalimu. Historia ya nchi hii haikupi nafasi uibadili na hatimaye ukubali kwamba Mwalimu ndiye alikuwa Rais wa Kwanza wa Tanganyika na hatimaye Tanzania. Labda nikuulize swali moja Mohamed; ulipata kuonana na kuongea na Mwalimu ukamuuliza juu ya haya unayoyasimulia?

WC,

Sina chuki na Nyerere.

Nishasema hapa jamvini mara kadhaa kuwa ikiwa utachangia bila
kuwa umesoma kitabu changu utaja uliza mambo ambayo kama
ungelisoma kitabu usingeliuliza.

Kama umesoma na umesahau basi kirudie tena na nenda kwenye
faharasha.

Kwenye name index utayakuta majina mengi sana.

Ama kuhusu hilo la Nyerere kuwa rais wa kwanza wa nchi yetu vipi
nitalikataa?

Nalosema mimi ni kuwa ipo historia nyingine ambayo haikuandikwa
na kwa kuwa haifahamiki kuna sifa kapewa Nyerere si zake.

Hazimstahili na kusema hivyo si kuwa nina chuki na yeye.

Mohamed
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom