Historia ya udhalimu ikihifadhiwa ni silaha kwa aliyedhulumiwa na huwa funzo jema kwa dhalimu

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,887
30,232
HISTORIA YA UDHALIMU IKIHIFADHIWA NI SILAHA KWA ALIYEDHULUMIWA NA HUWA FUNZO JEMA KWA DHALIMU

Mgahawa mpya ulitangazwa kuwa utafuguliwa tarehe kadhaa na ukawa unafanyiwa matangazo katika gazeti maarufu mjini Tel Aviv na tangazo likawa limetiwa kila aina ya maneno ya kuvutia wakisema, ‘’Watch This Page,’’ yaani usikose kuangalia ukurasa huu na tangazo lilikuwa na ukurasa mzima katikati ya gazeti sehemu ambayo msomaji hatakosa kufungua.

Ikawa hivyo kwa mwezi mzima na kila tangazo linawekewa nakshi, maandishi na picha za kuvutia huku siku zikihesaiwa kuwa leo zimebakia siku 5 mgahawa kufunguliwa siku ya pili tangazo litanadi zimebaki siku 4 mgahawa kufunguliwa na hivyo, hivyo tangazo likawa kila siku hadi ikabaki siku 1 na kuongezea, ‘’Kesho ndiyo siku yenyewe ya ufunguzi.’’

Hapo pakawekwa tangazo kuwa kwa watu 100 watakaopata kifungua kinywa hapo baina ya muda wa chai na chakula cha mchana mgawaha utakapofunguliwa watakula bure na watapewa zawadi ambayo haikutajwa na watapewa mwaliko maalum wa kuja kula chakula cha jioni na wake au waume zao.

Haya yote yatafanywa kwa ‘’rotary,’’ baina ya wakati wa chai asubuhi na chakula cha mchana.
Hata kabla hakujaanuka sawasawa muda wa kufungua mgahawa haujafika mtaa ukawa kama vile umevamiwa.

Pembeni ya mtaa karibu kabisa na mgahawa liliegesha gari la televisheni mtu wa camera akijaribu kupata picha zilizokuwa zinarushwa mubashara.

Jambo kama hili lilikuwa halijapata kutokea popote katika kumbukumbu za wakazi wa Tel Aviv.

Kweli kumekuwa na matangazo kama haya ya kuvutia biashara lakini hili lilikuwa limefurtu ada.

Kulikwa na uvumi kama kawaida ya miji mikubwa kuwa itatolewa zawadi ya dola za Marekani 10,000.00.

Muda wa kufungua mgahawa ukafika.

Mgahawa huu haukuwa umeelezwa jina lake.
Watu wakawa wamejipanga tayari kwa ufunguzi na kuingia ndani ya mgahawa.

Kabla ya kufungua milango mtangazaji akatawatangazia waliokuwapo kuwa watu wataingia baada ya kupachika bao lenye jina la mgahawa.

Mbele ya mlango palikuwa na wasichana warembo wamevaa vizuri wanasubiri kukaribisha watu.

Wakatokea watu wawili wamevaa nguo za wajenzi kichwani wana ‘’helmet,’’ yaani kofia ngumu na mabuti wakapanda zile ngazi kila upande wa mlango wamebeba bao limefunikwa kwa kitambaa cha hariri cheupe wakapanda ngazi zilizokuwa pembeni wakatundika bao na kwa haraka wakashuka chini.

Wakaja wasichana warembo wawili wakashika kamba huku na huku wakavuta na jina la mgahawa likaonekana likiwa katika maandishi ya makubwa meusi kwenye ubao mweupe.

Jina la mgawaha lilikuwa moja tu, ‘’Auschwitz.’’

Ulipigwa ukimya kwa sekunde ikawa kama vile wale waliofika pale wametokewa na zimwi mla watu anataka kuwatoa roho.

Wapiga picha walizubaa kwa sekunde chache kisha ghafla ikawajia kuwa wapo mbele ya tukio kubwa na kwa ghafla vilevile kama walivyoshtuka na kusita kupiga picha milio ya camera zikasika mianga ya camera ikikimbizana na kufanya kivuli na mwanga, kivuli na mwanga, kivuli na mwanga, camera zikatoka kwenye bao zikaelekezwa kwa watu wake kwa waume waliofika kwenye ufunguzi ule camera sasa zikiwa zimelengwa sura zao.

Wapigaji picha wale wenye uzoefu wa miaka na miaka wakijua kuwa tukio lile lote litabebwa na sura zilizopigwa na radi kali ya mshtuko wa yale yaliyokumbushwa na na yale waliofanyiwa wazee wao na Wajerumani Poland kwenye kambi iliyokuwa ’Auschwitz.’’

Milango ilikuwa wazi lakini hakuna aliyenyanyua mguu kuingia ndani ya mgahawa ule.

Kundi lile lililokuwa limejikusanya pale nje mbele ya mgahawa likawa sasa linarudi kinyume nyume, kimya kimya.

Ilichukua muda wa dakika mbili au tatu hivi kwa watu kurudi katika hali zao za kawaida.

Nyuma ikasikika sauti ya mtu akipiga ukelele, ‘’Vunja mgahawa huo, vunja!’’

Kama mashine ya saa inavyofanya kazi bao lilishushwa kwa haraka na mahali pale likapandishwa bao jingine kubwa mara mbili ya lile likiwa lineandikwa maneno haya, ‘’Hatujasahau!’’

Ikasikika sauti kutoka kipaza sauti kinapiga nyimbo maarufu ya Wayahudi, ‘Havanagila’’ na sauti ya msichana inaita,’’Karibuni ingieni ndani tunywe chai na tupongezane kwani tunastahili, baada ya miaka hii yote na vizazi kupita bado hatujasahau.’’

Taratibu watu wakawa wanaingia mgahawani na kabla hawajaingia ndani walikuwa wanafuta viatu vyao kwenye lile bao lililoandikwa, ’’Auschwitz.’’

Historia inayoishi kwa kukumbukwa ni silaha ya kuzuia dhulma ziliyofanywa na madhalimu kutorudiwa tena.

AUSCHWITZ.jpg
 
Kifalsafa unaweza kusema kuwa.

Mambo mabaya ukiwafanyia watu, hayatasahaulika kamwe vizazi hadi vizazi. Unaweza ukawafanyia watu au Inchi mema mengi sana lakini kamwe hayo hayawezi kufuta uovu uliowafanyia watu au Inchi.

Wanaokumbukwa daima milele ni wale wanaowatumikia watu kwa kuilinda haki yao ya kuishi na hata kukubali kufa kwa ajili ya wengine.

Pili, wanaokumbukwa daima milele ni wale wanaojali mahitaji ya kila siku ya wengine hasa chakula na mavazi.
Wale waumini wa Kikristo wanaposali sala ya Bwana husema " Utupe mkate/chakula chetu cha kila siku"

Yule Yusufu aliyepewa u waziri mkuu wa Misri na Farao, ilikuwa ni kwa ajili ya kukusanya chakula cha kuwalisha watu wakati wa njaa. Huyu anakumbukwa hadi leo kwa jina lake lakini Farao anakumbukwa kwa cheo chake na hapewi heshima kama Yusufu.

Mada hii inatoa angalizo kwa Viongozi wetu kuwa, ili wakumbukwe na waje wapate heshima kubwa baadaye ni kuhakikisha watu wanapata mlo wao wa kila siku kwa uhakika na kulinda uhai wao.
 
Mmmmmhhhhhhhhhh cjaelewa alieelewa anisaidie
Auschwitz iko Poland hapo kulikuwa na Gas Chambers ambako Wayahudi wengi waliuawa na Wajerumani wakati wa Vita Vya Pili Vya Dunia.

Hii ndiyo "holocust," na hakuna Myahudi asiyeijua historia hii.

BAKWATA hawataki historia yake ilivyoathiri Uislam ifahamike wanatuambia Waislam tuikubali Auschwitz na tuiunge mkono tusiwe watumwa wa historia.

Kuitaja historia ya Auschwitz kwao wao ni kufukua makaburi.

Nilihisi hii makala itawapa shida baadhi ya watu kuielewa.

Nadhani sasa umefahamu.
 
Mmmmmhhhhhhhhhh cjaelewa alieelewa anisaidie
Wakati wa utawala wa Adolf Hitler kule ujeruman,wayahudi waliteswa na kuuwawa katika kambi mbalimbali kama vile Auschwitz,Sobibor,nk .Hii iliktokea ujeruman na maeneo yote aliyoteka Hitler wakati wa vita kuu ya pili ya dunia na kote ambako aliungwa mkono.

Hii Ni katika mauaji ya kimbari yaliyojulikana Kama Holocaust.Lengo la kutumia jina la hiyo kambi dhalimu mjini Tel Aviv Ni kuwakumbusha wayahudi na ulimwengu hasa kizazi kipya kwamba ,Historia haiwezi kufutika hata iwe chungu namna gani.Historia iliyojaa uovu na udhalimu haiwezi kukubalika.
 
Laki...
Auschwitz ni kumbukumbu mbaya kwa Wayahudi.

BAKWATA ni kumbukumbu mbaya kwa Waislam wa Tanganyika.
Inawezekana mwanzo wa BAKWATA haukuwa mzuri, lakin bakwata ya sasa hivi imebadilika, inawaongoza waislamu vizuri kabisa, nakushauri uiunge mkono
 
inawezekana mwanzo wa BAKWATA haukuwa mzuri, lakin bakwata ya sasa hivi imebadilika, inawaongoza waislamu vizuri kabisa, nakushauri uiunge mkono

Laki,
Maneno hayo unayoniambia mimi Geogrey Sawaya aliyekuwa Director wa Criminal Investigation (DCI) alimwambia Bilal Rehani Waikela mwaka wa 1969 ndani ya chumba Tabora Hotel, Tabora kuwa aiunge mkono BAKWATA ili ikubalike Tabora na akatoa fedha za kifuta jasho 40,000.00 kumpa Waikela.

Mzee Waikela akakataa kupokea.
Kwenye mikoa mingine taarifa ni kuwa hizo fedha zilipokelewa.

Waikela akamuuliza Sawaya wapi hizo fedha zinatoka kupewa yeye?
Akamwambia wanaoikataa BAKWATA si yeye bali ni Waislam.

Waikela akinambia, ''Wewe Mohamed Allah amekuleta kwangu ili uwaeleze Waislam ukweli na mimi unitoe kwenye dhima.''

Hakika Mzee Waikela amenisomesha mengi.
 

Attachments

  • BILAL REHANI WAIKELA.jpg
    BILAL REHANI WAIKELA.jpg
    29.2 KB · Views: 1
Allah ampe umri mrefu mzee Bilal, wajina wa baba yangu. Mzee Mohammed nitapata wapi habari kuhusu BAKWATA na uanzishwaji wake/historian yake?
 
Tsh. 40,000/= mwaka 1969!!!!!!!!????

Zingine chai hizi
Laki,
Maneno hayo unayoniambia mimi Geogrey Sawaya aliyekuwa Director wa Criminal Investigation (DCI) alimwambia Bilal Rehani Waikela mwaka wa 1969 ndani ya chumba Tabora Hotel, Tabora kuwa aiunge mkono BAKWATA ili ikubalike Tabora na akatoa fedha za kifuta jasho 40,000.00 kumpa Waikela.

Mzee Waikela akakataa kupokea.
Kwenye mikoa mingine taarifa ni kuwa hizo fedha zilipokelewa.

Waikela akamuuliza Sawaya wapi hizo fedha zinatoka kupewa yeye?
Akamwambia wanaoikataa BAKWATA si yeye bali ni Waislam.

Waikela akinambia, ''Wewe Mohamed Allah amekuleta kwangu ili uwaeleze Waislam ukweli na mimi unitoe kwenye dhima.''

Hakika Mzee Waikela amenisomesha mengi.
 
Samahani mzee kwa lugha hiyo nimejikuta nimeitumia kwa kuwa ni kama kamsemo siku hizi

Kwa lugha ya kistaarabu nilimaanisha huo ni uongo, hiyo pesa ilikuwa kubwa sana, na halafu naambiwa hela kama hiyo ilitolewa mikoa mingine pia
T...
Huwa siingii katika ubishani wala simlazimishi mtu kuniamini.

Umenisikitisha tu kwa kunikejeli ati chai.
Ungekuwa mstaarabu ukasema hii si kweli.

Jibu ni lile lile lakini ndani ungeweka staha.
 
Samahani mzee kwa lugha hiyo nimejikuta nimeitumia kwa kuwa ni kama kamsemo siku hizi


Kwa lugha ya kistaarabu nilimaanisha huo ni uongo, hiyo pesa ilikuwa kubwa sana, na halafu naambiwa hela kama hiyo ilitolewa mikoa mingine pia
40,000 kwa mikoa 20 ni 800,000 ya mwaka 1969..

Mmh labda..
 
  • Thanks
Reactions: T11
Mzee wangu unapenda kuhubiri chuki sana kuliko upendo
Mind you chuki haitolewi na chuki bali upendo
Dawa ya moto ni maji sio moto.
 
Back
Top Bottom